TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 20, 2014

MAAFISA WA POLISI WATAKIWA KUTUMISHA NIDHAM

indexNa Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi.
Maafisa, Wakaguzi,  na Askari wa Jeshi la Polisi hapa nchini, wametakiwa kudunisha nidhamu wakati wote, kutenda haki kwa kila mmoja na kuwaheshimu wananchi wa rika zote bila ya kujali dini, rangi ama itikadi zao kisiasa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Chuo cha Polisi Dar es Salaam, SACP Ali Lugendo, wakati akizungumza na Wanafunzi wa Mafunzo ya Uofisa (Mrakibu Msaidiizi wa Polisi) na wale wa cheti na Stashahadi ya Sayansi ya Polisi kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.
Kamanda Lugendo amesema kuwa pamoja na kufundisha masomo ya sheria na haki za binadamu, lakini kazi kubwa inayofanywa na chuo chake ni kusisitiza nidhamu kwa kila afisa na askari wanaofika chuoni hapo.
Amesema kuwa nidhamu ni somo la kwanza analofundishwa askari anapokuwa katika mafunzo ya awali kwenye chuo cha Polisi Moshi kwani amesema nidhamu ni msingi wa kwanza kwa majeshi yote duniani.
“Hakuna Jeshi lolote duniani, likiwemo Jeshi letu la Polisi hapa nchini ambalo haliendeshi kwa misingi ya nidhamu”. Alisema Kamanda Lugendo na kuongeza kuwa bila nidhamu hakuna Jjeshi.
Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Nidhamu kwenye chuo cha Polisi Dar es Salaam (Dar es Salaam Police Academy) SSP Mussa Loyd, aliwataka Maafisa hao kuwa kioo cha jamii na kuwatendea haki wananchi  bila ya upendeleo wakati wote wanapokuwa kazini katika maeneo mbalimbali.
Alisema kuwa, mbali ya kuzuia vitendo vya kuhalifu, kushuku, kupeleleza na kuwakamata watuhumiwa, lakini kazi kubwa ya Jeshi la Polisi ni kuhakikisha kuwa kila Askari anatenda haki kwa kila anayemhudumia bila ya ubaguzi ama kumuonea mmoja wao.
“tunachotakiwa kufanya sisi Polisi ni kutenda haki kwa kila mmoja bila ya kujali dini, kabila, rangi ama itikadi ya mwananchi kisiyasa maana sisi hatuna chama”. Alisema Loyd.

No comments:

Post a Comment