TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, September 21, 2013

VITA NI VITA MULA: HUKO ENGLAND NI MPAMBANO KATI YA YAYA TOURE WA CITY NA MAROUANE WA UNITED

Viungo Yaya Toure wa City ataonyeshana ufundi na Marouane Fellaini wa United kesho kwenye uwanja wa Etihad.
Manchester, England. Mashabiki wa Manchester United wamefanikiwa kumpata Marouane Fellaini na kiungo huyo wa Ubelgiji ameonyesha kiwango cha juu kwa kutoa pasi nzuri na kunyang’anya mpira wakielekea katika mchezo wa kesho dhidi ya mahasimu wao City. Mabingwa wa msimu uliopita na washindi wa pili wanakutana kwenye Uwanja wa Etihad, wakiwa na rekodi ya ushindi waliopata katikati ya wiki katika Ligi ya Mabingwa.
Mshambuliaji wa Wayne Rooney amerudi kwenye kiwango chake na Jumanne alifunga mabao mawili wakishinda 4-2 dhidi ya Bayer Leverkusen, lakini uwepo wa Fellaini katika nafasi ya kiungo aliyeonyesha uwezo mzuri wa kumiliki mpira umeongeza ladha ya mchezo wa kesho. Wapinzani wao City baada ya kupoteza dira katika ligi katikati ya wiki walishinda 3-0 dhidi ya Viktoria Plzen katika Ligi ya Mabingwa, ushindi unaomfanya kocha Manuel Pellegrini kuamini kwamba umerudisha kujiamini kwa wachezaji wake.
“Tuna mechi ngumu Jumapili na ushindi wa ugenini katika Ligi ya Mabingwa tena wa mabao matatu, nafikiri umerudisha kujiamini kwa wachezaji.” Kiungo wa City,Yaya Toure, ambaye ni kama Fellaini ameonyesha kiwango cha juu, cha kutengeneza magoli na uwezo mkubwa wa kusoma mchezo, pia alifunga bao moja dhidi ya Plzen na kesho inategemewa itakuwa ni vita kubwa kati ya viungo hao wawili.
Hii ni mechi ya kwanza ya miamba ya Manchester kukutana wakati timu zote zikiwa na makocha wapya ambao wanajua kuwa City imekusanya pointi 10 kutoka kwa United katika michezo saba ya ligi waliokutana katika misimu mitatu iliyopita.
KUJIULIZA UPYA
Liverpool walioanza kwa kishindo msimu huu wakiongoza kwa pointi 10, leo watakuwa wenyeji wa Southampton, lakini watamkosa kiungo wao Philippe Coutinho aliyeumia bega na atakuwa nje ya uwanja hadi mwezi ujao. Tegemeo lao litabaki kwa Daniel Sturridge ambaye amefunga bao kila mechi aliyocheza msimu huu, kabla ya kurejea kwa mshambuliaji wa Uruguay, Luis Suarez anayemaliza kifungo chake cha mechi 10, baada ya mchezo wa leo.
Baadaye leo, Chelsea watawakaribisha Fulham huku wakiwa na kumbukumbu ya vipigo viwili mfululizo kutoka kwa Everton wiki iliyopita pia walichapwa nyumbani na Basel katika Ligi ya Mabingwa.

No comments:

Post a Comment