TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, June 4, 2016

TAMKO LA MTANDAO WANAFUNZI TANZANIA (TSNP) DHIDI YA UKIUKWAJI WA HAKI ZA WANAFUNZI WA STASHAHADA YA UALIMU SAYANSI, HISABATI NA TEKNOLOJIA (SPECCIAL DIPLOMA) KATIKA CHUO KIKUU DODOMA.


Baadhi ya Majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), katika Mwonekano huo
 
Hawa ni wanafunzi Miongoni mwao wapo walioweza kuathirika na timua hiyo leo wamelazimika kukutana na vyombo vya habari katia kujadili suala hilo ambalo mpaka sasa hakuna mwenye tamko la mwisho zaidi ya mheshimiwa Rais wa jamhuri waTanzania. na hii ndiyo barua ambayo leo imewasilishwa kwa baadhi ya Wandishi wa habari ikielezea jinsi Tanzania inavyotaka kukiuka Misingi ya haki za Binadam na haki ya Utawala Boba.
(Picha kwa Hissan ya Miss Demokrasia Tanzania   
=========================================
Press Release 

Ndugu Waandishi wa habari, 

Awali yayote tunapenda kupongeza jitihada kadha wa kadha ambazo zimekuwa zikifanywa na serikali kupitia Wizara ya Elimu kuhakikisha inaboresha mfumo wa Elimu nchini.
Pamoja na ukweli kwamba, kumekuwa na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia wizara ya Elimu haswa katika awamu hii ya Uongozi wa Mh. Raisi, John Pombe Makufuli. Mtandao wa Wanafunzi Tanzania unasikitishwa na kulaani baadhi ya maamuzi yaliyokwishafanyika na kukiuka utu, haki za Wanafunzi na vile vile taratibu, kanuni na sheria za nchi hii.

Kuhusu Sakata la Kufukuzwa Wanafunzi UDOM

Mumesikia hoja za viongozi mbalimbali juu ya sakata la Wanafunzi Waliosimamishwa UDOM, mmesikia hotuba ya Mh. Joyce Ndelichako, Waziri mwenye dhamana katika wizara ya Elimu, lakini vile vile mmesikia hotuba ya Mh. Raisi, John Pombe Makufuli aliyoitoa akiwa chuo kikuu cha taifa (UDSM)  tar. 02.06.2016

Tangu tar. 28 mei 2016, mara baada ya agizo la Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi (MoEST) la kuwarejesha nyumbani Wanafunzi takribani 7802 Mtandao huu umekua ukifanya tafiti za kina kupitia idara yake (Reseach& Training Department) na kupata taarifa za pande zote mbili kutoka vyanzo mbalimbali vya taarifa “Wahanga(Wanafunzi waliofukuzwa) na Watawala(Wizara ya Elimu) ”. Tumejiridhisha kwamba kitendo kilichofanywa dhidi ya Wanafunzi wa UDOM ni ukiukwaji mkubwa wa haki za Wanafunzi ambacho kilikuwa kwanza cha kimabavu na hakikuzingatia kabisa utu wa Wanafunzi husika. Taarifa zilizotufikia ni kwamba Wanafunzi walifukuzwa kama Wakimbizi ndani ya nchi yao, Polisi walizagaa kila kona na bunduki zao kama wanafukuza majambazi, hofu ilitanda na wanafunzi wengine kuogopa kurudi chuoni kwa hali ilivyokuwa. Mtandao huu unasikitishwa kwa matumizi makubwa ya vyombo vya dola lakini vile vile madhara yaliyowakumba Wanafunzi husika wakati wa zoezi la kuwaondoa chuoni.
Chimbuko la Mgogoro:

Ikumbukwe, wakati wa uongozi wa Mh. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu kama vile Mamlaka ya Elimu (TEA), Tume ya vyuo vikuu (TCU), Mamlaka ya vyuo vya Ufundi (NACTE) na wadau mbali mbali a Elimu, waliadhimia na kuzindua program maalumu ya kusomesha waalimu wa masomo ya Sayansi katika shule za sekondari nchini ili kutatua changamoto za uhaba wa waalimu wa masomo ya sayansi. Lakini ili kupata waalimu wenye sifa Serikali ikaweka sifa za Udahili kwamba itakuwa kwa wahitimu wa kidato cha nne tu waliopata daraja la 1,2 na 3 pia wawe na ufaulu wa alama A” au B” kutoka masomo ya sayansi. Na serikali ikawashawishi kwa ahadi ya kuwapa mkopo kwa 100%.

Tumeshangazwa kwamba, Sababu za kusimamishwa masomo wanafunzi hawa zimeendelea kubadilika badilika, sababu ya kwanza kabisa, ambayo ilisemwa na Prof. Joyce Ndelichako Bungeni ni Mgomo wa Wahadhiri uliotokana na kukosa posho za kuwafundisha Wanafunzi husika, Sababu ya pili ni wanafunzi kukosa sifa.

Mtandao huu umejiuliza, Kama suala kuu ni vigezo kwanini serikali isingeweka utaratibu maalumu wa kuwaondoa wanafunzi wasio na sifa na kuwawajibisha wale waliowadahili kinyume na standard zilizowekwa na serikali? 

1.      Tunapenda Kutumia fursA hii kukanusha taarifa zote za  uongo zilizotolewa na watawala/Viongozi dhidi ya wanafunzi husika. Na kumekuwa na utamaduni wa  Watawala kutumia Vyombo vya habari(Media coverage)  kama silaha ya kupotosha taarifa kwa umma (Taarifa hii itasomwa na muwakilishi wa wahanga wa Wanafunzi (UDOM)
Ombi letu.

1.      Tunaiomba serikali kupitia wizara yake ya Elimu ifanye hima kuwarudisha Wanafunzi husika ili kutoendelea kupoteza rasilimali muda wa wanafunzi husika
2.      Kama hotuba ya Mh. Raisi hapo juzi katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, akikiri kwamba kunawanafunzi wasio na vigezo walidahiliwa. Mtandao huu unaomba waliohusika kuwadahili wawajibishwe haraka iwezeanavyo lakini vile vile wanafunzi wafidiwe Rasilimali fedha na muda waliopoteza kwa wakati wote waliokuwa chuoni.

Hatma ya Wanafunzi (UDOM)
Kama itatokea, kunamwanafunzi au kundi Fulani la Wanafunzi, halitopewa haki zake, Mtandao huu utashirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu zikiwemo azaki zinazojihusisha na masuala ya utetezi kisheria kutafuta haki za Wanafunzi husika mahakamani

  Chanzo cha Migogoro katika Sekta ya Elimu Nchini.
v Kutokuwa na Muafaka wa Kitaifa katika Mfumo wa Elimu.
Mtandao huu unaamini kwamba haya yote ni madhara ya kutokuwa na muafaka wa kitaifa/Msimamo wa itaifa katia Sekta ya Elimu nchini. Kwa mda mrefu, mfumo wetu wa Elimu, Sekta ya Elimu nchini imekuwa inaendeshwa na kiwango cha utashi wa Waziri wa Elimu aliyepo madarakani na sio kuongozwa na dira/Muafaka/Msimamo wa kitaifa katika sekta ya Elimu

Tumeshuhudia, Mawaziri wa Elimu tofauti tofauti, katika awamu tofauti tofauti za uongozi tangu uhuru wa nchi hii (Mh.Jumanne Maghembe, Mh, Joseph Mongai, Mh. Shukuru Kawambwa na sasa Mh. Joyce Ndalichako), wakifanya maamuzi kutokana na kiwango cha utashi wao na mapenzi yao. Hii ni hatari katika taifa letu na imesababishwa na ukweli kwamba taifa limekosa dira/Muafaka wa kitaifa katika sekta ya Elimu nchini.
Hitimisho.

Mtandao wa Wanafunzi Tanzania unaamini kwamba kilichotokea Chuo Kikuu cha DODOMA kitakuwa msingi wa Serikali kupitia Wizara ya Elimu kuanza harakati rasmi za kimapinduzi za kuunganisha wadau wote wa Elimu nchini ili kuwa na mjadala mpana wa kitaifa wa namna ya kufikia Muafaka wa kitaifa katika sekta ya Elimu nchini.
 Vile vile Mtandao huu umeshaandaa waraka maalumu kwa Waziri wa Elimu unaotoa muongozo wa namna taifa litakavyofanikisha kuwa na Muafaka wa kitaifa katika sekta ya Elimu nchini ambao tutauwasilisha wizarani mapema wiki ijayo. 

Mwisho kabisa, tunaomba viongozi wote wa dini na wale wanaoamini, kuendelea kumwombea Mh. Raisi n a viongozi wengine ili waongoze taifa hili kwa hekima na busara na kwa kufuata taratibu, kanuni na sheria za nchi hii.




No comments:

Post a Comment