Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini,Alvaro Rodriguez
akizungumza katika mkutano wa Baraza Kivuli la Umoja wa Mataifa kuhusu
Vijana kutoka nchi nane Afrika uliofungwa jana kwenye makao makuu ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha .

Mratibu wa Kongamano hilo Marx Chocha akizungumza jambo kwenye mkutano huo.

Vijana wakisikiliza kwa makini mada mijadala iliyokua inatolewa.

Ushiriki wa vijana wa kike ulipewa umuhimu wa kipekee katika
mkutano huo na walionesha uwezo wao katika kujadili masuala mbalimbali
yakiwemo ajira ,usalama na amani na mabadiliko ya tabia nchi.

Mshiriki kutoka Zanzibar,Asma Omar akipokea zawadi yake baada ya
kuibuka mshindi katika kusambaza habari za mkutano kwa njia ya mitandao

Mshiriki kutoka jijini Dar es Salaam,Lilian Kimani akipokea cheti
chake baada ya kutambuliwa kufanya vizuri kama mkuu wa Itifaki kwenye
mkutano huo.

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini,Alvaro Rodriguez akimkabidhi mmoja wa vijana cheti cha kutambua mchango wake .
SERIKALI YAAHIDI KUVIPATIA MAJI VIJIJI VINAVYOZUNGUKA BOMBA KUU LA MAJI LA ZIWA VICTORIA NA MAENEO YA PEMBEZONI MWA TANZANIA.
Serikali
imesema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 itatekeleza mradi wa
maji katika vijiji 100 vilivyo pembezoni mwa bomba kuu la maji
linalotoka ziwa Victoria hadi Kahama na Shinyanga ili kuwawezesha
wanachi wanaoishi katika vijiji hivyo kupata huduma ya maji safi na
salama.SHINDANO LA MAISHA PLUS MSIMU WA 5 LAZINDULIWA RASMI, KUONYESHWA MOJA KWA MOJA NA AZAM TV
Mkurugenzi
wa Azam Media Tido Mhando (Kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa
Maisha Plus East Africa Mkurugenzi wa Maisha Plus East Africa msimu wa
5 ambapo shindano linatarajiwa kuanza hivi karibuni itakapotangazwa
ratiba ya kutafuta washiriki wa shindano hili mikoani na nchi zingine za
Afrika Mashariki, kulia ni mmoja wa waandaji wa shindano hilo Bw.
Masoud Kipanya, Masoud Kipanya ni miongoni mwa waanzilishi wa Maisha
Plus na mtangazaji wa kipindi hicho ambacho huandaliwa na kampuni ya
DMB Company Limited na mwaka huu inandaa kwa udhamini mkubwa wa Azam
Media, Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika jana katika studio za Uhai
Productions – Azam, Tabata jijini Dar es salaam.

Joyce Fisoo Katibu Mtendaji wa bodi ya filamu Tanzania akizungumza
mawili matatu wakati wa uzinduzi huo kama mgeni mwalikwa lakini pia kama
mdau muhimu wa shindano hilo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo
Mmoja wa waandaji wa shindano hilo Bw. David Seburi akizungumza na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya waandaji wa shindano la Maisha Plus kulia Francis Bonga na
David Sevuri wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo iliyofanyika
jana.Jikho Man na Vitalis Maembe wakitoa burudani wakati wa hafla hiyo
iliyofanyika jana.
Mwandaaji
wa shindano hilo Bw. Masoud Kipanya akizungumza na baadhi ya washiriki
waliowahi kushiriki katika shindano hilo kulia ni Abdul aliyekuwa
mshindi.
Aliyewahi kuwa mshindi wa shindano hilo Abdul akizungumza na wageni waalikwa katika uzinduzi huo uliofanyika jana.
Baadhi ya wafanyakazi wa Azam Media wakiwa katika hafla hiyo.
Mwanahabari na Bloger John Bukuku akihojiwa na mtangazaji wa Azam Tv
Benerick ambaye pia alikuwa ni mmoja wa washiriki wa msimu uliopita wa
Maisha Plus.
=============================================
MAONESHO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI YALIYOANDALIWA NA AGRIPROFOCUS YAFANYIKA UWANJA WA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI.
Mgeni
Rasmi katika maonesho ya Wakulima na Wagaji ,Mkuu wa idara ya Utumishi
na Utawala Manispaa ya Moshi,Wencelaus Lindi akisoma hotuba ya ufunguzi
wa maonesho hayo yaliyoandaliwa na Mtandao wa kusaidia Wakulima wa
AgriProFocus yanayofanyika katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika
mjini Moshi.

Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya
viongozi wa makampuni ya mafuta (hawapo pichani) wakati wa ziara ya
kukagua matanki ya kuhifadhia mafuta leo jijini Dar es salaam ili
kujionea hali ya upatikanaji wa mafuta ya ndege baada ya kugundulika
baadhi ya shehena ya mafuta hayo yaliyoingizwa nchini yalikuwa
yamechanganyika na mafuta ya petroli.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya
viongozi wa makampuni ya mafuta wakati wa ziara ya kukagua matanki ya
kuhifadhia mafuta leo jijini Dar es salaam ili kujionea hali ya
upatikanaji wa mafuta ya ndege baada ya kugundulika baadhi ya shehena ya
mafuta hayo yaliyoingizwa nchini yalikuwa yamechanganyika na mafuta ya
petroli.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongozana na baadhi ya
viongozi wa makampuni ya mafuta wakati wa ziara ya kukagua matanki ya
kuhifadhia mafuta leo jijini Dar es salaamWaziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo akiongozana na baadhi ya viongozi wa makampuni ya
mafuta wakati wa ziara ya kukagua matanki ya kuhifadhia mafuta leo
jijini Dar es salaam
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya
viongozi wa makampuni ya mafuta wakati wa ziara ya kukagua matanki ya
kuhifadhia mafuta leo jijini Dar es salaam eneo yalipo matanki ya mafuta
ya kampuni ya GAPCO ili kujionea hali ya upatikanaji wa mafuta ya ndege
baada ya kugundulika baadhi ya shehena ya mafuta hayo yaliyoingizwa
nchini yalikuwa yamechanganyika na mafuta ya petroli.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni wa Kampuni ya Oryx Energies Godifrey Fernandes
akimuonesha Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo baadhi ya
maeneo yanapohifadhiwa mafuta wakati wa ziara ya kukagua matanki ya
kuhifadhia mafuta leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo (wa pili mtasari wa kwanza
kulia) akiongozana na baadhi ya viongozi wa makampuni ya mafuta eneo la
“Deport” ya PUMA wakati wa ziara ya kukagua matanki ya kuhifadhia mafuta
katika leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya
madereva wanaosafirisha mafuta ndani na nje ya nchi leo jijini Dar es
salaam.(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
Balozi
wa Tanzania nchini Kenya, Dk. John Haule akipiga picha ya pamoja na
wachezaji na viongozi wa timu ya soka ya Tanzania baada ya kuzungumza
nao na kuwatoa hofu ya maisha na usalama wakiwa Nairobi, Kenya. Taifa
Stars ipo Nairobi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya
Harambee Stars ya Kenya utakaofanyoka kesho Jumapili kwenye Uwanja wa
Moi Kasarani.
Kipa
wa timu ya soka ya Tanzania-Taifa Stars, Deogratius Munishi maarufu kwa
jina la Dida, akifanya mazoezi ya kuzuia penalti kwenye Uwanja wa Camp
Toyoyo uliopo Jericho, nje kidogo ya jiji la Nairobi. Taifa Stars ipo
Nairobi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Harambee
Stars ya Kenya utakaofanyoka kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Moi
Kasarani.
Kikosi
cha timu ya soka ya Tanzania-Taifa Stars, kikifanya dua kwenye Uwanja
wa Camp Toyoyo uliopo Jericho, nje kidogo ya jiji la Nairobi. Taifa
Stars ipo Nairobi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya
Harambee Stars ya Kenya utakaofanyoka kesho Jumapili kwenye Uwanja wa
Moi Kasarani.
Mshambuliaji Elius Maguri na Kiungo Hassan Kabunda wakipumzika katika mazoezi hayo.
Kikosi
cha timu ya soka ya Tanzania-Taifa Stars, kikikifanya dua kwenye Uwanja
wa Camp Toyoyo uliopo Jericho, nje kidogo ya jiji la Nairobi. Taifa
Stars ipo Nairobi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya
Harambee Stars ya Kenya utakaofanyoka kesho Jumapili kwenye Uwanja wa
Moi Kasarani. (Picha na Alfred Lucas wa TFF).




Na Lorietha Laurence








No comments:
Post a Comment