TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 19, 2014

REDIO ZA JAMII NCHINI ZIMETAKIWA KUWA MAKINI NA UANDAAJI WA VIPINDI PAMOJA NA HABARI, KATIKA KUEPUSHA UIBUAJI WA MIGOGORO KATIKA JAMII ZINAZOWAZUNGUKA

Mwezeshaji wa warsha hiyo ambaye pia ni Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco, Mama Rose Haji Mwalimu, akitoa utambulisho kwa waendesha warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kutoka Shirika la Search for Common Grounds (SFCG), yanayoendelea mjini Dodoma.
DSC_0006
Meneja Mradi wa SFCG wilaya ya Tarime, Bwana Jacob Mulikuza, akielezea maudhui ya warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kwa washiriki ambao ni waandishi wa redio za jamii kutoka Tanzania, warsha hiyo inafanyika mjini Dodoma.
DSC_0016
Washiriki wa warsha wakimsikiliza Bw. Jacob Mulikuza kutoka Shirika la Search for Common Grounds – SFCG (hayupo pichani) akielezea jambo wakati wa warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro inayoendelea mjini Dodoma kwa waandishi na watangazaji wa Redio za Jamii nchini iliyofadhiliwa na UNESCO kupitia mradi wa DEP.
DSC_0018
DSC_0023
Mmoja wa washiriki akifafanua jambo katika warsha hiyo iliyojadili namna ya kuandika habari za migogoro kutoka Shirika la Search for Common Grounds (SFCG) yanayoendelea mjini Dodoma.
DSC_0082
Meneja mradi wa SFCG wilaya ya Tarime, Bwana Jacob Mulikuza, akiwapatia maelekezo washiriki wa warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kuhusu namna ya uwajibikaji katika kutatua migogoro ndani ya Jamii.
DSC_0076
Mmoja wa washiriki Bwana Baraka kutoka ORS Fm Radio, akiwaelezea washiriki wenzaka namna Ya kutatua fumbo lililokuwa sehemu ya kazi za Vikundi, katika warsha ya Uandishi wa habari za Migogoro kuhusu namna ya uwajibikaji katika kutatua migogoro ndani ya Jamii.
DSC_0105
Mratibu wa vyombo vya habari wa SFCG Zanzibar, Bwana Ali sultan, akielezea kuhusu ushiriki wa SFCG huko Zanzibar katika warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kwa washiriki ambao ni waandishi wa Redio za Jamii kutoka Tanzania, warsha hiyo inayofanyika mjini Dodoma imefadhiliwa na Shirika la UNESCO kupitia mradi wa Demokrasia na Amani (DEP) kuelekea Uchaguzi 2015.
DSC_0115
Meneja Mawasiliano wa SFCG kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bwana Dupont Ntererwa, akielezea kuhusu ushiriki wa SFCG huko DRC katika warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kwa washiriki ambao ni Waandishi wa Redio za Jamii kutoka Tanzania, warsha hiyo inayofanyika mjini Dodoma.
DSC_0156
Washiriki wakifanya kazi za vikundi.

No comments:

Post a Comment