BARUA ZATOLEWA RASMI,WAPEWA SIKU 14
BAADA YA MAJIBU,KUJIELEZA KAMATI KUU
LISSU ADAI UTETEZI WAO ULIPOTOSHA UKWELI
 Na Goodluck Hongo  
Aliyekuwa
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. 
Zitto Kabwe pamoja na wenzake, wameandaliwa mashtaka 11 kwa madai ya 
kuandaa mapinduzi ya siri dhidi ya uongozi wa chama hicho kinyume cha 
katiba. 
Bw.
 Kabwe na wenzake ambao ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Dkt. 
Kitila Mkumbo na Bw. Samson Mwigamba, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA 
jijini Arusha, jana walikabidhiwa barua rasmi ili wajieleze ndani ya 
siku 14. 
Mkurugenzi
 wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, Bw. John Mnyika, aliyasema hayo Dar es 
Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya 
chama hicho. 
Bw.
 Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam, alisema 
chama hicho kimeandaa mashtaka hayo baada ya Sekretarieti ya CHADEMA 
kupitia maamuzi ya Kamati Kuu yaliyowavua nyadhifa za uongozi watuhumiwa
 hao. 
 "Watuhumiwa
 hawa watatakiwa kujieleza kwa maandishi ndani ya siku 14, baadaye 
watajieleza mbele ya Kamati Kuu ambayo itatoa maamuzi ya hatua za 
kuchukua," alisema Bw. Mnyika. 
Alisema
 mashtaka hayo yametokana na waraka wa siri ambao ulikamatwa na kutolewa
 mbele ya Kamati Kuu unaowakashifu viongozi wakuu wa chama hicho. 
"Wote
 watatakiwa kujieleza kwa nini wasifukuzwe ndani ya chama chetu kwa 
makosa waliyofanya... Kamati Kuu ya chama ndicho chombo chenye maamuzi 
ya kuwaondoa viongozi au wanachama wanaokiuka Katiba. 
"Waraka
 uliochapishwa katika baadhi ya vyombo vya habari (si Majira) na 
mitandao ya kijamii unaodaiwa kuwaponza Bw. Kabwe na wenzake si wenyewe 
ni batili," alisema. 
Aliongeza
 kuwa, maamuzi yaliyofanywa na Kamati Kuu yalizingatia kanuni, sheria na
 taratibu za chama kwa kufuata katiba, hivyo Bw. Kabwe na wenzake 
hawakufukuzwa kwa sababu walizozitoa kwenye vyombo vya habari bali kwa 
kuandika waraka wa kimapinduzi. 
Msimamo wa CHADEMA 
Bw.
 Mnyika alisema, chama hicho hakipo tayari kuwavumilia viongozi na 
wanachama wote ambao watakuwa kikwazo kwa chama hicho kufikia malengo 
yake bila kujali cheo alichonacho. 
"Wanatafuta
 huruma kwa wananchi kutokana na makosa ambayo wameyafanya hasa la 
kuandaa waraka wa siri, wao wenyewe walikiri kuhusika nao lakini 
wanapotosha ukweli," alisema. 
Alisema
 Sekretarieti hiyo imepokea na kutoa mapendekezo mbalimbali ya 
utekelezaji wa mikakati waliyojipangia ambayo ni Vuguvugu la Mabadiliko 
(M4C) na "CHADEMA ni msingi". 
Akizungumzia
 uchomaji wa bendera za chama, ofisi, fulana na kuondoa mabango ya 
CHADEMA, baada ya Bw. Kabwe na wenzake kuvuliwa nyadhifa za uongozi, Bw.
 Mnyika alisema chama kimezisikia taarifa hizo. 
"Uchunguzi
 wa awali unaonesha kilichotokea ni kiini macho tu si wanachama wa chama
 chetu waliofanya hivyo, viongozi wa maeneo husika wanaendelea na vikao,
 usalama upo," alisema. 
Tundu Lissu azungumza 
Kwa
 upande wake, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Bw. Tundu Lissu, alisema 
watuhumiwa walifanya mkutano na vyombo vya habari kwa lengo la kupotosha
 ukweli wa mambo juu ya mazingira halisi ya kuvuliwa nyadhifa zao. 
"Hawakuondolewa
 katika nyadhifa zao kwa sababu ya kuuza majimbo yetu ya uchaguzi mwaka 
2010, si posho, wala uwepo wake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya 
Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), aliyeibua hoja ya kukaguliwa kwa 
hesabu za vyama vya siasa. 
"Amevuliwa nyadhifa hizo na wenzake kwa sababu ya kuandaa mapinduzi ndani ya chama kwa kukiuka maadili," alisema. 
Akizungumzia
 madai ya kugawanyika au kupasuka kwa chama hicho kama Bw. Kabwe 
atafukuzwa uanacham, Bw. Lissu alisema kwa nyaraka alizoziona, Kabwe 
alikuwepo katika kikao cha Kamati Kuu kilichomfukuza aliyekuwa Katibu 
Mkuu wa chama hicho mwaka 2004, Dkt. Amaan Kabourou. 
"Ka
 bwe p i a a l i k uwe p o kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichomfukuza 
aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hiki, marehemu Chacha Wangwe mwaka 
2007; hivyo hata kikao kama hicho ndicho kilichowavua vyeo yeye na 
wenzie hivyo Kamati Kuu isilaumiwe," alisema. 
Bw.
 Lissu alisema, madai ya Bw. Kabwe kudai alijitoa katika utiaji saini 
katika masuala ya fedha ndani ya chama hicho kwanza hakuwahi kuwa mtiaji
 saini ili kuidhinisha fedha, hivyo anashangaa kulizungumzia hilo wakati
 hakuwahi kuwa mtiaji saini. 
"Chama
 kimepasuka mara nyingi tangu enzi ya Bw. Kabwe kuingia kwenye Kamati ya
 Jaji Bomani, Chacha Wangwe, ugaidi wa Rwakatare hata sakata la mabomu 
lakini tuliibuka upya, hadi sasa chama kinaendelea na mapambano yake," 
alisema. 
Alipoulizwa
 na waandishi kama viongozi hao wakiamua kuondoka, chama kimejipangaje, 
alisema si vizuri kuwahukumu Bw. Kabwe na wenzake kwa sababu bado 
hawajaanza kujitetea, lakini kugombea uongozi ndani ya chama si uhaini 
wala dhambi. 
Alibainisha
 kuwa, sh. milioni 100 zilizotolewa na mfanyabiashara maarufu nchini, 
Bw. Mustafa Sabodo, hesabu za matumizi yake zipo wazi na zilipelekwa 
kwenye hesabu za chama hicho ili zikaguliwe na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu 
wa Hesabu za Serikali (CAG). 
Aliongeza
 kuwa, licha ya vyama vya siasa kuwa tayari kukaguliwa, CAG alishindwa 
kukagua hesabu hizo kwa sababu ya ukosefu wa fedha, hivyo alivitaka 
vyama husika kuwalipa wakaguzi ambao wangefanya ukaguzi huo jambo ambalo
 walilipinga. 
"Tuna
 ushahidi wote kuhusu suala hili, hata Msajili mpya wa Vyama vya Siasa, 
aliandika barua kwa CAG kuhusu kupinga vyama kuwalipa wakaguzi wa hesabu
  kwani huo si utarabu wa Serikali, lakini tunamshangaa Kabwe kuzungumzia suala hili wakati analijua vizuri," alisema Bw. Lissu
No comments:
Post a Comment