TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, May 14, 2012

FUNDI BAJAJ MADAI YA ASKARI Gemini kudhamini mchezo wa Judo Waislaamu watakiwa kupuuza wanapinga sensa IFNA yashauri Taifa Queens icheze Kombe la Dunia TOZI Good Hope kuibua makocha, Waamuzi Songea Ngoma NCCR-Mageuzi wapata pigo, Athanasi ajivua kundini KATUNI Magereza ziwe vyuo cha maadili kwa wafungwa Mama Tunu Pinda awajaza 'manoti' Taifa Queens TIC Vijana Yanga wamuangukia Manji


Posted: 14 May 2012 12:22 AM PDT
Mbunge wa jimbo la Kisesa (CCM) Bw.Luhaga Mpina akihutubia mkutano wa kuhamasisha maendeleo jimboni mwake
Posted: 14 May 2012 12:16 AM PDT

Fundi wa kutengeneza pikipiki za gurudumu tatu (Bajaj) jina (halikufahamika) akining'inia kwenye chombo hicho wakati akikifanyia majaribio bila kujali usalama wake, kama alivyokutwa Magomeni Mikumi, Dar es Salaam jana. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 14 May 2012 12:13 AM PDT

Posted: 13 May 2012 11:50 PM PDT

Na Mwali Ibrahim

KAMPUNI ya Gemini  Corporation imejitokeza kudhamini mashindano ya taifa ya mchezo wa Judo yanayotarajiwa kufanyika Mei 26 hadi 27 Landmark Ubungo  Dar es Salaam.
Mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha wachezaji kutoka Tanzania Bara na Zanzibar watakaochuana kuwania ubingwa huo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Yuil Tarverdyan alisema kutokana na mapenzi ya mchezo huo kampuni yake imejitokeza kugharamia mashindano hayo kwa mara ya pili ikiwa ni katika kugharamia gharama zote za mashindano.
Alisema, gharama hizo zitahusisha mahali pa kufanyia mashindano zawadi ambazo nifedha kwa washindi wa mashindano hayo.
Alisema, kutokana na chama cha Judo nchini (JATA) kwa sasa kuwa na viongozi wapya, anatarajia kufanya kikao cha pamoja na viongozi hao ambao tayari wameshawasiliana kuhusu udhamini huo, ambapo gharama za mashindano pamoja na zawadi atazitaja katika kikao hicho.
Alisema licha ya kuwa na mahusiano mazuri na uongozi uliopita hakusita kuacha kudhamini mchezo huo kutokana na mapenzi yake katika mchezo huo ambao pia huchezwa nchini kwao Ujerumani.
Kwa mujibu wa  aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Kashinde Shaaban aliyezungumza kwa simu alisema wanaitambua kampuni hiyo kutokana na kujitokeza kuwadhamini wakati wa uongozi wao, ambapo kwa sasa kiongozi huyo amefungiwa maisha.
"Alinipigia kutaka kudhamini kutokana na kufahamiana na uongozi wetu kipindi hicho, lakini nilimfahamisha kuwa sipo tena madarakani na kumtaka kuendeleza udhamini huo kwa viongozi waliokuwepo madarakani sasa," alisema Kashinde.
Posted: 13 May 2012 11:32 PM PDT

Na Anneth Kagenda

MKURUGENZI wa Taasisi ya Kiislam ya  Peace Foundation Tanzania (TIPF), Bw. Sadiki Godigodi, amewataka Watanzania kupuuza ushawishi unaotolewa na baadhi ya watu wa dini hiyo wa kuwataka wasishiriki kwenye sensa kwani hakuna nchi ambayo inaweza kukaa bila kujua idadi ya wananchi wake.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, alisema kuwa ni muda muafaka kwa waumini wa dini hiyo kutosikiliza ushawishi unaotolewa na baadhi ya watu badala yake wakubali kushiriki vyema kwenye sensa hiyo.
"Tunawaomba waislam, wakristo na Watanzania wote kwa ujumla kujitokeza kutoa ushirikiano wa zoezi la kuhesabu watu na makazi linalotarajia kuanza hivi karibuni na wapuuze kauli za watu wachache wenye malengo ya kujipatia maslahi binafsi," alisema.
Alisema watu hao ambao wamekuwa wakishawishi wenzao kutoshiriki Sensa ni kikuzwa, kwani hii ni fursa muhimu.Katika hatua nyingine (TIPF) ilimpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua yake ya kusikiliza mawazo ya wabunge na badaye kuchukua hatua mbadala ya kuwawajibisha wale wote walioonekana kuwa si waadilifu kwenye Baraza la Mawaziri.
"Kwanza kabisa taasisi yetu inapenda kumpongeza Rais Kikwete kwa uamuzi wake wa kusikia kilio cha wabunge hatimae kuwawajibisha mawaziri wenye kashfa za ufisadi.
Posted: 13 May 2012 11:31 PM PDT
Na Amina Athumani

SHIRIKISHO la Kimataifa la Mchezo wa Netiboli (IFNA), limekipa Changamoto Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) kuiingiza timu ya Taifa ya Netiboli (Taifa Queens) kwenye michezo ya Dunia.
Akizungumza Dar es Salaam juzi, Mwakilishi wa IFNA,  Joan Smith alisema Tanzania imepiga hatua kubwa katika mchezo huo hususani kikosi cha Taifa Quens kilichoshiriki michuano ya Afrika kimeimarika tofauti na alichokiona mwaka 2009 katika  mashindano kama hayo.
Alisema pia maandalizi yaliyofanywa na CHANETA kwa mwaka huu yamekuwa ni mazuri zaidi na kwamba chama hicho kina uwezo pia wakuandaa mashindano ya Dunia endapo watafanikiwa kuwa na Uwanja wa Ndani wa kisasa.
Alisema kutokana na maandalizi waliyofanya CHANETA, IFNA inao uwezo wa kuipa kibali Tanzania kuandaa mashindano ya Dunia na kwamba cha msingi ni Serikali ya Tanzania kukisaidia chama hicho katika kuhakikisha kinapata kiwanja cha ndani chenye hadhi ya kisasa.
Tanzania ni mara ya pili kuandaa michezo ya Afrika ambapo mara ya kwanza iliandaa michezo hiyo mwaka 2009 na iliiwezesha Tanzania kupanda viwango vya kimataifa vya mchezo huo vinavyotambulika na IFA.
Kwa sasa Tanzania ipo nafasi ya 20 katika viwango vya mchezo huo na  ipo nafasi ya tatu kwa viwango vya Netiboli Afrika (AN) ambapo kupitia mashindano yaliyomalizika juzi huenda Tanzania ikapanda viwango vya Afrika.
Posted: 13 May 2012 11:30 PM PDT

Posted: 13 May 2012 11:28 PM PDT
Na Mhaiki Andrew, Songea

SHIRIKA lisilokuwa la Kiserikali la Klabu ya michezo ya Good Hope la mkoani Ruvuma, lina mpango na mikakati ya kutoa mafunzo ya ukocha na waamuzi kwa wanafunzi wa shule za Sekondari ikiwa na lengo la kuibua na kuendeleza taaluma ya michezo mkoani hapa.
Akizungumza mjini hapa juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Joseph Mapunda alisema mafunzo hayo yatalenga wanafunzi wa shule hizo za Sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha tatu katika kuwapa taaluma ya michezo badala ya kutegemea makocha kutoka nje ya mkoa kuja kufundisha.

Alisema Shirika hilo limejiwekea malengo endelevu katika kusaidia kuinua michezo hiyo kitaaluma ambapo alidai baada ya kukamilika zoezi hilo kwa shule za Sekondari pia mafunzo hayo yatatolewa kwa vijana wa shule za msingi kwa kuanzia darasa la tano.
Alisema kabla ya kuanza kwa utoaji wa mafunzo ya ukocha kwa wanafunzi hao, alidai bodi ya Shirika hilo limekutana na kuweka mikakati itakayowezesha  kufanikisha zoezi hilo.
Alisema katika mapendekezo yao wamedai wataanzia na shule za Sekondari katika wilaya mbili  za Songea na Namtumbo na baadaye Nyasa, Mbinga na Tunduru.
Aliongeza mafunzo hayo yatatolewa kwa michezo 10 ambayo baadhi ni soka, netiboli, ngumi, riadha  na mpira wa wavu.
Posted: 13 May 2012 11:27 PM PDT

Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Mkoani Simiyu (CCM),  Luhaga Mpina (mwenye vazi la chama) akishiriki kucheza ngoma za utamaduni wakati alipofanya ziara katika Kata ya Kisesa kwa ajili ya kutoa zawadi kwa vikundi vya ngoma za Wagika na Wagalu na kuimarisha utamaduni jimboni humo. (Picha na Suleiman Abeid)
Posted: 13 May 2012 11:23 PM PDT

Na Anneth Kagenda

ALIYEKUWA mgombea Ubunge Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi Bw. Mawazo Athanasi amejiondoa kwenye chama hicho kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kukosa imani na Mwenyekiti wake Bw. James Mbatia.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam mara baada ya kufika jijini hapa akitokea Kigoma, alisema kuwa amechukua maamuzi hayo magumu kutokana na mwenyekiti wake kuwa mwanachama wa CCM kutokana na kwamba kama angekuwa ni mwanachama wa NCCR- Mageuzi asingekubali kupewa cheo cha wanawake wa CCM (Viti Maalum).
"Awali tulikuwa tunajiuliza maswali mengi kwamba Bw. Mbatia ni wa chama chetu au CCM...sasa ukweli tumeupata kwamba ni wa CCM, pia ninajiuliza kama angekuwa na nia ya dhati na chama basi angekataa cheo hicho ambacho ni cha wanawake wa viti maalum CCM, lakini ninajiuliza je? Huko bungeni anaenda kufanya nini na anakitetea chama gani.
"Niko katika chama hiki tangu mwaka 2003, lakini nilikuwa nashangazwa na mwenendo wa chama changu, baada ya kuona mambo yanazidi kuharibika ngoja nikae pembeni kwani chama hiki hiki kilishindwa kunitetea hata nilipokuwa nashughulikia kesi yangu ambapo nilishindwa kutimiza masharti ya kupeleka sh. milioni tano mahakamani wakati milioni mbili zilikuwa zimepatikana, lakini nikakosa milioni tatu," alisema.
Aidha, alisema kuwa awali Bw. Mbatia alimwambia (Bw. Athanasi) kwamba aachane na kesi hiyo ambayo aliamini kwamba angeshinda kutokana na kwamba aliibuka kidedea cha mshindi wa pili na kwamba kura zake ziliibiwa na Bw. Christopher Chiza wa CCM ambapo alisema kuwa kitendo hicho cha kuhujumiwa na chama chake hakukifurahia.
Alisema, pia anakubali uteuzi wa Rais wakati akijua kuwa tayari alimteua mwizi wa kura zake (Chiza) kuwa Waziri na kusema kuwa iweje ampende Bw. Mbatia wakati anajua kuwa aliwaibia kura katika Jimbo la Buyungu na kusema kuwa kilichoendelea kumuudhi ni viongozi wa NCCR-Mageuzi kuunga mkono uteuzi wa Bw. Mbatia.
Hata hivyo aliwataka vijana wote wa mkoani Kigoma ambao wako kwenye chama alichokihama kuondoka mara moja kwa madai kuwa chama hicho kinakufa na kuwa CCM kwani viongozi wake wataendelea kuongopewa kwa kupewa vyeo na Rais Jakaya Kikwete.
Posted: 13 May 2012 11:20 PM PDT

Posted: 13 May 2012 11:19 PM PDT
Na Darlin Said

KWA nyakati tofauti Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imekuwa ikitoa taarifa juu ya mlundikano wa wafungwa na hali mbaya ya magereza nchini.
Mfungwa ni mtu aliyeadhibiwa kwenda Gerezani baada ya kutenda makosa au uhalifu katika jamii ili kujifunza na kutorudia kosa hilo.

Adhabu hutolewa kisheria na mahakama ambapo hutumikia adhabu hiyo huku akisimamiwa na kurekebishwa tabia zao.Mfungwa hupokea mafunzo mbalimbali na kupelekea kupata ujuzi katika ufundi, ukulima, ufugaji na fani nyingine nyingi.Ni tegemeo la serikali na jamii kuwa, mfungwa anamaliza kutumikia kifungo chake awe amebadilika kitabia na kuwa raia mwema anayeweza kushiriki katika kuleta maendeleo ya jamii inayomzunguka.Kwa kulitambua hilo Chama cha kurekebisha mwenendo wa watu waliomaliza kifungo Tanzania (E.R.S.T) kilianzishwa mwaka 2009 chini ya mwenyekiti  Bw.Shafii Kondo ili kuwapatia mafunzo.

Pia, ni kuwaunganisha wafungwa waliomaliza vifungo vyao na kuwarekebisha
tabia zao ili wasiweze kufanya tena uhalifu ambao utawasabishia kurudi tena gerezani.Lengo lengine ni kutoa elimu katika jamii ili waweze kuwapokea na kushirikiana nao katika shughuli mbalimbali za maendeleo kwa kutumia ujuzi walioupata gerezani.Vilevile kuhakikisha wanasimamia vema haki za wafungwa zilizosaulika  mfano haki ya kupiga kura na ya kukutana na wanandoa wenzao.

Pia kuhakikisha kwamba wanatoa  msaada wa kifedha, vifaa na rasilimali ardhi ili iwe changamoto kwa waliomaliza vifungo kujiunga  na Taasisi za aina  hii ili waweze kujiepusha  kujiingiza katika vitendo vya uhalifu.Ili waweze kufanikisha malengo yao chama kimeanzisha miradi mbalimbali ikiwemo shughuli za kuchana mbao, karakana, ukulima na ufugaji.

Kwa uhalisia tunaona kwamba, katika magereza nchini kuna matatizo  ya kisheria yanayopelekea wafungwa kukosa uhuru wao ambayo ni kinyume na haki za binaadamu.Kwa mfano katika sheria zetu wafungwa hawana haki ya kupiga kura kumchagua kiongozi anayemtaka na pia hawana haki ya kukutana na wanandoa wao ambapo ni kinyume na haki za kibinaadamu.Serikai inatakiwa kubadili mfumo wa sheria ya magereza kutoka mfumo wa kikoloni  ambazo zinaonekana kandamizi kwa wafungwa na kuwanyima haki zao za msingi.

Sheria ziliopo ni za kikoloni wakati wafungwa ni wa kisasa, pia washirikishwe kutoa mawazo  yao katika mchakato wa kubadilisha katiba kwani ni haki yao ya msingi. Katika magereza bado sheria hazijaboreshwa ukilinganisha na sehemu nyingine hali inayopelekea kuwa na matatizo mbalimbali ikiwemo msongamano wa wafungwa.Magereza mengi yamefurika wafungwa na mahabusu kupita kiasi, huduma za chakula, matibabu na haki nyingine za wafungwa zimekuwa ama haziheshimiwi kabisa au pale zinapoheshimwa ni kwa kiwango cha chini kabisa.

Nionavyo gerezani kuna matatizo mengi ambayo wafungwa wanakumbana nayo ambao aidha yanasabashwa na sheria zilizopo ambayo wafungwa ndio wanayoyafahamu vema kuliko mtu yeyote.
Mfano wafungwa kutoruhusiwa kuwa karibu na waume/wake zao ni tatizo kubwa ambalo linaweza ikapelekea tatito la ushoga gerezani.Lakini kama kungekuwa na sheria inayoruhusu wafungwa kukutana na wake zao ingesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo hilo na maambukizi ya VVU.

Aidha upande wa serikali itilie mkazo kwa kufanya magereza yawe ni vyuo vya mafunzo ya kuwafanya wafungwa wapate ujuzi mbalimbali na siyo sehemu ya kupata adhabu na unyanyaji .Tunafahamu na kutambua kuwa magereza siyo hoteli ya kitalii kwa maana hiyo iwe na huduma za kiwango cha juu sana, lakini pia siyo sehemu ya kuwatesa wafungwa na kukataa walau kutambua haki zao za msingi.

Tujifunze kutoka kwa ngugu zetu wa visiwani badala ya kuita magereza wanaita vyuo vya mafunzo hii inasaidia jamii kuwaona wafungwa ni wenzetu ambao wapo mafunzoni.Kwa upande wa magereza ya watoto, serikali ihakikishe kuwa inawapatia watoto hao elimu bora na wasiwape adhabu kubwa zisizo endana na umri wao. wa kufanya hivyo tunaweza kujenga taifa linalowajali wafungwa  ingawaje  wametenda makosa au uhalifu katika jamii.

Serikali imetakiwa kuwashirikisha wafungwa katika mchakato mzima wa kupiga kura, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kupata haki ya kukutana na wenzi wao hasa wanapokuwa  kifungoni.
Posted: 13 May 2012 11:17 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

BAADA ya kuwa wa pili katika michuano ya netiboli ya Afrika kwa kuifunga Botswana mabao 32-23,Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ametimiza ahadi aliyoitoa kwa timu ya Taifa ya Netiboli (Taifa Queens) kwa kutoa jumla ya sh. milioni 20.8.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Irene Bwire, ilieleza kwamba Mama Pianda alitoa sh. milioni moja kwa kila mchezaji endapo wangetwaa ubingwa wa kombe hilo ambayo mashindano yake yalimalizika juzi na Malawi kutwaa ubingwa.
Ilieleza Mama Pinda ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kuisaidia timu hiyo, alitimiza ahadi hiyo juzi katika hafla fupi ya kukabidhi mfano wa cheki iliyofanyika juzi usiku, Dar es Salaam.

"Wachezaji 16 walipewa sh. milioni moja kila mmoja, na maofisa sita wa timu walipewa sh. 800,000 kila mmoja, hivyo kufanya jumla ya sh. milioni 20.8," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Akizungumza na wachezaji hao, viongozi wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA), na baadhi ya Wake wa Viongozi ambao ni wanachama wa New Millenium Women Group, Mama Pinda aliwapongeza wachezaji hao kwa jinsi walivyojituma na kufanikiwa kushika nafasi ya pili.

Aliwataka wachezaji hao kuzidi kujituma zaidi hata katika mashindano yatakayofanyika mwakani nchini Malawi na kwamba walifanya kazi kubwa kuifunga timu ngumu kama Botswana.
Akitoa shukrani kwa niaba ya wachezaji wenzake, nahodha wa timu hiyo, Lilian Sylidion alisema ahadi ya Mama Pinda ambayo aliitoa wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo iliwapa hamasa na kuchochea kupatikana kwa ushindi huo.
TIC
Posted: 13 May 2012 11:11 PM PDT

Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bi. Beatrice Chonjo (kushoto) na Mkurugenzi wa Program ya kusaidia wajasiriamali wa nchi zinazoendelea ya Finnpartnership ya Finland, Bi.Siv Ahlberg, wakizungumza na wadau wakati wa mkutano huo ulitayarishwa na ubalozi wa Finland na TIC, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. (Na Mpigapicha Wetu)
Posted: 13 May 2012 11:08 PM PDT

Na Elizabeth Mayemba

VIJANA wa Klabu ya Yanga, wamemuangukia aliyekuwa Mfadhili wa timu hiyo, Yusuph Manji aje kuinusuru hasa katika kipindi hiki kigumu walichonacho.
Klabu hiyo hivi sasa ipo katika mvutano mkubwa kati ya uongozi uliopo madarakani chini ya Llody Nchunga ambaye Baraza la Muafaka la Wazee pamoja na vijana wa klabu hiyo wanashinikiza kiongozi huyo kujiuzulu kutokana na kudai ameshindwa kuiongoza timu.

Wakizungumza kwa niaba ya vijana wenzao katika kikao cha vijana kilichofanyika jana Dar es Salaam ambacho kilihudhuriwa na zaidi ya wanachama 200, Omari Chambuso (003850), Hussein Mfaume (00607) na Waziri Jitu (001732), walisema wanataka Mkutano Mkuu ufanyike Mei 20, mwaka huu badala ya Julai 15 kama alivyotangaza Nchunga.

Walisema tarehe hiyo waliyopanga ndiyo tarehe ambayo Nchunga atakutana na Wazee wote wa Yanga na kwamba kama ana uwezo wa kukutana na wazee wote ni bora uwe mkutano mkuu kabisa.
"Nchunga amepanga Mkutano Mkuu ufanyike Julai lakini ni mbali sana, hivyo sisi tunataka ufanyike Mei 20 na pili tunataka ajiuzulu yeye pamoja na uongozi mzima," walisikika wakisema kwa nyakati tofauti.

Pia walimuomba Manji arudi kuisaidia klabu hiyo kwani uongozi uliopo madarakani wamedai umeshindwa kuiongoza timu hiyo kutokana na kukabiliwa na madeni mengi.Waliongeza watajihidi vijana kwa umoja wao kuhakikisha wanajipanga kusaidia katika suala zima la usajili hususani katika kipindi hiki ambacho timu yao inakabiliwa na mashindano ya Kombe la Kagame.

No comments:

Post a Comment