TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 30, 2013

ULIMWENGU,SAMATTA-KATIKA KIBARUA KOMBE LA SHIRIKISHO, MASWALI NI KAMA WATAWEZA KUVAA KIATU CHA DHAHABU.


FAINALI ya pili ya kombe la shirikisho itapigwa leo katika dimba la Mazembe mjini Lubumbashi baina ya wenyeji TP Mazembe dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia.
Katika mchezo wa leo washambuliaji wawili raia wa Tanzania Mbwana Ally Samatta na Thomas Ulimwengu watakuwa wakiiongoza timu yao kutafuta ushindi muhimu na wakihistoria kwao.
Samatta anatarajiwa kuonesha makali yake zaidi huku ikizingatiwa kuwa ni miongoni mwa wachezaji wanaowania tuzo ya CAF ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza klabu za ndani.
Kama mshambuliaji huyo atafunga leo na kuonesha kiwango cha juu, itamsaidia kujiweka mazingira mazuri zaidi ya kubeba tuzo hiyo inayotolewa na shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
samataMazembe wanahitaji kushinda mabao 3-0 wakiwa katika dimba lao, kwani fainali ya kwanza walifungwa mabao 2-0 na Watunisia hao dimba la Olympique de Rades mjini Tunis.

Mabao hayo yaliyoipa karaha Mazembe na mashabiki wake, yalifungwa na washambuliaji wawili raia wa Gabon, Ibrahim Didier Ndong aliyefunga bao la kwanza dakika ya 16 na mshambuliaji Taha Yassine Khenissi aliyefunga la pili dakika ya 90.
Siku hiyo Samatta na Ulimwengu wote walianza kikosi cha kwanza pamoja na mkali Tressor Mputu Mabi, lakini bado mambo yalikuwa magumu zaidi kwani Watunisia walionekana kuwa bora zaidi yao na kuweza kutumia nafasi walizopata.
image1 
Thomas Ulimwengu naye mzigoni kama kawaida leo
Bingwa wa Kombe hilo atazawadiwa kitita cha dola za Kimarekani, 625 000, wakati mshindi wa pili atapata dola 432 000.
Mshindi pia atamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri kuwania taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014.
Wachezaji waliokuwa wakiunda kikosi cha Simba SC mwaka 1993 walivalishwa Medali za Fedha na Rais mstafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada ya kufungwa mabao 2-0 na Stellah Abidjan ya Ivory Coast mwaka 1993 katika fainali ya pili ya Kombe la CAF Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Awali, Simba ilitoa sare ugenini na kuwapa matumaini Watanzania kwamba taji la kwanza kubwa Afrika lingetua nchini mwaka 1993. 
Baada ya mchezo wa leo wa fainali, kesho, Samatta na Ulimwengu watakwea pipa kuelekea jijini Nairobi Kenya kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania bara, Kilimanjaro Stars kinachojiandaa na mchezo wa pili wa kombe la CECAFA dhidi ya Somalia desemba 2 mwaka huu.
Mchezo wa kwanza, Kili Stars walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya waliowahi kuwa mabingwa wa soka barani Afrika, timu ya Taifa ya Zambia maarufu kwa jina la Chipolopolo.

No comments:

Post a Comment