TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, June 2, 2016

WAZIRI WA MALIASILI PROF. JUMANNE MAGHEMBE AIOMBA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KWA VITENDO KATIKA VITA DHIDI YA UJANGILI




Alieleza kuwa changamoto kubwa inayoikabidili hifadhi ya Selous ni ujangili ambao kwa kiasi kikubwa umesababisha idadi ya Wanyamapori hususani tembo kupungua kwa kasi kubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma.
Alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa mwaka 1986 idadi ya tembo katika pori hilo ilikuwa  50,000, idadi ambayo iliongezeka mwaka 2003 na kufikia 70,000 baada ya Serikali ya Ujerumani kusaidia kuanzishwa kwa Mpango wa Kuendeleza Selous (Selous Conservation Program) na Serikali ya Tanzania kukubali aslimia 50 ya makusanyo yanayotokana na utalii yabaki kuendeleza uhifadhi katika pori hilo.
Alisema kuwa baada ya mradi huo kuisha na mfumo wa “retention” kuondolewa na Serikali hali ilibadilika na kuwa mbaya zaidi ambapo kati ya mwaka 2008 na 2011 vitendo vya ujangili viliongezeka maradufu, sensa ya mwaka 2013 ilionesha idadi ya tembo hao kupungua hadi kufikia 13,000.
Prof. Maghembe aliongeza kuwa pamoja na hayo Serikali imejipanga kuhakikisha Wanyamapori wanalindwa usiku na mchana na kwamba wale wote wanaojihusisha na vitendo vya ujangili watakamatwa na kufikishwa mahamani ili sheria ichukue mkondo wake.


Prof. Maghembe ameeleza kuwa pamoja na mambo mengine ili kukomesha ujangili ni lazima mataifa yaliyoendelea ambayo ndiko yaliko masoko makubwa ya meno ya tembo na bidhaa zake kusitisha kabisa uingizwaji wa meno hayo katika nchi zao ili kukomesha biashara hii haramu.
“Kuna nchi ambazo tayari zimechukua hatua ya kukataza kabisa uingizwaji wa meno ya tembo nchini mwao, mfano Marekani, tunaiomba sana jumuiya ya kimataifa wakiwemo marafiki zetu China na nchi nyingine wakatae kabisa uingizwaji wa meno haya nchini mwao, hii itasaidia sana kukomesha biashara hii haramu” Alisema.
Katika hatua nyingine Prof. Maghembe aliwataka wafugaji walioingiza mifugo katika maeneo yote ya hifadhi nchini waondoe mifugo yao kwa hiari kabla ya kushinikizwa kufanya hivyo na Serikali kwa mujibu wa sheria.
Sheria ya Wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 Ibara ya 18 (2) inasema “Si ruhusa mtu yeyote kuingia na kulisha mifugo ndani ya Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu na Ardhioevu”
Prof. Maghembe alisema kuwa “mtandao wa ujangili unaanzia na watu wanaoingiza mifugo ndani ya hifadhi, hivyo ni lazima sheria zifuatwe  na waondoke mara moja, watakaokaidi sheria itafuata mkondo wake na mifugo itakayokamatwa itataifishwa na Serikali kwa mujibu wa sheria za nchi, sheria hizi hazina tofauti na sheria zinazokataza watu wasijenge mabondeni au kwenye hifadhi za barabara”  
Awali akitoa taarifa, Meneja wa Pori hilo la Akiba la Selous  Mabula Misungwi alieleza baadhi ya changamoto kuu zinazoikabili hifadhi hiyo kuwa ni pamoja na ujangili, miundombinu mibovu ya barabara kwa ajili ya doria na vifaa ikiwemo magari ya doria na nyumba za watumishi.

No comments:

Post a Comment