TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, February 20, 2014

MSD YATOA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UTARATIBU WA MANUNUZI NDANI YA BOHARI YA DAWA

  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Cosmas Mwaifwani (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa Umma kuhusu utaratibu wa manunuzi ndani ya bohari ya dawa. Kulia ni Mkurugenzi wa Manunuzi wa MSD, Heri Mchunga na Mwanasheria, Domonica Meena.
………………………………………………………………………………..
 Idara ya Bohari ya Dawa (MSD) iliundwa kwa sheria ya Bunge Na. 13 ya mwaka 1993. Ni Idara inayojitegemea chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ilianzishwa ili kuunda, kudumisha na kusimamia mfumo ulio bora na wenye gharama nafuu wa ununuzi, uhifadhi na usambazaji dawa na vifaa-tiba, vitendanishi kwa ajili ya hospitali  navituo vya kutolea huduma ya afya nchini
Takwimu zilizopo kwa sasa  zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia  Themanini (80%) ya mahitaji yote ya Dawa,Vifaa tiba, Vitendanishi nchini vinatoka nje ya nchi hivyo taratibu za manunuzi hufuata taratibu na miongozo ya  ndani ya nchi na ya kimataifa.
Utaratibu wa uagizaji na uingizaji wa dawa ndani ya nchi huratibiwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), kuwa dawa yoyote kabla ya kuingizwa chini lazima iwe imesajiliwa na Mamlaka na  hukaguliwa pindi inapogombolewa ili kuhakikisha ubora wake. Sambamba na ukaguzi huo pia Bohari inavyo vitengo vya Ukaguzi wa Ndani (Internal Audit) na Uthibiti Ubora (Quality Assurance) ili kujihakikishia zaidi  kuwa taratibu za manunuzi zinazingatiwa pia dawa zinazonunuliwa  zinakidhi viwango vilivyokwishawekwa.
Aidha taribu za manunuzi  katika Bohari kama ilivyo taasisi nyingine yoyote ya Serikali husimamiwa  na kuongozwa na sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na
kanuni zake  za mwaka 2013. Taratibu za manunuzi huanza pale ambapo kuna  uhitaji wa dawa fulani kutoka katika vituo vya kutolea  huduma ya afya nchini. Mahitaji ya dawa kutoka katika vituo vya kutolea huduma ya afya huenda sambamba na mgawo wa  fedha kwa kila kituo husika. Bohari inayo Bodi 
ya Zabuni (MSD Tender Board)  kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma yenye wajumbe ambao ni wafanyakazi katika Bohari wa ngazi za juu na wenye utaalamu tofauti. Bodi  ya Manunuzi 
ndiyo chombo cha juu chenye maamuzi ya manunuzi ndani ya Bohari hivyo manunuzi yote ndani ya Bohari husimamiwa na Bodi hii.
Njia  inayotumika katika manunuzi ya bidhaa ndani ya Bohari ni kwa kupitia zabuni za kimataifa na hii ni kutokana na ukweli kwamba zaidi ya asilimia 80 ya bidhaa hutoka nje ya nchi. Zabuni ya kimataifa iko wazi kwa kila mshitiri ndani na nje ya nchi bila kubagua nchi anayotoka. Kigezo cha  kwanza  kwa mshitiri  kushiriki katika zabuni ni kuwa na bidhaa yake imesajiliwa nchini na mamlaka zinazohusika na kigezo hiki cha kusajili hakina kinga  kwa mshitiri yoyote yule.
Utangazaji wa zabuni  hufuata  na kutumia  njia na machapisho ya kitaifa na Kimataifa kupitia tovuti (webistes) za Bohari (www.msd.or.tz) na ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (www.ppra.go.tz). Aidha tunatumia Magazeti ya kimataifa, na ya kitaifa katika lugha za Kiingereza na Kiswahili ili kuwafikia watu wote. Zabuni hufunguliwa hadharani kwenye siku ambayo ilitamkwa kwenye gazeti na washitiri au wawakilishi wao hualikwa kwenye zoezi hilo ili kujiridhisha kuwa vigezo mbalimbali ikiwapo bei iliyotamkwa na uwepo wa nyaraka muhimu vimefuatwa
Baada ya ufunguzi hufuata mchakato  wa tathmini (evaluations) kwa kutumia wataalamu huru  kulingana na zabuni husika, wakati mwingine wataalam hao hutoka nje ya Bohari kulingana na  utaalam wao katika zabuni husika.
Baada ya mchakato wa tathmni hufuata zoezi la kuwapata washindi , zoezi ambalo hufanywa na Bodi ya zabuni. Washindi hupatikana kutokana na vigezo vilivyoweka na hupaswa kutimizwa. Washitiri wote hupewa mrejesho juu ya mchakato mzima jinsi ya zabuni ilivyokwenda na matokeo yake. Bohari hutumia mfumo  uliowazi, haki na usawa katika manunuzi ili kuhakikisha kunakuwa na ushindani na thamani fedha kwenye mali ya umma.
Sheria ya Manunuzi ya Umma inalinda haki za mshindani yeyote yule ambaye baada ya kwisha mchakato anaweza kuwa na hisia kuwa Bohari ya Dawa haikumtendea haki kwani inamruhusu kukata rufaa kwenye Mamlaka ya ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ambao huitisha nyaraka zote toka Bohari na kuzipitia na kisha huzitolea maamuzi.
Ili kuhakikisha uwazi na haki, Sheria ya manunuzi inatutaka tuchapishe katika vyombo vya habari matokeo ya washindi wa zabuni wote kila mwisho  wa mwaka.  Taarifa ya zabuni yamwaka wa fedha wa 2012/ 13 iliiyotolewa kwenye Mwananchi la tarehe 27/ 12/ 13 na la The Guardian la  tarehe 31/ 12/ 13 nairudia hapa ili kuonyesha washindi wa zabuni hizo, thamani na nchi ambazo makampuni hayo yanatoka.
Namba ya Zabuni    Aina ya Bidhaa    Kampuni iliyoshinda    Thamani    Tarehe ya kutoa mkataba    Nchi 
PHARMACEUTICALS
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/04    Supply of Pharmaceuticals    Samiro Pharmacy    $ 3,379,327    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/05    Supply of Pharmaceuticals    Tata Africa Holdings Ltd    $ 177,668    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/13    Supply of Pharmaceuticals    Nirma Limited    $ 1,214,951    12/7/2013    India
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/07    Supply of Pharmaceuticals    Novo Nordisk A/S    $ 1,516,643    12/7/2013    Denmark
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/14    Supply of Pharmaceuticals    Abacus Paraental Drugs Ltd    $ 2,914,336    12/7/2013    Uganda
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/03    Supply of Pharmaceuticals    SG Star Pharmaceutical Limited Total    $ 470,150    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/16    Supply of Pharmaceuticals    Bahari Pharmacy Ltd Total    $ 1,820,539    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/06    Supply of Pharmaceuticals    Planet Pharmaceutical Ltd Total    $ 846,730    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/08    Supply of Pharmaceuticals    Serum Institute of India Total    $ 953,577    12/7/2013    India
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/10    Supply of Pharmaceuticals    Medopharm PVT Ltd Total    $ 386,009    12/7/2013    India
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/09    Supply of Pharmaceuticals    Pyramid Pharma Total    $ 1,422,933    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/18    Supply of Pharmaceuticals    Fresenius Kabi Total    $ 1,294,587    12/7/2013    India
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/01    Supply of Pharmaceuticals    Jilichem (T) Ltd Total    $ 6,473,661    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/04    Supply of Pharmaceuticals    IDA Foundation Total    $ 797,802    12/7/2013    Netherlands
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/15    Supply of Pharmaceuticals    Claris life  sciences Limited Total    $ 970,819    12/7/2013    India
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/17    Supply of Pharmaceuticals    Keko Pharmaceticals Industries (1997) Ltd Total    $ 19,485,669    12/7/2013    Tanzania
IE-009/2012/2013/HQ/G/30/12    Supply of Pharmaceuticals    Galentic Pharma (India) PVT Ltd Total    $ 819,836    12/7/2013    India

No comments:

Post a Comment