TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, September 21, 2013

MBUNGE SAME KUNG'OLEWA NA CHADEMA

Same. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza operesheni maalumu ya kumng’oa ubunge, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi, Dk David Mathayo David katika Uchanguzi Mkuu wa 2015.
Operesheni hiyo iliyopewa jina la “Operesheni Mathayo Out” kwa kifupi OMO ilianza wiki iliyopita kwa kufanya mikutano ya hadhara jimboni humo na itaendelea tena wiki ijayo.
Mmoja wa makamanda wa operesheni hiyo, Gervas Mgonja alisema jimbo hilo limekuwa chini ya himaya ya CCM tangu Uhuru lakini wananchi wake wapo kama wamefunga ndoa na tatizo la maji.
Dk Mathayo ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi alipoulizwa kuhusu operesheni hiyo ya kumng’oa alisema, Chadema ni chama kidogo na hakimnyi usingizi kwa madai uwezo wa kampeni unaishia Himo.

No comments:

Post a Comment