TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, September 17, 2013

PINDA KORTINI LEO

Posted: 16 Sep 2013 05:03 AM PDT
  •  ZAIDI YA MAWAKILI 20 KUWAKILISHA LHRC

Na Rachel Balama
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) dhidi ya Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda. 

Katika kesi hiyo, Jaji Kiongozi F a k h i J a n d u , a n a t a r a j iwa kuongoza jopo la Majaji wawili ambao watasikiliza kesi hiyo, Jaji Augustine Mwarija na Jaji Dkt. Fauz Twaib.LHRC na TLS walifungua kesi hiyo dhidi ya Bw. Pinda, wakidai alitoa kauli ya kuruhusu vyombo vya usalama kuwapiga watu wanaokataa kutii sheria zinazotolewa na mamlaka husika akiwa bungeni Mjini Dodoma.  

Mbali na Bw. Pinda, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ambapo upande wa LHRC unawakilishwa na mawakili zaidi ya 20.Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Bw. Pinda, anakabiliwa na tuhuma za kudaiwa kuvunja Katiba ya nchi kwa kuruhusu askari kuwapiga wananchi.

LHRC imepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli ya Bw. Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.Mkurugenzi wa LHRC, Dkt. Hellen KijoBisimba, alisema Bw. amekiuka kifungu cha Katiba ya nchi Ibara 13 (1).

Katika kesi hiyo, Jaji Kiongozi F a k h i J a n d u , a n a t a r a j iwa kuongoza jopo la Majaji wawili ambao watasikiliza kesi hiyo, Jaji Augustine Mwarija na Jaji Dkt. Fauz Twaib.LHRC na TLS walifungua kesi hiyo dhidi ya Bw. Pinda, wakidai alitoa kauli ya kuruhusu vyombo vya usalama kuwapiga watu wanaokataa kutii sheria zinazotolewa na mamlaka husika akiwa bungeni Mjini Dodoma.

Mbali na Bw. Pinda, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ambapo upande wa LHRC unawakilishwa na mawakili zaidi ya 20.Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Bw. Pinda, anakabiliwa na tuhuma za kudaiwa kuvunja Katiba ya nchi kwa kuruhusu askari kuwapiga wananchi.

LHRC imepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli ya Bw. Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.Mkurugenzi wa LHRC, Dkt. Hellen KijoBisimba, alisema Bw. amekiuka kifungu cha Katiba ya nchi Ibara 13 (1).

No comments:

Post a Comment