Na Mwandishi Maalum
 Waziri
 Mkuu, Mizengo Pinda, amewataka maofisa mipango miji nchini kurekebisha 
utendaji wao wa kazi ili waweze kubadili taswira mbaya iliyojengeka 
miongoni mwa jamii dhidi yao.
Alitoa
 kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Wataalam wa 
Mipango miji waliosajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango 
miji ulioanza jana jijini Dar   es Salaam.
“Taswira
 ya utendaji kazi katika taaluma ya mipango miji na katika sekta ya 
ardhi kwa ujumla miongoni mwa wananchi na Serikali sio nzuri sana. 
 Watafiti wanatueleza kuwa kati ya asilimia 60 na 80 ya makazi kwenye miji yetu hapa nchini yamejengwa kiholela. 
Na kwa kiwango hicho hicho wakazi wa mijini wako kwenye makazi hayo na wanaishi kiholela,î alisema. 
“Wako
 wanaosema ninyi ndiyo chanzo cha hiyo migogoro, wako wanaosema ninyi 
kwa rushwa ndiyo wenyewe, mimi sishangai madai haya ila ninawasihi muwe 
na roho ngumu katika kushinda vishawishi hivi,” alisisitiza. 
Aliwataka
 wajadili masuala yanayohusu migogoro ya ardhi baina ya wafugaji na 
wakulima, baina ya mipaka ya vijiji, baina ya wilaya, baina ya 
wanavijiji na hifadhi za Taifa au maeneo ya uchimbaji madini na kujadili
 njia za kutatua migogoro hiyo ili kuwa na mipamgo endelevu. 
Aliwataka
 waangalie suala la ukuaji wa miji iliyokaribu na Jiji la Dar es Salaam 
kwa kuangalia dhana ya miji mikubwa kubeba vijiji vinavyoizunguka na 
hasa kuangalia uwezekano wa kupunguza mrundikano wa watu katika jiji 
hilo. 
“Miji
 ya Kibaha, Mkuranga na Bagamoyo inatumikaje kusaidia kupunguza 
msongamano katika jiji la Dar   es Salaam,” Waziri Mkuu alihoji. 
Alisema
 wataalamu wa mipango miji wanapaswa kuwa na maono makubwa ya baadaye 
kama kweli wanataka kupunguza majanga katika siku za usoni. 
“Angalieni
 utafiti wa gesi unaoendelea pale Mtwara na mjipange, angalieni mpango 
wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na kuunganisha na reli ya kati, 
angalieni Lindi na upatikanaji wa Liquified Naturala Gas (LNG), pangeni 
miji kwa siku za baadaye siyo sasa,” alisisitiza. 
Aliwataka
 wanataaluma hao wasimamie vyema taaluma yao kwani katika miaka 37 
ijayo, (mwaka 2050) inakadiriwa kwamba nusu ya watu wote watakuwa 
wakiishi mijini. “ Kuweni wakweli, tumieni weledi wenu la sivyo katika 
miaka 37 ijayo kama wanavyosema watafiti, itakuwa balaa tupu,î alisema.
Mapema
 akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wataalamu hao kutoka mikoa yote
 hapa nchini, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna 
Tibaijuka, alisema maofisa mipango miji wanakabiliwa na changamoto ya 
kufikiri na kubuni aina ya miji ambayo itakidhi mahitaji ya jamii ya 
baadaye. 
Alisema
 hata hivyo maofisa hao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kushindwa
 kutoa maamuzi au ushauri wa kitaalamu kwa kuhofia kuadhibiwa na 
madiwani. 
Wizara
 ya Fedha. " Kwa nafasi yake ndiye alikuwa akishiriki kuandaa bajeti ya 
upinzani bungeni, kuwasilisha bajeti ya wizara ya fedha akiwa waziri 
kivuli, lakini kwa kuvuliwa wadhifa wake maana yake haaminiki tena," 
alisema mmoja wa watoa habari ndani ya chama hicho kwa sharti la jina 
lake kutochapishwa gazetini.
Hata
 hivyo, juhudi za kumpata Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, 
John Mnyika, ili kuweza kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba kutokana
 na simu yake ya kiganjani kutopokelewa. 
Wakati
 huo huo, Jeshi la Polisi Makao Makuu jijini Dar es Salaam leo 
linatarajia kufanya mahojiano na Katibu wa CHADEMA mkoa wa Dar es 
Salaam, Henry Kileo, baada ya mahojiano hayo kukwama kufanyika jana 
kutokana na malalamiko yanayodaiwa kuwasilishwa na Mbunge wa Kigoma 
Kaskazini, Zitto Kabwe. 
Mahojiano
 hayo yalikuwa yafanyike Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es 
Salaam jana mchana, lakini yaliahirishwa muda mfupi baada ya Kileo 
kuwasili akiwa na mwanasheria wake na makada wengine wa CHADEMA. 
Baada
 ya kufika maofisa wa Polisi walifanya mazungumzo na mwanasheria wake, 
lakini baada ya muda walikubaliana yafanyike leo saa tano.
Akizungumza
 na gazeti hili jana, Kileo, alisema awali mahojiano yalitakiwa 
yafanyike jana saa nane mchana, lakini walichelewa kufika makao makuu ya
 polisi kutokana na wakili wake kuchelewa kwani alikuwa na kesi makao 
makuu ya Polisi. 
Kileo,
 alipoulizwa anatakiwa polisi kwa ajili ya makosa gani, alisema hana 
taarifa kwa undani, kwani alipigiwa simu na ofisa aliyejitambulisha kwa 
jina la Mbutta na kumwambia kuwa anatakiwa kufika makao makuu ya Polisi 
kwa mahojiano kutokana na malalamiko ambayo Zitto, ameyafikisha. 
"Niliambiwa
 nahitajika kujibu tuhuma ambazo Zitto amezifikisha Polisi, lakini 
sikuelezwa ni tuhuma gani hizo," alisema Kileo. Alipoulizwa ni kwa nini 
Zitto apeleke shtaka hilo Makao Makuu ya Polisi, badala ya vituo vingine
 kama ilivyo kawaida, Kilewo alijibu; "Mimi sijui labda wapigie polisi 
ili muwaulize swali hilo." 
Gazeti
 moja (sio Majira) jana lilichapisha habari inayoeleza kuwa Zitto, 
amemfungulia mashtaka Kileo akimtuhumu kusambaza waraka katika mitandao 
ya kijamii unaomhusisha na mipango ya kufanya mapinduzi ya chama hicho. 
No comments:
Post a Comment