Na Suleiman Abeid, Shinyanga 
Wanachama
 wa vikundi vya wajasiriamali wadogo katika kata ya Kitangili Manispaa 
ya Shinyanga wametakiwa kuepuka kuingiza siasa katika vikundi vinginevyo
 vitasambaratika
Tahadhari
 hiyo ilitolewa juzi na diwani wa viti maalumu (CCM) manispaa ya 
Shinyanga, Mariamu Nyangaka, alipokuwa akizungumza na viongozi wa vikund
 imbalimbali vya wajasiriamali waliokutana kwa ajili ya kuanzisha Chama 
cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS ). 
Nyangaka
 alisema viongozi wa vikundi vya wajasiriamali pamoja na wanachama wao 
kwa ujumla wanatakiwa kuhakikisha wanaendesha shughuli zao bila kuingiza
 au kutanguliza itikadi ya vyama vya siasa katika vikundi vyao kitu 
ambacho kinaweza kusababisha mgawanyiko miongoni mwao. 
Alisema
 wapo baadhi ya wanasiasa wanaotumia wajasiriamali wadogo kufikia 
malengo yao waliyojipangia huku wengine wakidiriki hata kuwazuia wafuasi
 wa vyama vyao wasishirikiane na watu ambao si wafuasi wa vyama vyao vya
 siasa hata kama shughuli zao zinapaswa kuendeshwa kwa ushirikiano wa 
pamoja. 
"Ndugu
 zangu mkakati ambao mnataka kuuanzisha ni mkakati mzuri utawasaidia 
kuendesha shughuli zenu kwa ufanisi mkubwa, mtakapokuwa na SACCOS yenu 
itawasaidia kuweza kupata mitaji ya kuendesha biashara zenu kupitia 
mikopo mtakayokopa yenye masharti nafuu tofauti na inayotolewa na benki 
zetu nyingi nchini,"alisema. 
"Lakini
 naomba mjihadhari na siasa katika vikundi vyenu, mkimruhusu mdudu huyu 
kuwa miongoni mwenu eleweni wazi hamtadumu kwa kipindi kirefu, 
hakikisheni mnaendesha shughuli zenu bila kuchanganya na itikadi za 
kisiasa na wakemeeni wale wote watakaoonesha dalili za kuingiza siasa 
ndani ya vikundi," alisema Nyangaka. 
Kwa
 upande wake ofisa ushirika kutoka manispaa ya Shinyanga, Athumani, 
alisema serikali kwa kipindi kirefu imekuwa ikihimiza umuhimu wa 
wananchi kujiundia vyama vyao vya ushirika wa akiba na mikopo (SACCOS) 
kwa vile ni rahisi zaidi kusaidiwa na asasi mbalimbali za kifedha. 
Alisema kupitia SACCOS watu wengi wamefanikiwa katika biashara zao na 
baadhi wameweza kujenga nyumba za makazi huku wengine wakisomesha watoto
 wao bila matatizo. Alisema jambo la msingi ni uaminifu wa viongozi wa 
SACCOS zinazoanzishwa kwa kuhakikisha zinakuwa na wanachama waadilifu na
 wenye kuzingatia sheria za uendeshaji wa ushirika huo. 
Katika
 hatua nyingine, viongozi hao wa vikundi vya wajasiriamali wadogo 
wameunda uongozi wa muda utakaosimamia taratibu za uanzishwaji wa 
ushirika wa akiba na mikopo. 
Alisema
 utaundwa na vikundi vyote vilivyopo katika kata ya Kitangili na 
kuhakikisha SACCOS hiyo inasajiliwa kisheria ili iweze kuanza kazi mara 
moja. 
Viongozi
 wa muda waliochaguliwa Elias Joseph (Mwenyekiti), Richard Maige 
(mwenyekiti msaidizi), Patrick Kileo (katibu), Masunga Elias (katibu 
msaidizi) ambapo Timothy Kakiri, alichaguliwa kuwa mweka hazina.
No comments:
Post a Comment