TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, June 5, 2016

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KIONGOZI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA CHINA LUO ZHIJUN IKULU JIJINI DAR

WAZIRI MAKAMBA ASHIRIKI KUPANDA MITI YA MIKOKO NA WAKAZI WA KATA YA MBWENI JIJINI DAR LEO




NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI DK. JULIANA PALLANGYO AFANYA ZIARA KATIKA KAMPUNI YA PUMA ENERGY

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAENDESHA DROO YA PILI YA MILLIONI 100 NA TUSKER FANYA KWELI NA UWINI

Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombela (kulia) akimkabidhi vocha ya mshindi afisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya kubahatisha nchini Humud Semvua ili kuhakiki taarifa za mshindi wakati wa droo ya pili ya promosheni ya Millioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombela (kulia) akiongea kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa droo ya pili ya promosheni ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini wakati wa droo hiyo, pembeni yake ni afisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya kubahatisha nchini Humud Semvua akifurahia jambo alilosikia kutoka kwa mmoja ya washindi kupitia njia ya simu.
Kundi la pili la washindi wa mamilioni ya Tusker watangazwa.
Wiki iliyopita ilishuhudiwa washindi kumi kutoka mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na Kilimanjaro wakiondoka na Million moja kila mmoja kupitia promosheni inayoendelea ya Millioni 100 na Tusker Fanya Kweli na Uwiniinayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti. 
Katika droo ya pili iliyochezeshwa leo, washindi wengine kumi walitangazwa. Katika droo hiyo iliyofanyika ITV na kushuhudiwa na maofisa kutoka Bodi ya kusimamia Michezo ya Kubahatisha walitangazwa washindi kumi ambao ni Rose Mkwizu, Sijali Ally, Anna Lazaro kutoka Dar es Salaam, Elizabert Wiliam kutoka Mlandizi –Pwani, Josephat Lukindo,George Mlay kutoka Kilimanjaro,Geofrey Manangwa kutoka Tanga, Wanzagi na Lucas Fransis kutoka Mwanza na Umoja Nyakwa kutoka Morogoro. 
Mbali na washindi hao ambao walijipatia zawadi ya pesa taslim, pia kuna washindi kibao waliojishindia bia za bure tangu promosheni ilipoanza. Bado kuna wiki nane ambapo zimebaki Millioni 80 kushindaniwa kwa kipindi hicho kilichobaki cha promosheni hiyo.
Naye mmoja wa washindi Elizabert Wiliam alisema kuwa Shoo ya kwanza iliyorushwa kupitia runinga ya ITV ndiyo iliyomsukuma kushiriki promosheni hiyo. “Nilitazama droo ya kwanza wiki iliyopita na siku zote mimi ni mtumiaji mzuri wa bia ya Tusker, baada ya muda punde tu nilienda kunywa huku nikiwa na shauku ya kushinda tu na kuingia kwenye droo” alisema bi Elizabeth. Aliendelea kwa kuipongeza Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kuendesha promosheni kama hiyo inayogusa maisha ya wateja wao kwa kubadili sehemu au maisha yote kwa ujumla. Aliongeza kuwa pesa aliyoipata ataitumia katika kukuza biashara zake.
Naye Meneja Masoko wa Bia ya Tusker Nandi Mwiyombela alieleza kuwa, promosheni ya ‘Tusker Fanya Kweli Uwini’ inaendelea vyema kabisa na washindi wanaendelea kushinda kutoka kila pande za Tannzania ambako sasa mikoa ya kanda ya ziwa imeungana nasi katika promosheni hii wiki iliyopita. Tuna washindi kutoka nchi nzima, Mwanza, Morogoro, Arusha, Moshi na Dar es Salaam. 
Tunapenda kuwathibitishia wateja wetu kuwa promosheni hii si ya watumiaji wa bia ya Tusker waliopo Dar es Salaam tu bali kwa ushahidi huu wa washindi kutoka mikoa mingine unatosha kuthibitisha kuwa ni ya nchi nzima.
Washindi wetu wa wiki iliyopita watapokea zawadi zao za fedha taslim Million 1 katika hafla fupi ya makabidhiano itakayofanyika leo jijini Dar es Salaam na Moshi.
========================================

MAMA JANETH MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUWAJALI WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye Ulemavu wa Ngozi Mkoa wa Lindi Bw. Hemed Said mafuta ya kuzuia mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi leo Ikulu ndogo ya Mkoa wa Lindi.Katikati ni Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akikabidhi zawadi ya mbuzi na kuku kwa Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye Ulemavu wa Ngozi Mkoa wa Lindi Bw. Hemed Said walipomtembelea leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya ngozi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akikabidhi zawadi ya kuku kwa Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye Ulemavu wa Ngozi Mkoa wa Lindi Bw. Hemed Said walipomtembelea leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya ngozi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli, Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh. Godfrey Zambi wakiwa katika picha ya Pamoja na jamii ya watu wenye ulemavu leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Chama cha watu wenye Ulemavu wa Ngozi Mkoa wa Lindi walipomtembelea leo asubuhi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya kujikinga na mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa wakifurahia jambo na mtoto mwenye ulemavu wa ngozi walipomtembelea leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya kujikinga na mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi..
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiongea na jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi walipomtembelea leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya kuzia mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi ambapo aliiasa jamii kujali kundi hili na kuacha imani potofu dhidi yao. Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh. Godfrey Zambi
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiongea na jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi walipomtembelea leo asubuhi Ikulu ndogo Mkoani Lindi kwa ajili ya kupokea msaada wa mafuta ya kuzia mionzi ya jua kwa watu wenye ulemavu wa ngozi ambapo aliiasa jamii kujali kundi hili na kuacha imani potofu dhidi yao. Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Mary Majaliwa na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh. Godfrey Zambi

KILELE CHA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA BENKI KUU YA TANZANIA (1966 – 2016) KUFANYIKA JUNI 22, 2016















================================================

PROF.MBARAWA:BARABARA YA IRINGA- DODOMA KILOMITA 260 KUFUFUA UCHUMI WA MIKOA HIYO








TANZANIA YATEULIWA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA 37 WA SHIRIKA LA MAKAZI AFRIKA


Katika Mkutano Mkuu wa Abuja changamoto iliyojitokeza ni uwezo wa nchi za kiafrika wa kuwapatia wananchi wake nyumba za gharama nafuu, huku wajumbe wakitoa rai kwa serikali zao kuainisha vigezo vya kutambua nyumba ya gharama nafuu. Aidha, wajumbe wa Mkutano huo wanaona changamoto kubwa ya wananchi wengi wa Afrika kuweza kumiliki nyumba ya gharama nafuu ni uwezo mdogo unaotokana na vipato vidogo, kutokuwepo sera ya kuwezesha raia kumiliki nyumba za gharama nafuu, kukosekana kwa miundombinu katika makazi ya gharama nafuu, riba kubwa za mikopo ya ujenzi wa nyumba nafuu na ukosefu wa ardhi ya kujenga nyumba hizo.

Kwa ujumla changamoto za nchi za kiafrika katika kuwapatia wananchi wa kawaida makazi nafuu zinafanana na kilio kikubwa katika nchi hizo ni kuwepo makazi holela hata baada ya nchi hizo kujikomboa kutoka ukoloni mkongwe. Hivyo, Mkutano Mkuu huu umeazimia nchi wanachama kuweka juhudi katika kuipa kipaumbele sekta ya nyumba kwa kuwa ni sekta mtambuka katika kuharakisha ukuaji wa uchumi na maisha bora ya watu.(Habari za mkutano huo katika picha na Muungano Saguya, Abuja, Nigeria).

TAGLA NA TBA WAKAMILISHA MAFUNZO YA SIKU TANO KWA NJIA YA MTANDAO (VIDEO CONFERENCING).

MUHAMMAD ALI AFARIKI DUNIA




Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amina

**********  *********
HISTORIA FUPI YA MUHAMMAD ALI.

Muhammad Ali alikuwa bondia kwa sababu kuna mtu aliyemuibia baskeli yake. Alikuwa na umri wa miaka 12 wakati ule na alikuwa akiishi Louisville katika jimbo la Kentucky akijuilikana kwa jina la Cassius Mercellus Clay Jr.

Joe Martin, aliyekuja kuwa kocha wake baadaye, anaelezea jinsi kijana huyo alivyokuwa akilia huku akiahidi kumtandika magumi aliyemuibia baskeli yake pindi akimpata. Kocha huyo wa ubondia alimchukua Clay, kijana mweusi anayetokea katika familia ya watu maskini, na kumjumuisha na watoto wengine aliokuwa akiwafundisha.

“Alikuwa na bidii zaidi kuliko waatoto wote wengine niliokuwa nikiwasimamia,” anasema Joe Martin.
Ingawa Clay wakati ule hakuwa na nguvu ya kuvurumisha masumbwi, alikuwa mwepesi wa kuranda randa kupita kiasi. Mnamo mwaka 1960, akiwa na umri wa miaka 18, alishinda katika pambano la ndondi la michezo ya Olympiki mjini Rome, Italia. Medali yake ya dhahabu inasemekana aliitupa ndani ya Mto Ohio kwa sababu alikasirishwa na jinsi watu weusi wanavyobaguliwa nchini mwake.

Cassius Clay alikamilisha michuano ya wasiolipwa baada ya kuibuka na ushindi mara 100 katika jumla ya mapambano 108 aliyopigana. Wafanyabiashara 11 wa Kizungu kutoka Louisville walishirikiana ili kumfungulia njia Cassius Clay ya kuingia katika ulingo ya mabondia wa kulipwa.

Bondia huyo mwenye kipaji alikuwa akitajikana pia kuwa ni mtu aliyekuwa na majivuno na mdomo mpana. Kabla ya mapambano yake, Cassius Clay daima alikuwa akijinata kuwa yeye “ndie mbabe wa wababe na mzuri kuliko mabondia wote na kuwakejeli wapinzani wake.

Katika pambano lake la kwanza la kuwania ubingwa wa dunia Februari 1964 dhidi ya mtetezi wa taji hilo, Sonny Liston, Clay hakuwa akijulikana ni nani na watu waliamini angeshindwa tu. Lakini baada ya raundi ya sita, Liston aliungama. “Mie ndie mbabe,” alinguruma Cassius Clay kupitia kikuza sauti.

*Mwaka huo huo, alisilimu na kujiunga na kundi la Nation of Islam lililokuwa likiongozwa wakati huo mwanaharakati wa haki wa Wamarekani Weusi, Malcolm X. Akabadilisha jina la Cassius Clay na kujiita wakati huo huo Muhammad Ali*

Muhammad Ali hakuwa bondia tu, alikuwa mwanaharakati pia. Alipinga vita vya Marekani nchini Vietnam na alikataa kutekeleza sheria ya kutumikia jeshi. Mnamo mwaka 1967, akapokonywa sio tu leseni yake ya ubondia, bali pia alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela, ingawa baadaye bondia huyo wa aina pekee aliachiwa kwa dhamana.

Wasanii na wasomi mfano wa Richard Burton na Henry Fonda au mwandishi vitabu Truman Capote wakampigania mpaka Muhammad Ali akaruhusiwa tena kurejea ulingoni baada ya kulazimika kukaa nje kwa miaka mitatu.

Machi 8, 1971 Muhammad Ali aliteremka ulingoni Madison Square Garden mjini New York kwa kile kilichotaajwa “kuwa pambano la ndondi la karne” dhidi ya bingwa wa wakati ule, Joe Frazier. Lilikuwa pambano kati ya mafahali wawili, kati ya mpinzani na yule aliyekuwa akiangaliwa kama mwakilishi wa mtindo wa maisha wa Kimarekani. Katika pambano hilo la kusisimua la zaidi ya raundi 15, Frazier akashinda kwa pointi. Ali akalazimika kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya ubondia kunusa jamvi.

Yakafuata mapambano mengine ya kusisimua mfano wa lile la mjini Kinshasa dhidi ya George Foreman mnamo mwaka 1974, ambapo Muhammad Ali anasema “aliranda mfano wa kipepeo na kuuma kama nyuki”

Muhammad Ali alilipiza kisasi dhidi ya Joe Frazier mwaka 1975 na kumlazimisha kusalimu amri mnamo rauni ya 14. Mohammed Ali alistaafu mwishoni mwa mwaka 1981 baada ya kuranda kwa karibu miaka 40.

Wakati huo tayari alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya Parkinson. Licha ya maradhi hayo, Muhammad Ali ndiye aliyewasha mwenge wa Olimpiki huko Atlanta mnamo mwaka 1996 na kuusisimua ulimwengu mzima. Mwaka 1999 aliteuliwa na kamati kuu ya michezo ya Olimpiki kuwa “mwanaspoti bora wa karne.”

Mpinzani wake wa zamani George Foreman amegeuka hivi sasa kuwa rafiki yake mkubwa na kuungama “Muhammad Ali ndie bingwa wa mabingwa.”


Mpaka leo june 4 2016. Muhhamad Ali anapoteza maisha ndie mwanamasumbwi mstaafu kutoka nchini Marekani. aliepata kuwa bingwa wa uzito wa juu mara tatu

No comments:

Post a Comment