Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Tamisemi), Hawa Ghasia ameingia matatani
 baada ya Chama cha Walimu Wilaya za Mbozi na Momba mkoani Mbeya 
kumchongea jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
CWT kilidai Ghasia alikataa 
kusomewa risala ya walimu wenye kero akidai anazijua, hivyo hana haja ya
 kusikiliza. Kutokana na kauli hiyo, Kinana aliomba asomewe taarifa 
hiyo.
Msoma taarifa,Leonard Nyamiye 
alisema walimu wanaidai Serikali zaidi ya Sh1 bilioni za mishahara 
,uhamisho na mengine mengi. Mwalimu huyo alisema kutolipwa madeni hayo 
kumewafanya waichukie sana CCM na Serikali.
Akizungumza Kinana alisema suala
 la Ghasia atalifikisha kwa mwajiri wake. Kinana ambaye katika ziara 
yake amekuwa akikutana na viongozi wa CWT kila wilaya, alikiri kusikia 
kero za walimu siku nyingi. ”Nakumbuka mwaka 2010 Rais Kikwete alikaa na
 CWT Taifa kwa saa tisa ili kumaliza tatizo, lakini kila baada ya mwaka 
linajitokeza”, alisema.
Kinana alisema sasa CCM 
italivalia njuga na kwamba itajadili chanzo cha tatizo katika kikao cha 
NEC ijayo. Hata hivyo alidokeza kuwa amegundua kwamba walimu hawana 
mwajiri mmoja na ndiyo maana wanasumbuliwa.
Alisema
 walimu kwa sasa wanashughulikiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya 
Ufundi, Tamisemi, Tume ya Ajira na Hazina jambo ambalo ni kero.

No comments:
Post a Comment