FAINALI
 ya pili ya kombe la shirikisho itapigwa leo katika dimba la Mazembe 
mjini Lubumbashi baina ya wenyeji TP Mazembe dhidi ya CS Sfaxien ya 
Tunisia.
Katika
 mchezo wa leo washambuliaji wawili raia wa Tanzania Mbwana Ally Samatta
 na Thomas Ulimwengu watakuwa wakiiongoza timu yao kutafuta ushindi 
muhimu na wakihistoria kwao.
Samatta
 anatarajiwa kuonesha makali yake zaidi huku ikizingatiwa kuwa ni 
miongoni mwa wachezaji wanaowania tuzo ya CAF ya mchezaji bora wa Afrika
 kwa wachezaji wanaocheza klabu za ndani.
Kama
 mshambuliaji huyo atafunga leo na kuonesha kiwango cha juu, itamsaidia 
kujiweka mazingira mazuri zaidi ya kubeba tuzo hiyo inayotolewa na 
shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
Mazembe
 wanahitaji kushinda mabao 3-0 wakiwa katika dimba lao, kwani fainali ya
 kwanza walifungwa mabao 2-0 na Watunisia hao dimba la Olympique de 
Rades mjini Tunis. 
Mabao hayo 
yaliyoipa karaha Mazembe na mashabiki wake, yalifungwa na washambuliaji 
wawili raia wa Gabon, Ibrahim Didier Ndong aliyefunga bao la kwanza 
dakika ya 16 na mshambuliaji Taha Yassine Khenissi aliyefunga la pili 
dakika ya 90.
Siku hiyo 
Samatta na Ulimwengu wote walianza kikosi cha kwanza pamoja na mkali 
Tressor Mputu Mabi, lakini bado mambo yalikuwa magumu zaidi kwani 
Watunisia walionekana kuwa bora zaidi yao na kuweza kutumia nafasi 
walizopata.
Thomas Ulimwengu naye mzigoni kama kawaida leo
Bingwa wa Kombe hilo atazawadiwa kitita cha dola za Kimarekani, 625 000, wakati mshindi wa pili atapata dola 432 000. 
Mshindi
 pia atamenyana na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ya Misri 
kuwania taji la Super Cup mechi itakayopigwa nchini Misri Februari 2014.
Wachezaji
 waliokuwa wakiunda kikosi cha Simba SC mwaka 1993 walivalishwa Medali 
za Fedha na Rais mstafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada 
ya kufungwa mabao 2-0 na Stellah Abidjan ya Ivory Coast mwaka 1993 
katika fainali ya pili ya Kombe la CAF Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Awali, Simba ilitoa sare ugenini na kuwapa matumaini Watanzania kwamba taji la kwanza kubwa Afrika lingetua nchini mwaka 1993. 
Baada
 ya mchezo wa leo wa fainali, kesho, Samatta na Ulimwengu watakwea pipa 
kuelekea jijini Nairobi Kenya kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya 
Tanzania bara, Kilimanjaro Stars kinachojiandaa na mchezo wa pili wa 
kombe la CECAFA dhidi ya Somalia desemba 2 mwaka huu.
Mchezo
 wa kwanza, Kili Stars walitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya waliowahi kuwa 
mabingwa wa soka barani Afrika, timu ya Taifa ya Zambia maarufu kwa jina
 la Chipolopolo.

No comments:
Post a Comment