TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, February 20, 2014

VIONGOZI WA VILABU VYA MICHEZO YA SHIMIWI KUNOLEWA FEBRUARI 24

Na Happiness Shayo
Shirikisho la Michezo Wizarani (SHIMIWI) limeandaa mafunzo ya uongozi,ualimu wa michezo na huduma ya kwanza viwanjani   kwa viongozi wa vilabu vya michezo ya SHIMIWI,yatakayofanyika mjini Morogoro  Februari 24-28 mwaka huu.
Hayo yalisemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa SHIMIWI Bw.Moshi Makuka mapema leo ofisini kwake alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa mikakati ya shirikisho hilo kwa mwaka wa fedha 2013/2014.
Bw.Makuka alifafanua kuwa lengo la mafunzo hayo kwa viongozi wa vilabu ni kuwajengea uwezo wa kuongoza shughuli za michezo,kuwapa ufahamu zaidi juu ya  katiba,sheria na kanuni za michezo ya SHIMIWI na kuwapa uelewa wa namna ya kutoa huduma ya kwanza katika viwanja vya michezo.
Akielezea sababu za Shirikisho hilo kuandaa mafunzo hayo Bw.Makuka alisema kuwa mafunzo hayo yanafanyika kutokana na na changamoto zilizojitokeza katika mashindano ya SHIMIWI ya miaka iliyopita  ambapo baadhi ya viongozi huvunja sheria na kanuni za michezo.
“Baadhi ya viongozi wa SHIMIWI katika Wizara ,Idara Zinazojitegemea,wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa (SHIMIWI) wamekuwa wakilalamikiwa kutumia wachezaji ambao sio watumishi wa umma .”alisema Bw.Makuka.
Pia,aliongeza kuwa mafunzo hayo yatawahamasisha viongozi wa ofisi za Serikali zilizoshindwa kushiriki katika michezo ya mwaka jana ili iweze kushiriki mwaka huu kwa kuwa michezo kwa watumishi wa umma hujenga afya,mshikamano na pia huongeza ufanisi mahala pa kazi.
Michezo ya SHIMIWI ilianzishwa kwa madhumuni ya kuwakutanisha watumishi wa Serikali kwa lengo la kujenga nakuendeleza tabia ya ushirikiano,upendo na undugu hivyo hufanyika kila mwaka.Mafunzo haya hufanyika kila mwaka kwa mujibu wa kalenda ya SHIMIWI.

No comments:

Post a Comment