TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, June 3, 2016

Wazanzibari wahimizwa kupanda miti



Mzee alisema ni jambo la kusikitisha kwamba mazingira ya Zanzibar yamegeuka kutoka rangi ya kijani iliyokuwepo zamani na kuwa yabisi, hali inayosababisha kuongezeka kwa joto.“Bila miti, viumbe hutaabika na nchi inakuwa kavu na maradhi hasa presha huongezeka kila uchao. Lazima tuzinduke kwani tusipopanda miti, tunakaribisha janga kwa taifa,” alisema Mzee. 

Aidha alivitaka vyombo vya habari kuandaa vipindi na makala mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kupanda miti.
Mapema, Mwenyekiti wa jumuiya ya Green World Family Foundation iliyodhamini zoezi hilo Nazir Ahmad Bachoo, alisema jumuiya yake inathamini mazingira na imeamua kulifanya zoezi la upandaji miti kuwa endelevu.

Alisema ni jambo lililo wazi kwamba dunia nzima sasa inalia na hali ya joto litokanalo na ongezeko la hewa ukaa (carbon dioxide), inayosababishwa na upungufu wa miti na kuongezeka kwa vyombo vya usafiri barabarani vinavyozalisha moshi kwa wingi.“Umefika wakati sasa kila mmoja ahamasike kupanda na kuitunza miti katika eneo analoishi na yale yanayomzunguka, ili ilete manufaa kwa kizazi cha sasa na kijacho,” alisisitiza.

Kwa upande wake, mratibu wa zoezi hilo na mwanaharakati wa mazingira Mohammed Abdulrahman Bajbeir, alisema Zanzibar imejaaliwa kuwa na wataalamu wengi wa masuala ya mazingira, lakini bado hawajatumika kikamilifu kuisaidia nchi.

Kwa hivyo amezishauri mamlaka za juu kutanabahi na janga la kimazingira linaloinyemelea Zanzibar kutokana na utashi wa binadamu ambao wamekuwa wakikata miti ovyo bila kupanda mingine.
“Zanzibar ya sasa sio kama ile ya zamani ambayo ilijaa kila aina ya miti pembezoni mwa barabara na mitaani. Tunafyeka miti kujenga nyumba za makaazi na maduka tukisahau kwamba miti ni muhimu kwa uhai wetu. Tubadilike,” alieleza Bajbeir.

Wananchi mbalimbali wa mitaa ya Malindi, Mchangani na Mbuyuni wakiwemo wanasoka wa zamani wa klabu ya Malindi SC walioshiriki zoezi hilo, walieleza umuhimu wa kuilinda miti hiyo ili kuunusuru uwanja wa michezo, kwani umekuwa ukiharibiwa sana na watu wanaoweka magari pamoja na mifugo.

Jumla ya miti 41 ya aina mbalimbali ilipandwa kuzunguka uwanja huo, na itakuwa ikilindwa na wananchi kwa kushirikiana na vijana wa ulinzi shirikishi na polisi jamii wa shehia ya Malindi.

No comments:

Post a Comment