Na Rose Itono 
 
 
 Mhariri na Msanifu Mkuu Msaidizi wa gazeti la Uhuru, Dunia Mzobora, 
amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya Taifa ya 
Muhimbili (MNH) kutokana na ugonjwa wa shinikizo la damu. 
Akizungumza kwa
 njia ya simu jana, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Uhuru, Josia Mufungo, 
alisema marehemu kabla ya mauti yake alikuwa kazini kama kawaida ambapo 
saa mbili usiku alimaliza kazi zake na kurejea nyumbani. 
 
Alisema
 usiku wa saa sita walipata taarifa kutoka kwa familia yake kuwa Dunia 
amezidiwa na kukimbizwa haraka hospitali kwa ajili ya matibabu. 
 
"Marehemu
 alikimbizwa Hospitali ya Agha Khan lakini walishindwa na kuamua 
kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi na saa 12 za asubuhi alifariki", 
alisema. 
 
Mufungo
 alisema marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu 
kwa muda mrefu na kuongeza kuwa msiba wake utafanyika nyumbani kwake 
Tabata Kimanga, ambapo anatarajiwa kuzikwa leo saa 7.00 za mchana na 
shughuli zote za mazishi zitakuwa hapo hapo nyumbani kwake. 
 
Alisema
 marehemu ameacha mjane na watoto watano. Alijiunga na gazeti la Uhuru 
mwaka 1989 kama mwandishi mwanafunzi ambapo baadaye alipanda hadi 
kufikia nafasi aliyokuwepo
No comments:
Post a Comment