TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 8, 2012

WANANCHI ARUSHA WALALAMIKA KUPORWA ARDHI

NA GLADNESS MUSHI - ARUSHA
WANANCHI wa kjiji cha Olkunjwado kilichopo kata ya Ngarenanyuki wilayani Arumeru wamemlalamikia mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Joseph Loibai kwa kosa la kuuza ardhi kinyume cha sheria sambamba na kutowasomea mapato na matumizi wananchi hao. Wakiongea na WAANDISHI WA HABARI baadhi ya wananchi ambao hawakupenda kutajwa majina yao walisema kuwa mwenyekiti huyo amakuwa na tabia ya kuuza maeneo ya watu wasiokuwa na uwezo kwa mzungu anaeishi katika kijiji hicho kwa manufaa yake binafsi Aidha walisema kuwa sheria ya ardhi inasema ardhi haiuzwi kiholela na hata kama basi itauzwa kuna asilimia ambayo itaenda serikalini lakini kwa mwenyekiti huyo ni tofauti na sheria hiyo. Mbali na hilo waliongeza kuwa kwa kipindi cha mwaka jana walimtaka mwenyekiti huyo kuwasomea wananchi hao mapato na matumizi kwa ajili ya michango mbali mbali wanaochanga kijijini hapo lakini hakufanya kama walivyokuwa wanataka wao. Waliongeza kuwa mapato hayo na matumizi waliyoomba kusomewa yanatokana na michango waliyochanga kwa ajili ya shule ya kutwa ya sekondari ya Momela na hadi sasa fedha hizo hazijulikani zilipo hali ambayo inawatia mashakani na mwenyekiti huyo ambapo hadi sasa wamekataa kuchanga michango mingine hadi wasomewe mapato hayo Hata hivyo walimtaka diwani wa kata hiyo kuitisha mkutano ili waweze kutoa kero zao kwa kuwa mwenyekiti huyo amekataa kusikiliza kero zao Aidha gazeti hili liliweza kuongea na mwenyekiti huyo kwa njia ya simu na kueleza kuwa hajauza ardhi kinyume cha sheria bali ni makubaliano yao wote waliopitisha kumpatia mzungu huyo eneo. Kwa upande wa kuwasomea mapato na matumizi alisema kuwa alishawaomea mapato na matumizi kwa kipindi cha nyuma ila mara ya mwisho koramu haikutimia hivyo kushindikana kusomewa kwa mapato hayo... .

No comments:

Post a Comment