TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 18, 2014

HIV YAMKIMBIZA KIJIJINI- WANANCHI WAMLAZIMISHA KUHAMA NYUMBANI KWAO

Kirusi kinacho waogofya wa China
Hatma ya mvulana mwenye asili ya China anayeishi na virusi vya ugonjwa wa ukimwi ,imetaarifiwa amelazimika kuhama nyumbani kwao baada ya wanakijiji wapatao 200 .
Kisa chake kinatanabahisha kiwango cha unyanyapaa kwa wanaoishi na virusi vya ukimwi nchini China,pindi wanapotambulika basi hukumbana na unyanyapaa.

Mlezi wa motto huyo ambaye ni babu yake,alikuwa ni miongoni wanakijiji waishio kusini magharibi katika jimbo la Sichuan waliosaini makubaliano ya kumuwinga mvulana huyo mwenye umri wa miaka nane ili kulinda afya ya wanavijiji hao .
Taarifa zinaeleza kwamba mvulana huyo aliupata ugonjwa huo kutoka kwa mama yake mzazi,na aligunduliwa kwa mara ya kwanza kama ana ugonjwa huo mnamo mwaka 2011, alipokwenda kupata matibabu hospitalini baada ya kuumia.
Unyanyapaa haukuishia hapo kwa mvulana huyo kwani kila shule aliyokwenda kutaka kujiunga nayo ilia pate elimu walimkataa, na wanakijiji hawataki hata kuchangamana naye.
Na Kunkun kwa jina alilopewa la utani analalama akisema,hawataki hata kucheza nami,nacheza peke yangu, na wananiona kama bomu linalotaka kulipuka wakati wowote.
Pamoja na kumnyanyapaa na kutotaka kuchangamana naye, wanakijiji hao wanadai wanamuonea huruma,hana hatia na ni motto mdogo, lakini wakadai kuwa virusi alivyonavyo vinawatisha.
Wanakijiji hao wanadai mama wa mvulana huyo alifariki mnamo mwaka 2006,wakati baba wa mvulana huyo hajulikani alipo baada ya kujua afya ya mwanawe na hivyo kumtelekeza.

Elimu kwa jamii ya raia wa China juu ya ugonjwa wa ukimwi ni finyu,na hivyo kusababisha unyanyapaa na hofu miongoni mwao.
Wizara ya afya ya China na masuala ya uzazi wa mpango imeeleza takwimu zinazoishia mwezi October mwaka huu zinaonesha kwamba watu walioathiriwa na virusi vya ugonjwa huo ni laki nne na elfu tisini na saba,nah ii ni tangu mgonjwa wa kwanza kugunduliwa nchini humo mwaka 1985,na inakadiriwa kuwa china ina watu bilioni 1.36.
Suala la unyanyapaa dhidi ya ugonjwa huo ni changamoto inayokabili shule,hospitali,maeneo ya kazi na kwingineko nchini China,nah ii ndio sababu ya kudumaza harakati za kutambua na kupamba na virusi hivyo.

No comments:

Post a Comment