TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 30, 2013

WAZIRI GHASIA ACHONGEWA NA CWT JIJINI MBEYA.


1 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Tamisemi), Hawa Ghasia ameingia matatani baada ya Chama cha Walimu Wilaya za Mbozi na Momba mkoani Mbeya kumchongea jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
CWT kilidai Ghasia alikataa kusomewa risala ya walimu wenye kero akidai anazijua, hivyo hana haja ya kusikiliza. Kutokana na kauli hiyo, Kinana aliomba asomewe taarifa hiyo.
Msoma taarifa,Leonard Nyamiye alisema walimu wanaidai Serikali zaidi ya Sh1 bilioni za mishahara ,uhamisho na mengine mengi. Mwalimu huyo alisema kutolipwa madeni hayo kumewafanya waichukie sana CCM na Serikali.
Akizungumza Kinana alisema suala la Ghasia atalifikisha kwa mwajiri wake. Kinana ambaye katika ziara yake amekuwa akikutana na viongozi wa CWT kila wilaya, alikiri kusikia kero za walimu siku nyingi. ”Nakumbuka mwaka 2010 Rais Kikwete alikaa na CWT Taifa kwa saa tisa ili kumaliza tatizo, lakini kila baada ya mwaka linajitokeza”, alisema.
Kinana alisema sasa CCM italivalia njuga na kwamba itajadili chanzo cha tatizo katika kikao cha NEC ijayo. Hata hivyo alidokeza kuwa amegundua kwamba walimu hawana mwajiri mmoja na ndiyo maana wanasumbuliwa.
Alisema walimu kwa sasa wanashughulikiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Tamisemi, Tume ya Ajira na Hazina jambo ambalo ni kero.

No comments:

Post a Comment