Na Mwandishi Wetu 
  Rais
 Jakaya Kikwete, amemtumia salamu za rambirambi Makamu Mwenyekiti wa 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula, kufuatia kifo cha mtoto wake,
 Peter Philip Mangula, kilichotokea juzi katika Hospitali ya Taifa ya 
Muhimbili (MNH) alikokuwa amepelekwa kwa matibabu akisumbuliwa na 
ugonjwa wa shinikizo la damu.
"Nimeshtushwa,
 nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha 
mwanao (Peter Philip Mangula)," alisema kwa masikitiko Rais Kikwete 
katika salamu zake.
Rais
 Kikwete aliongeza kusema kuwa; nasikitishwa zaidi na taarifa za kifo 
hiki kwa kuzingatia kwamba ni katika kipindi kifupi kilichopita, Mangula
 alimpoteza binti yake, Neema Nemela Mangula aliyefariki dunia kutokana 
na ajali ya gari, hivyo ni dhahiri kwamba kifo cha kijana wake huyu 
kimeongeza machungu na simanzi kwa familia ya Mangula na kimesababisha 
pengo kubwa kwa wanafamilia kwa ujumla. 
"Kutokana
 na taarifa hizo za kusikitisha, ninakutumia wewe salamu zangu za 
rambirambi na pole nyingi kwako wewe binafsi na kwa familia yako yote 
kwa ujumla kwa kupotelewa na mtoto wako." 
Alisema
 anamuomba Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mjalie yeye na familia yake 
moyo wa uvumilivu na ujasiri ili kuhimili machungu ya kuondokewa na 
kijana wao.  
No comments:
Post a Comment