TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, February 21, 2014

MWIGULU NCHEMBA AZUNGUMZA NA WANANCHI WA JIMBO LAKE.

Hii leo nimefanya Mkutano wa Hadhara Viwanja Vya Kiomboi -Stendi Wilayani kwangu Iramba.Kubwa nimezungumza na Wananchi Kazi za Maendeleo na Kupokea Kero mbalimbali Wanazokutana nazo kwenye Maeneo Wanayoishi.Msisitizo Wangu nimeagiza Serikali kupitia kwa Mkuu Wa Wilaya Kuwachukulia hatua Kali Viongozi wote Wanaokwepa Kusoma Mapato na Matumizi ya Fedha za Umma.Wananchi Wanahitaji Uwazi wa Michango yao namna ilivyotumika,Kodi zao zilivyotumika.
Pia nimeendelea kusisitiza kuwa nimeamua kupigania Sera/Sheria ya Manunuzi Serikalini inatakiwa kurekebishwa na hili nitalifanyia Kazi.
Serikali inabeba Mzigo Mkubwa sana kwenye Manunuzi.Mf.Kiatu kinauzwa Tsh.10,000/=,Mwananchi wa Kawaida anaweza kununua kiatu hicho kwa Tsh. 10,000/=.Lakini kupitia Mzabuni Serikalini kiatu hicho hicho kitanunuliwa Tsh.50,000/=.Kwa maana hiyo kunafedha nyingi sana inapotea ya Serikali kupitia Mfumo huu tulio nao sasa wa Manunuzi.
Tuungane,Tulijenge Taifa letu.
Like · · · 9 hours ago ·

  • Peter J'quix and 35 others like this.
  • Nyakia Ally Hongera kaka! Hiyo ndiyo kazi ya siasa na uongozi sharti uwe karibu na watu wako na kusikiliza na kupokea kero zao, ili zitafutiwe ufumbuzi wa kuzitatu.
  • Stahimili Wanyaka kwa kuwa wewe ni naibu waziri-ww sasa uko kiserikali zaidi kuliko ki-chama. wewe kwa sasa ni waTZ wote na si Iramba tu, nikuombe mate wangu ufike maeneo mengine ya nje ya Iramba ikiwezekana na sehemu zilizosahauliwa pia. Tatizo langu ni hayo manunuzi k...See More
  • Juma Abdallah Sadick Hongera mh.hiyo ndiyo mikakati hai na endelevu itakayoinua na kuboresha maisha ya wana iramba na watanzania kwa ujumla.juhudi zaidi zielekeze kwenye kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili wapiga kura wako.mfano wako ni wa kuigwa na naomba waheshimiwa wengine waige mfano wako ili waipe heshima zaidi CCM na serikali yake.Viva CCM,viva Jk,viva mwigulu aluta continua....
  • Mathew Mndeme Kwenye hili ulikua na support yangu hata kabla hujawa waziri. Kwa wanaojua kinachoendelea kwenye mfumo wa manunuzi, ni jambo la kusikitisha, kuumiza na kutoa machozi kwa jinsi tunavyopoteza fedha nyingi bila tija
  • Mpalule Shaban

No comments:

Post a Comment