TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 30, 2013

JE KUPOROMOKA KWA MAJENGO NINI TAFAKARI YA TAIFA?


…………………………………………………………………..
Dar es Salaam. Utafiti uliofanywa hivi karibuni na Taasisi ya Twaweza unaonyesha kuwa licha ya kuwapo sababu nyingine zinazochangia kutokea kwa ajali za kuporomoka kwa majengo, rushwa inaonekana kuwa chanzo kikuu cha kukithiri kwa hali hiyo.
Ripoti ya utafiti huo inaeleza kuwa rushwa imekuwa ikichangia kwa kiasi kikuba majengo mengi kujengwa chini ya kiwango, hali inayochangia kutokea kwa majanga mbalimbali yanayogharimu maisha ya Watanzania.
Utafiti huo umekuja kufuatia tukio la Machi 29 mwaka huu ambapo jengo la ghorofa 36 katika Mtaa wa Indira gandhi liliporomoka na kusababisha vifo na wengine  kadhaa kujeruhiwa.
Akiwasilisha ripoti hiyo, mmoja wa watafiti kutoka katika mradi wa Sikiliza, Dk Thomas Maqway alisema licha ya serikali kusisitiza kuchukua hatua mbalimbali lakini utafiti huo unaonyesha  kuwa wananchi hawana imani na mfumo wa  kisheria katika kuwawajibisha na kuwaadhibu wanaohusika kusababisha ajali zinazotokana na majengo kuporomoka.
Alisema hali hiyo inatokana na mfumo wa rushwa unaonekana kutawala katika ujengaji wa majengo kuanzia ukandarasi, usanifu, vifaa, ujenzi  hadi kwenye ukaguzi wa majengo katika jiji ji la Dar es Salaam.
“Asilimia 78 ya wahojiwa walioshiriki katika utafiti huu wanataja  rushwa ndiyo sababu ya kuendelea kutokea kwa hali hii, hivyo hata uwajibishwaji wa wahusika hawana imani.

No comments:

Post a Comment