TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, November 28, 2013

KILI STARS , CHIPOLOPOLO HAKUNA MBABE


 Na Mwandishi Wetu, Nairobi
  Timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro jana imeshuka uwanjani kumenyana na Zambia, katika mechi ya ufunguzi ya michuano ya Kombe la Chalenji.

Kilimanjaro Stars na Zambia zimechuana kuwania pointi tatu katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Machakos ulioko nje kidogo ya jiji la Nairobi. 
 
Timu hiyo ya Tanzania Bara iliyopangwa Kundi B, ilihitaji ushindi ili kupata pointi tatu ambazo zingeiweka katika nafasi nzuri kwenye michuano hiyo. 
 
Akizungumzia mchezo huo wa jana, Kocha Mkuu wa Kili Stars, Kim Poulsen alisema timu yake imeshindwa kupata ushindi kutokana na wachezaji wengi kuwa wachovu wa safari, 
 
Alisema kikosi chake kimefanya mazoezi  magumu, amb a y o bado wachezaji wanauguza viungo vyao,  hata hivyo kulikuwa na upinzani mkubwa dhidi ya Zambia inayosifika kwa kutandaza soka ya kiwango bora Afrika. 
 
Kilimanjaro Stars iliwategemea zaidi wachezaji kama Mrisho Ngasa, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Said Morad, Athuman Idd na Salum Abubakar. 
 
Pia, wamo Frank Domayo, Himid Mao, Haruna Chanongo, Ramadhan Singano ‘Messi’, Farid Mussa na Elias Maguli.
Katika mechi ya ufunguzi iliyochezwa juzi mchana timu ya taifa ya Zanzibar iliifunga Sudan Kusini mabao 2-1 katika mchezo mkali uliokuwa na ushindani.

No comments:

Post a Comment