TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 20, 2014

SAKATA LA ESCROW LIMECHANGIA KUPUNGUZA KURA ZA CCM MKOANI IRINGA

Katibu wa chama cha mapinduzi mkoani Iringa HASSAN MTENGA akiongoza makatibu wa wilaya kuongea na waandishi wa habari mkoani Iringa
………………………………………………………………………………………..
Na Fredy Mgunda,Iringa
Katibu wa chama cha mapinduzi CCM HASSAN MTENGA amekiri kuhusu sakata la fedha za tegeta ESRWO na IPTL kuwa limechangia kudondoka katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni. Akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa suala hilo lilihitaji elimu kubwa kuwaelimisha wananchi kabla ya uchaguzi huo wa serikali za mitaa.
Mtenga amesema dalili za awali kuhusu uchaguzi mkuu utakao fanyika mwakani ni nzuri kuhusu chama cha Mapinduzi na watashinda kwa kishindi kama uchaguzi wa serikali za mitaa. Aidha amezungumzia kuhusu vijana walioondoka katika chama cha mapinduzi na kujiunga na Chadema kuwa umetumika ujanja wa kuwa nunua vijana ili kupigia kura chama cha demokrasia na maendeleo Chadema. Kwa upande wa chama cha mapinduzi wilayani mufindi mkoani Iringa wameulalamikia uongozi wa serikali uliopewa dhamana ya kusimamia zoezi zima la uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo dosari nyingi zimejitokeza tofauti na chaguzi zilizopita. Akizungunza na na mtandao huu katibu wa chama hicho wilayani mufindi MIRAJI MTATARU amesema kuwa uchaguzi huu umekuwa na changamoto nyingi hivyo kupelekea ucheleshaji wa vifaa pamoja na kufanya uchaguzi kuwa kama wa kushitukiza wakati walikuwa wamejipanga kwa muda muda mrefu. MTATURU ameitaka serikali iangalie kwa makini suala hili la uchaguzi kwa kuwa kuna wananchi wengi wamekosa haki yao ya msingi kwa kuwa walishindwa kupiga kuwa kutokana na kukosekana kwa karatasi za kupigia kura.
Aidha MTATURU amewapongeza wananchi wa wilaya ya mufindi kuendelea kukipigia kura wagombea wa CCM na kuwapa ushindi wa asilimia 99 na kuwaachia wapinzania asilimia moja tu licha ya changamoto zilizojitokeza kwenye uchaguzi huo.

No comments:

Post a Comment