Na Mwandi shi Maalumu, Panama 
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), 
Dkt. Edward Hoseah, amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la 
Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Duniani (IAACA). 
Dkt.
 Hoseah alichaguliwa na wajumbe 460 wa Mkutano Mkuu wa saba wa 
shirikisho hilo kutoka nchi mbalimbali uliofanyika Panama, Amerika ya 
Kati kuanzia Novemba 22-24, mwaka huu. 
 
Wajumbe
 wa mkutano huo ni pamoja na wakuu wa taasisi 98 za Kuzuia na Kupambana 
na Rushwa Duniani ambapo kaulimbiu ya mkutano huo inasema, "Utawala wa 
Sheria na Rushwa: Changamoto na Fursa Zilizopo". 
 
Kabla
 ya kuchaguliwa katika nafasi hiyo, Dkt. Hoseah alikuwa Mjumbe wa Kamati
 Kuu ya Utendaji katika shirikisho hilo ambapo kutokana na uteuzi huo, 
anakuwa Mwafrika wa kwanza kushika wadhifa huo mkubwa katika mapambano 
dhidi ya rushwa duniani. 
 
Uchaguzi
 huo ni heshima kubwa kwa Tanzania na Bara la Afrika pia ni fursa nzuri 
kwa Dkt. Hoseah kuonesha uwezo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya 
rushwa kimataifa. Nyadhifa nyingine za kimataifa ambazo Dkt. Hoseah 
amewahi kuzishikilia ni pamoja na Rais wa 
 
 Kwanza
 wa Shirikisho la Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Afrika 
Mashariki (2007-2008), Rais wa kwanza wa Jukwaa la Taasisi za Kuzuia na 
Kupambana na Rushwa katika nchi za SADC (SAFAC-2010-2011). 
 
Nyingine ni Mwenyekiti wa Bodi ya Umoja wa Afrika ya Ushauri wa Masuala ya Rushwa (AU-ABC 2011-2012). 
 
IAACA
 linajumuisha taasisi 298 pamoja na wanachama zaidi ya 2,000 kutoka 
katika asasi mbalimbali zisizo za kiserikali na lilianzishwa Aprili 19, 
2006, Makao Makuu yapo Peking, China. 
 
Lengo
 la kuanzishwa kwa shirikisho hilo ni kuziwezesha nchi wanachama 
kutekeleza Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Rushwa uliopitishwa na 
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Desemba 30, 2003.
No comments:
Post a Comment