TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, September 19, 2013

SUMATRA YAPIGA ‘STOP’ MATUMIZI YA ECTN BANDARINI

Na Reuben Kagaruki


MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), i m e a m u r u kusimamishwa mara moja kwa mpango wa tozo ya ufuatiliaji mizigo bandarini kwa njia ya mtandao (Electonic Cargo Tracking Note-ECTN) uliopigiwa debe na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA). Hatua hiyo ya SUMATRA inatokana na malalamiko ya Chama Cha Mawakala wa Meli Tanzania (TASAA) kupinga mpango huo na kumwandikia Mkurugenzi Mkuu wa TPA kutaka mpango huo usitishwe.Mpango huo ulipangwa kuanza kutumika kwa mizigo yote inayoingia bandarini kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.

Pamoja na kulalamikia dosari  m balimbali zilizojitokeza kwenye mpango huo likiwemo suala la kutoshirikishwa wadau katika mjadala wa wazi kwa mujibu wa SUMATRA, TASAA iliukataa mpango huo kwa maelezo kwamba ni batili na haupaswi kutumika kwa kuwa uliwaweka kando wadau na unaongeza gharama zisizo za lazima.

Barua ya TASAA yenye kumb. HS /TASAA/TPA/ 130712 ya Julai 12, mwaka huu iliyotumwa kwa Mkurugenzi wa TPA, ilielezea wasiwasi wa wadau kuhusu matokeo ya kiuchumi yanayoweza kuikumba sekta hiyo na taifa kwa ujumla endapo mpango huo ungetekelezwa.Barua hiyo iliyosainiwa na Katibu wa TASAA, Peter Kirigini, iliwataka wateja wa chama hicho kote duniani kupuuza waraka huo wa TPA kutangaza matumizi ya ECTN, sambamba na kuitaka mamlaka husika SUMATRA kuingilia kati mara moja suala hilo ili kulipatia ufumbuzi.

Baada ya SUMATRA kupitia suala hilo, ilifikia mwafaka na kutoa maamuzi kusitisha mara moja mpango huo. Katika hukumu yake iliyosainiwa na Mkurugenzi wake, Kilima, SUMATRA imejiridhisha kwamba ni kweli TPA ilisaini makubaliano ya kuanzisha mpango huo na ulipangwa kuanza kutumika Septemba mosi 2013 kwa mizigo yote ya meli inayoingizwa nchini.
Katika uamuzi wake SUMATRA imeeleza kuwa tayari kuna mifumo (systems) inayotumika kufuatilia mizigo kuanzia inapopakiwa na pia kuna mifumo inayofanya kazi vizuri kupima thamani kwa CIF.Pia SUMATRA ilibaini kwamba TPA haikushirikisha wadau wakubwa wa bandari katika uanzishwaji wa mpango huo na kueleza kwamba matumizi ya ECTN yataongeza gharama kwa mawakala wa meli na mzigo huo utawaangukia wanaoingiza bidhaa moja kwa moja na hatimaye kuwagusa watumiaji wa mwisho.

SUMATRAimebainisha kwamba matumizi ya ECTN yataongeza mchakato na mlolongo wa nyaraka hivyo kusababisha gharama zingine kwa mawakala wa meli na kuweka wazi kwamba, mbaya zaidi bandari zingine shindani hazijaona umuhimu wa matumizi ya mpango huo, hivyo matumizi ya ECTN utasababisha mdororo kwa bandari zetu.

P i a  i m e s e m a k w a kutegemea huduma za kampuni ANTASER BVBA itasababisha shughuli za kuingiza mizigo kuwa za kificho jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi kwa kukosa usimamizi wa mizigo inayoingia.Kutokana na mazingira hayo, SUMATRA imeitaka TPA kuiagiza Antaser BVBA kuachana na mpango wake wa kuanzisha ECTN sambamba na kuondoa jedwali la gharama lililokwishawekwa kwenye mtandao wake.

SUMATRAimeitaka TPA kuiagiza Antaser BVBA kutumia mtandao wake kuwafahamisha mawakala wa meli kwamba utekelezaji wa matumizi ya ECTN umesitishwa na kwamba TPA ilipaswa kuwasiliana na mdhibiti kwa kufuata kanuni na taratibu zilizopo kabla ya kuanzisha huduma ya ECTN.TPA ambao waliingia mkataba na kampuni moja ya Ubelgiji, iitwayo ANTASER BVBA kwa lengo la kuanzisha tozo hiyo.

Tozo hiyo ya ECTN ilikuwa kwa ajili ya ufuatiliaji wa mzigo kutoka nchi inakotoka kwa njia ya mtandao, kazi ambayo wadau walisema hufanywa na kampuni za meli na zile za wakala wanaosafirisha mizigo hiyo na si dhamana ya TPA ambao jukumu lao ni kupokea mizigo kutoka kwenye meli cargo handling) na kuhifadhi kwa muda ikisubiri wateja kuichukua

No comments:

Post a Comment