TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 17, 2014

TATIZO LA WAMACHINGA NA OMBA OMBA MAENEO YASIYORUHUSIWA DAR KUTAFUTIWA DAWA .

unnamed
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Mecki Sadiki akifuangua kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Dar es salaam (RCC) leo jijini Dar es salaam.Kushoto ni Katibu Tawala wa mkoa wa Dar es salaam Bi. Theresia Mmbando.
……………………………………………………………………………………………..
 Aron Msigwa –MAELEZO
.Dar es salaam.
 
Jiji la Dar es salaam linaangalia upya utaratibu wa kuwaondoa ombaomba na wafanyabiashara ndogondogo(wamachinga)  katika maeneo yasiyoruhusiwa katika jiji la Dar es salaam kufuatia sheria na hatua zinazochukuliwa ikiwemo kuwarudisha ombaomba hao katika mikoa wanayotoka kutokuzaa matunda na kuwa endelevu kufuatia wengi wao kurudi katika maeneo ya awali kila wanapoondolewa.
 
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Said Mecki Sadiki wakati akifuangua kikao cha wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Dar es salaam (RCC) kilichofanyika leo jijini Dar es salaam kujadili masuala mbalimbali ya mendeleo katika jiji la Dar es salaam.
 
Amesema kuwa kuendelea  kuwepo kwa wafanyabiashara hao katika maeneo yasiyo rasmi ni moja ya changamoto inayolikabili jiji la Dar es salaam kutokana na biashara wanazozifanya kuchangia kuzuia maeneo ya barabara ya waenda kwa miguu, kusababisha uchafuzi wa mazingira,kusabisha msongamano wa magari kwa baadhi yao kuweka bidhaa  barabarani.
 
Amesema kutokana na hali hiyo baadhi ya wafanyabiashara walio na biashara rasmi  ambao hulipa kodi za Serikali wamekuwa wakilamikia hali  ya ukwepaji wa kodi inayofanywa na wafanyabiashara hao.
 
Bw. Sadiki amesema mpango wa mkoa wa sasa ni kuendelea kuwatumia wafanyabiashara hao kama  fursa ya mtaji wa rasilimali watu ambayo itatumika kama chanzo cha mapato katika kuleta maendeleo ya mkoa.

No comments:

Post a Comment