TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, August 2, 2014

Dunia nzima lazima iifuate Azam Mbagala

Wachezaji wa Azam wakijadiliana jambo wakati wa mechi ya kirafiki dhidi ya Kombaini ya jeshi jana Ijumaa kwenye uwanja wa Azam Complex. Azam ilifungwa mabao 3-0. 
By DORIS MALIYAGA  (email the author)

Posted  Agosti2  2014  saa 12:13 PM
SHARE THIS STORY
0
Share

KATIKA kujiweka sawa, Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Bara  klabu ya Azam FC, itakipiga na Zesco ya Zambia Uwanja wa  Azam Complex Agosti 10 na imetamka rasmi kuwa itacheza  mechi zake zote za Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja  wao na siyo Taifa.
Katibu Mkuu wa Azam, Idrissa Nassor ameliambia Mwanaspoti  kuwa: “Baada ya mechi yetu na Mtibwa, tutacheza mechi ya  kirafiki na Zesco ya Zambia siku hiyo mipango yote  imeshakamilika.”
Muivory Coast  wa Azam, Kipre Tchetche ameondolewa  kikosini kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya shingo na  anatarajiwa kuanza mazoezi na wenzake, wiki ijayo.
Pia Mhaiti Leonel Saint-Preux anasumbuliwa na majeruhi  kwenye mguu wa kulia. Omog amesema: “Tchetche  nimempumzisha hadi wiki ijayo, anamatatizo mgongoni kwenye  shingo na Leonel hayuko vizuri nafikiri ataanza mazoezi na  wenzake kesho (leo),”alisema Omog. Azam leo itafanya  mazoezi ya ufukweni Coco.

No comments:

Post a Comment