TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 8, 2012

MIUNDOMBINU YA MIFUGO SOKO LA NYAMATALA MISUNGWI HAIJAKAMILIKA KUWA SOKO LA KIMATAIFA

Mwenyekiti wa wafanyabishara wa mifugo Nyaga wa Nyaga akitoa mapendekezo ya wafanyabiashara kupinga kuhamia katika soko hilo kutokana na kutokamikilia kwa miundombinu huku Dkt Mugarula na Dkt Qwali wakitupia kisogo kamera wakiwa wameweka mikono nyuma kuashiria kushindwa kwa hoja zao. Wafanya biashara hao wamesema kama Wizara ya Mifugo na Uvuvi haitarekebisha kasoro ambazo ziko katika soko la Nyamatala, hawako tayari kuhama katika soko la Igoma ambako wanafanyia biashara yao kwa sasa, na kama watalazimishwa kuhama watasitisha kutoa huduma ya kuuza na kuchinja mifugo ili kuipa serikali ujumbe kuhusu kutatua tatizo hilo.
Choo kinachotarajiwa kutumiwa na wafanyabiashara wa mifugo pamoja na wateja mbalimbali watakaofika katika soko la Kimataifa la mnada wa Nyamatala, Misungwi Mwanza.Choo hicho kina matundu manne mawili kwa ajili ya wanawake na mengine kwa matumizi ya wanaume.
Trekta na bolzer la maji likiwa limeegeshwa katika soko la Kimataifa Nyamatala, Misungwi bolzer hilo linauwezo wa kubeba maji lita 4000, maji ambayo yatatumika kwa ajili ya kunywesha mifugo pamoja na matumizi ya choo
Jengo la kujikinga na mvua ama jua liliojengwa katika soko la mnada wa Kimataifa wa Nyamatala ,Misungwi Mkoani Mwanza, ambalo linalalamikiwa na wafanyabiashara wa mifugo kuwa ni dogo na halikidhi mahitaji ya soko hilo kulingana na hadhi yake.
Sehemu ya kunyweshea mifugo maji katika soko la mnada wa Kimataifa, Nyamatala wilayani Misungwi kama linavyoonekana.
Dkt Mugarula wa kwanza kushoto akisikiliza maswali kutoka kwa Joseph Sikila, Makamu Mwenyekiti wa MWASIBA aliysimama kulia.
Dkt Mugarula akijitetea mbele ya umati wa wafanyabiashara wa mifuko kwenye mkutano uliofanyika katika eneo la soko la kimataifa Nyamatala Misungwi, kushoto kwake ni misimamizi wa minada kanda ya ziwa dkt. Bura Qwali.
Ikengele Simon akimbana kwa maswali Dkt Mugarula. (PICHA NA MASHAKA BARTAZAR -MWANZA)

No comments:

Post a Comment