Siku moja baada ya gazeti hili kuripoti habari za watoto wanadaiwa 
kutekwa na kufichwa katika handaki lililopo kwenye msitu wa Mabwepande, 
Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, ambalo ndani yake kuna jengo kubwa 
lenye vyumba, Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi mkali, anaripoti Masau Bwire.
 
Chanzo
 chetu cha habari kimedokeza kuwa, uchunguzi huo unafanywa na Jeshi la 
Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi 
mkoani Pwani. 
"Polisi
 wapo katika uchunguzi mkali tangu leo (jana), asubuhi, si vyema kuzitoa
 taarifa mapema kabla uchunguzi haujakamilika, tunaweza kuharibu 
upelelezi na wahusika kukimbia. 
"
 Watoto wal i o j i o k o a w a m e p e l e k w a h o s p i t a l i 
kuchunguzwa afya zao baada ya kuhojiwa na kutoa picha kamili ya eneo 
lenye handaki, hivyo uchunguzi ukikamilika mtaambiwa," kilisema chanzo 
hicho kwa sharti la kutotajwa jina lake. 
Utekaji
 watoto wanaodaiwa kuwa zaidi ya 60 katika handaki hilo, unadaiwa 
kufanywa na raia wa kigeni (Wazungu), wakishirikiana na Watanzania 
ambapo watoto hao hufungiwa katika vyumba hivyo, kuteswa, kulawitiwa na 
kubakwa. 
Watoto
 waliodai kutoroka kwenye handaki hilo ni Emmanuel Robert (11) anayesoma
 darasa la tano Shule ya Msingi Maendeleo iliyopo Tabata, Segerea, Dar 
es Salaam na mdogo wake Godianus Robert (8), anayesoma darasa la tatu 
shuleni hapo. 
Watoto
 hao walidai kutekwa na Wazungu wawili asubuhi ya Septemba 2 mwaka huu, 
wakati wakienda shuleni na kufanikiwa kutoroka katika jengo hilo 
Septemba 23 mwaka huu.  
Wakiwa
 wamechoka na afya zao kuzorota katika Kituo kidogo cha Polisi, Kibaha 
Maili Moja, mkoani Pwani, watoto hao walisema ndani ya jengo hilo kuna 
watoto wengi wa kike na kiume. 
Wa
 l i s e m a w a t o t o h a o wanafanyishwa kazi na kuteswa kwa 
kutandikwa fimbo, kuchomwa moto na kupigwa shoti ya umeme hasa 
wanapowaulizia wazazi wao ambapo baadhi yao hubakwa na kulawitiwa. 
Akizungumza na Majira,
 Emmanuel alisema baada ya kutekwa yeye na mdogo wake, walifungwa na 
vitambaa vyeusi usoni hadi walipofikishwa ndani ya jumba hilo la mateso.
 
 
Aliiomba Serikali kufanya jitihada za hali na mali ili kuwaokoa watoto wengine waliopo katika jengo hilo. 
Mama
 mzazi wa watoto hao, Martha Godianus (29), ambaye anafanya shughuli za 
mama lishe, njia panda ya Barakuda, Tabata Manispaa ya Ilala, alisema 
amehangaika zaidi ya miezi mitatu kuwatafuta watoto hao bila mafanikio. 
Juzi Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei alikiri kupata taarifa
 za tukio hilo na kuanza kuzifanyia kazi
No comments:
Post a Comment