TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, May 15, 2012

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, Linapozungumza



 
 
ASPIRE KUANZA KUSAKA VIPAJI MEI 21
Mchakato wa kusaka vipaji kwa chipukizi wenye umri chini ya miaka 14 kupitia mpango wa kukuza vipaji wa Aspire Football Dream ambao uko chini ya Idara ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utafanyika kuanzia Mei 21 mwaka huu.
Vituo vitakavyohusika ambavyo kila kimoja kinatakiwa kuwa na watoto wasiopungua 176 na tarahe ya kufanyika mchakato huo kwenye mabano chini mng’amua vipaji (scout) kutoka Hispania ni Morogoro (Mei 21 mwaka huu saa 3 asubuhi) na Bagamoyo mkoani Pwani (Mei 21 mwaka huu saa 8 mchana).
Vingine ni Kawe, Dar es Salaam (Mei 22 mwaka huu saa 3 asubuhi), Makongo, Dar es Salaam (Mei 22 mwaka huu saa 8 mchana) na Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam (Mei 26 mwaka huu saa 9 mchana).
 
Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani kwa Tanzania una jumla ya vituo 14. Vituo vingine ni Kigamboni, Tandika, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni na Tabata.
 
Watoto watakaochaguliwa katika mchakato huo watakwenda katika mchakato mwingine kwa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki utakaofanyika jijini Nairobi, Kenya.
 
Watakaofuzu kutoka hapo ndiyo watakaokwenda kwenye vituo vya kuendeleza vipaji (centre of excellence) vya Aspire Football Dreams. Aspire ina vituo viwili vya kuendeleza vipaji ambavyo viko Doha, Qatar na Dakar, Senegal.
 
TWIGA STARS KUJIPIMA KWA BANYANA BANYANA
Timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) inatarajia kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini (Banyana Banyana) itakayofanyika Mei 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Happy Mothers Day - Tumsaidie Mama Yetu Mpendwa

 
Ni siku moja tu imepita tangu tusherehekee siku ya akina mama Duniani.
Lakini si kila mwanamke anapata bahati ya kushereheka sikukuu kama hii ilihali wengine tukimshukuru Mungu kwa siku hii muhimu.
Mimi na Tanzania ilimhoji Mama yetu Mpendwa Christophina ambaye amekuwa akiteseka na maumivu ya mguu kwa muda mrefu. Hadi sasa amekwishapata mchango wa shillingi 710,000/= na anahitaji jumla ya shilingi 1,200,000/= kwa ajili ya operesheni. Hivyo amepungukiwa shillingi 490,000/=. Shime watanzania!
Anahitaji msaada wa matibabu. Hebu tumsikie na tumsaidie.
Namba za simu na account zilizotolewa hapo ni za kwake mwenyewe kama kuna mtu atapenda kuwasiliana naye.
Hoyce Temu – A.k.a Mama Ruby
Mtangazaji – Mimi na Tanzania
Happy Mothers Day!

Exim Bank FC beats Stanbic FC in bankers’ soccer bonanza

Exim Bank Football Club (Exim FC) in a group photo shortly before the kickoff of their friendly match against Stanbic Bank team played yesterday at Karume grounds in Dar es Salaam. Exim beat Stanbic 3-2. Picture by our photographer.
By Staff Reporter

Exim Bank Tanzania FC beat Stanbic Bank FC 3-2 during a bankers’ soccer bonanza held at Karume Stadium in Dar es Salaam yesterday.
The Stanbic Bank FC looked superior in the first half emerging beating Exim Bank 2-1 during the first 45 minutes with Exim getting a consolation goal through Abass Digole that was scored in the 13th minute
Exim FC however made a coma back in the second half scoring an equalizer in the 64th minute through their striker Nobert Misana.
The bank’s equalizer created enthusiasm and moral for the team that consequently saw Exim bank score its third goal through Norbert Missana in the 82nd minute with Exim bank emerging winners after the final whistle.
Speaking shortly after the final whistle of the game, Norbert Missana who emerged as the game’s hero said the match was rather difficult as compared to their last match with Diamond Trust Bank.
 “Sincerely, we did not believe we would emerge victorious due to our poor performance in the first half.
“We managed to work upon our mistakes in the second half working as a team that saw us score an equalizer and a third goal (winner) in the second half. Am grateful that we managed to utilize the chances that have been generated in the second half,” he added.
The match was geared towards testing employees’ fitness in sports since sports activities play an important part in people’s lives especially after a hard day’s work.

Ufunguzi wa mkutano wa sayansi na mabadiliko ya tabia nchi mjini Bonn

Bi. Christiana Figeres, Executive Secretary wa  United Nations Framework Convention on Climate Change (UNFCCC) akifungua mkutano  wa kimataifa wa sayansi na taaluma wa mabadiliko ya tabia nchi, Mjini Bonn Ujerumani. (Picha na Evelyn Mkokoi Bonn)

WATU 120 WAFANIKIWA KUJENGEWA UWEZO SPRINGS OF HOPE TANZANIA

Shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kwa jina la Springs of
Hope –Tanzania lenye makao yake makuu Mjini Arusha  limefanikiwa
kuelimisha jumla ya watu 120 waishio kwenye mazingira magumu ikiwa ni
pamoja na kuwajengea uwezo jinsi ya kuweza kuanzisha miradi
midogomidogo ili kujikwamua na hali ngumu ya kimaisha  waliyo nayo.

Kutolewa kwa elimu hiyo kunafanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoani
hapa, huku wakilenga zaidi jamii iishiyo katika mazingira magumu
kutokana na kuwa  wengi wao wakishindwa kuwasomesha watoto wao
kutokana na ugumu wa maisha walio nao hivyo kuwaozesha ili kupunguza
gharama .

Akizungumza na Fullshangweblog, Kiongozi wa vikundi  hivyo kutoka  shirika
hilo ,Linus Hokororo  alisema kuwa mbali na kutoa elimu hiyo wameweza
kuwaelimisha kuunda vikundi vya watu 30 kwa lengo la kuweza
kukopeshana mikopo midogomidogo  pamoja na kuwawezesha wao kuunda
mfuko wa jamii  utakaowawezesha wao binafsi kujitatulia changamoto
mbalimbali za maisha , ikiwa ni pamoja na  kuwasaidia wao kuanzisha
saccos yao wenyewe bila kusaidiwa na mtu yeyote.

Alisema kuwa, baada ya elimu hiyo tayari jumla ya vikundi vinne vyenye
idadi ya watu 120 vimekwisha undwa huku wakiweza kuchangishana fedha
na kuanzisha miradi midogomidogo pamoja na kuweza kujiwekea akiba yao
 kwa ajili  ya kuwasomesha watoto wao ambao wengi wao wamekuwa
wakibakia majumbani tu kutokana na ukosefu wa ada.

‘Sisi tulifikia uamuzi wa kufanya hivi baada ya kuona kuwa, jamii
nyingi zimekuwa zikipata magonjwa mbalimbali ikiwemo ukimwi kutokana
na kuwepo kwa umaskini, hali inayowapelekea kuingia kwenye vishawishi
mbalimbali, hivyo kwa kufanya hivi elimu hii imewawezesha kuwatoa
kwenye mazingira magumu na kuweza kujiinua kuichumi kwa
ujumla.’alisema  .

Aliongeza kuwa, katika kufanikisha shughuli zao wamekuwa wakiwezeshwa
na wahisani mbalimbali ikiwa ni pamoja na  East Africa Adventure
Safari company ambao waliwapatia masaada wa kiasi cha USD 360 kwa
ajili ya kutoa elimu hiyo kwa jamii itokayo kwenye mazingira magumu.

Aidha alisema kuwa , elimu hiyo imewafikia watu waishio mazingira
magumu kutoka kata ya Bwawani, Oldonyosambu, Muriet  , kata ya Suye ,
Tengeru, Kimandolu na Sanawari.

Hokororo alisema kuwa, watu hao wametokea halmashauri ya Arusha
vijijini, halmashauri ya Meru na manispaa ya Arusha huku wakiendelea
kuongeza maeneo zaidi kulingana na watakavyoendelea kufanya uchunguzi
na kubaini maeneo yenye uhitaji huo.

TANZANIA YAWA TISHIO INDABA


Naibu Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini Bibi Tokozile Xasa (watatu kushoto) pamoja na Kurugenzi Mwendeshaji Biashara na viwanda wa Afrika Kusini Bibi Elizabeth Thabethe  (wa kwanza kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya waoneshaji kutoka Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Dk. Aloyce Nzuki (wan ne kushoto) alipotembelea Banda la Tanzania katika maonesho ya INDABA mjini Durban Afrika Kusini.
Na: Geofrey Tengeneza, Durban. 
 
Banda la Tanzania katika maonyesho ya Utalii ya Kimataifa ya INDABA yanayoendelea jijini Durban Afrika Kusini limeendelea kuvutia viongozi na watu wa kada mbalimbali kutoka ndani na nje ya Afrika Kusini wanaotembelea maonyesho hayo.  Miongoni mwa waliotembelea banda hilo shindwa kuzuia hisia zao hususan kwa maelezo na vielelezo vinavyoonesha uzuri na upekee wa vivutio vya utalii vya Tanzania na shughuli za utalii zinavyoendeshwa nchini ni Naibu Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini Bibi Tokozile Xasa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Viwanda na Biashara la Afrika Kusini Bibi Elizabeth Thabethe  ambao kwa pamoja walitembelea Banda la Tanzania na kujionea vielelezo mbalimbali sambamba na kupata maelezo yaliyowafurahisha sana kuhusu utalii wa Tanzania kwa ujumla.
Akizungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Dk Aloyce Nzuki na waoneshaji wa Tanzania kwa ujumla Naibu huyo waziri alifurahishwa na kuvutiwa na jinsi Tanzania kupitia Bodi ya Utalii ilivyojipanga katika kuitangaza Tanzania duniani  na jinsi ambavyo Tanzania imekuwa ni mshiriki mzuri wa maonesho ya INDABA na kukiri kuwa Tanzania imekuwa ikitoa changamoto kubwa kwa nchi nyingine wanachama wa SADC katika sekta ya Utalii. “Tanzania ni nchi tishio katika sekta ya utalii miongoni mwa nchi za SADC, ni nchi inayonivutia sana “ alisema Bibi Tokozile Xasa
Jumla ya makampuni 49 kutoka sekta binafsi na taasisi sita za serikali zinashiriki katika maonesho hayo ambayo ni makubwa kuliko yote barani Afrika. Maonesho haya hufanyika kila mwaka jijini Durban Afrika Kusini. Katika maonesho kama haya mwaka jana Banda laTanzania lilitunukiwa tuzo ya kuwa Banda Bora kuliko yote katika maonesho hayo miongoni mwa nchi za SADC.

Rais Kikwete afungua semina ya APRM kwa wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa mjini Dodoma leo asubuhi

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua semina ya Africa Peer Review Mechanism(APRM) kwa wajumbe wa Halmashauri kuu ya  CCM taifa katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo
Baadhi ya Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa wakihudhuria semina maalumu ya APRM iliyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo asubuhi(Picha na Freddy Maro)

VIJANA WATAKIWA KUZINGATIA ELIMU ILI KUZIKOMBOA NCHI ZAO KATIKA UTEGEMEZI


Mkurugenzi wa kituo cha utamaduni  ubalozi wa Iran, Morteza Sabouri, akifafanua jambo.
 
NA MWANDISHI WETU
VIJANA nchini wametakiwa kutambua kuwa chanzo cha mabadiliko ya kweli katika kila nchi duniani huanzia kwao, hivyo ni vema wakazingatia elimu ili kuzikomboa nchi zao kutoka katika utegemezi.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha utamaduni cha Jamhuri ya Kiislam  ya Watu wa Iran wakati akimkaribisha Profesa kutoka Chuo Kikuu cha Teheran, Kitivo cha Hadith na Sayansi, Atefeh Noor katika mkutano wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala jijini Dar es Salaam leo.
Alisema vijana ndio nguzo ya taifa, hivyo wanapo pata nafasi ya mafunzo katika Vyuo wasikubali kupoteza muda kwani kwa kufanya hivyo watakuwa hawakirudisha nyuma maendeleo ya nchi.
Naye Profesa Noor, katika mkutano huo, alisema baada ya miaka zaidi  ya 30 ya Mapinduzi,Iran imfanikiwa kupiga hatua za kimandeleo kutokana na nguvu za vijana.
Alisema iwapo vijana wataitumia elimu kunauwezekanao wa kuzikomboa nchi zao katika kutegemea misaada kutoka nchi nyingine.
Prefesa Noor alisema maendeleo ya kweli kila nchi hayawezi kupatikana iwapo nchi husika itakuwa ikitegemea misaada mbalimbali ya kutoka nje hivyo ni bora wakachukuwa majukumu ya kuondoa mfumo huo.
Aidha, alisema baada ya nchi yake kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo vikwazo kutoka ilivyokuwa ikiwekewa na Mashirika ya kimataifa imejaribu mbinu za kila aina kwa kuwatumia wasomi ambao ni vijana katika kujiondolea matatizo katika nchi hiyo.
Alibainisha kuwa pamoja na changamoto mbalimbalinchi hiyo inajivunia mafanikio katika nyanja mbalimbali ikiwamo kwenye sekta ya Afya, Elimu na Sayansi.
 
Profesa Noor alisema hali ya kuwekewa vikwazo imetokana na baadhi vyombo vya habari vya nchi za Mgharibi katika kile wanachodai kuwa nchi hiyo imekuwa ikikiuka baadhi ya maazimio ya Umoja wa Mataifa.

MAZINGIRA MAGUMU KWA WANAFUNZI SHULENI NANI ALAUMIWE


HAWA NI BAADHI YA WANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA  KATIKA SHULE YA
MSINGI MAKUMBUSHO YA JIJINI  DAR ES SALAAM WAKIWA DARASANI, SIJUI WAPO
WANGAPI, WATOTO HAWA HULAZIMIKA KILA MWEZI KULIPA Tsh1000 YA MTIHANI
WA MWEZI,Tsh 1500 YA MTIHANI WA TERM,Tsh500 YA KILA SIKU YA UJI HAPO
BADO TUISHENI,USAFI, MLINZI,LEBO,VIDUMU,FAGIO, NA MADAFTARI PIA
HULAZIMISHWA KUNUNUA HAPOHAPO.

WASANII WATAKIWA KUJIPANGA KUKABILI TEKNOLOJIA MPYA


Na Mwandishi Wetu
Wasanii nchini wameshauriwa kujipanga katika kutumia fursa na changamoto mbalimbali zitakazojitokeza wakati Ulimwengu ukijiandaa kuingia kwenye mfumo wa digital kutoka ule wa nalogia ifikapo mwaka 2014.
Ushauri huo umetolewa wiki hii na Msimazi wa Vipindi vya televisheni wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Mwanga Kirahi wakati akiwasilisha mada iliyohusu Teknolojia ya kisasa Katika Utengenezaji Filamu kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.
Alisema kuwa kuhama kutoka mfumo wa analogia kwenda digitali kutazalisha fursa mbalimbali za kuendeleza Sanaa nchini lakini pia ni mwanzo wa kuibuka kwa changamto nyingi ambazo kama wasanii hawatakuwa makini basi wanaweza kupotea na kushindwa kushindana ipasavyo.
  “Mfumo wa digitali utaleta ushindani katika kuandaa programu za televisheni, utazalisha fursa kwa kazi za wasaniii wetu kuonekana ulimwengu mzima lakini unaweza kuwa mwanzo wa kufa kwa ubunifu kama wasanii watategemea vifaa vya kisasa tu pasipo kuingiza ubunifu binafsi” alisisitiza.
Katika hili aliwashauri wasanii kutengeneza kazi zenye ubora na zisizo za kunakiri kutoka kwa wengine lakini pia zenye ubunifu binafsi pasipo kutegemea vifaa hivi vya kisasa pekee kwani kinyume chake ni kukataliwa kwa kazi zao na hatimaye kupwaya.
“Digital maana yake ni kazi za Wasanii wetu kuonekana Ulimwengu mzima, sasa kama zitakuwa za kunakiri kutoka kwa wengine na kutegemea vifaa hivi vya kisasa tu pasipo ubunifu binafsi hatutafanikiwa. Haya pekee yanazifanya kazi zetu zisivume muda mrefu kwani zinakuwa si original (halisi)i” alizidi kusisitiza.
Aliongeza kuwa, wasanii hawana budi kubadilika sasa na kuacha tabia ya wao kufanya kila kitu kikuanzia umeneja, utunzi, uongozaji (directing), uzalishaji (producing) na kadhalika kwani kwa kufanya hivyo kunazifanya kazi zao kuwa na radha moja pekee ambayo haiwezi kudumu muda mrefu.
Wadau wengi waliofika kupata elimu hiyo kupitia programu ya Jukwaa la Sanaa waliiomba Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) kupanga kukutana na wasanii ili kuwapa elimu juu ya mchakato wa kuhama kutoka mfumo wa analogia kwenda digitali.

Vodacom awards 10 Million to grand winner in M-Pesa promotion

Vodacom Tanzania Corporate Communications Manager, Rukia Mtingwa (left), M-PESA Expert Ms, Reenu Verma and the representative of the Gaming Board of Tanzania, Mr Abdallah Hemed follow proceedings during the draw to pick monthly winner of TShs 10 million of the M-PESA Transfer & Win promotion whereby a  Geita resident, Mr Denis Kaesha emerged the winner.
 Vodacom TZ has awarded over TShs 450 million in daily winnings to 9000 customers, and TShs 30 million in monthly prizes.
*       MPESA has endeared itself to customers, resulting into a substantial increase in the number of new adopters who have learnt not only of its reliability but also its ease of use.


Tanzania's leading mobile phone company, Vodacom has presented a cash prize of TShs 10 million to the winner of the ongoing MPESA promotion which targets users of the service during a brief ceremony at the company Headquarters at Mlimani City in Dar es Salaam.
Dennis Kaesha, an accountant from Geita was all smiles as he received news of winning the prize from Vodacom Corporate Communications Manager, Rukia Mtingwa, bringing to a close the M-Pesa Transfer and Win campaign which kicked off in March.
"I am very thrilled with this win. It's unbelievable," said a seemingly pleasantly surprised Dennis.
Dennis now joins Peter Kilalo, a traffic police officer from Dar and Revocatus Mkama, a car mechanic from Mwanza who emerged winners of the monthly grand draws in March and April, respectively.
In her remarks during the conversation with the winner, Rukia urged Vodacom customers to continue using the service, adding that the win was testament that the telecoms operators was increasingly reaching to its customers with innovative products that do not only make life pleasurable but also supports their day to day lives by addressing their unique needs.
The M-Pesa Transact and Win promotion allowed subscribers to win TShs 50,000 daily and a grand monthly prize of TShs 10 million every time they sent money.  To date, Vodacom has awarded over TShs 480 million in daily winnings to 9000 customers, and TShs 30 million in monthly prizes.
"I am pleased to tell you that you are the winner of the MPESA transact and win promotion during the month of May. We are very proud of you and will make every effort to present the money to you soon so that it can help make a difference in your life and your entire family," Rukia announced.
He said Vodacom was keen to use the MPESA platform which continues to experience exponential growth to power the lives of the Tanzanian people, irrespective of their economic standing.
The campaign is intended to not only excite users of the MPESA service and attract more but also to build the customers and general public's trust in its safety, reliability, speed and stability.
Increasingly, MPESA is becoming popular in Tanzania as more people prefer it for; payment of bills, money transfer both locally and across the borders and as a safe haven for money, especially for people on transit.
He said that while the campaign sought to increase the use of the service in the market, the company was also doing everything possible to ensure it remained strong, intact, safer, reliable and more importantly, affordable to all across the country.
The MPESA service was first introduced into the TZ market in April, 2008. Over the years, more service providers have included it in its financial management systems. These include; utility companies such as LUKU, DAWASCO, and DSTV. MPESA is also used to; pay for local flights on Precision Air, pay school fees as well as examination fees to NECTA, deposit and withdraw money through CRDB Bank, to name just a few.

NCHI MBALIMBALI ZAENDELEA KUTANGAZA WAWAKILISHI WAO MISS EAST AFRICA 2012

Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka Ethiopia
Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu wanaendelea kupatikana kutoka katika Nchi mbalimbali zinazoshiriki mashindano hayo.
Mrembo mwingine aliyeingia fainali ni Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka Nchini Ethiopia ambae alipatikana mwishoni mwa wiki baada ya kuwashinda warembo wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Ethiopia katika fainali hizo.
Miss Lula Teklehaimanot ana urefu wa 1.79m na uzito wa 52kg ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo cha St. Merry University cha jijini Addis Ababa, Ethiopia ampapo anasomea degree ya Marketing
Pia Mrembo huyo ni miongoni mwa wanamitindo maarufu  wanaochipukia kwa kasi Nchini Ethiopia.
Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.
Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam

Prostate Cancer Tanzania 50plus



No comments:

Post a Comment