TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 18, 2014

MIONGOZO YA UKAGUZI KULETA MABADILIKO MIGODINI- KAMISHNA

03Kamishna Msaidizi wa Madini anayeshughulikia Ukaguzi wa Migodi, Mhandisi Ally Samaje, akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha kuandaa miongozo ya Ukaguzi wa Migodi kinachoendelea Jijini Mwanza.
01Wakaguzi wa Migodi kutoka maeneo mbalimbali nchini wakiwa katika kazi za vikundi kuandaa miongozo (checklist) itakazotumiwa na Wakaguzi wa migodi nchini katika kikao kinachoendelea Jijini Mwanza.
02 Mmoja wa washiriki wa kikao kazi cha Wakaguzi wa Migodi akiwasilisha kazi ya vikundi wakati wa kikao cha kuandaa miongozo ya Ukaguzi wa Migodi
04
Sehemu ya Wakaguzi wa Migodi waliohudhuria kikao kazi cha kundaa miongozo ya Ukaguzi wa Migodi nchini wakifuatilia mada zilizowasilishwa katika kikao hicho.
=====================================================
Na: Asteria Muhozya, Mwanza

Kamishna Msaidizi wa Madini anayeshughulikia Ukaguzi wa Migodi Mhandisi, Ally Samaje, amesifu zoezi la kuandaa miongozo (checklist) ya Ukaguzi wa Migodi na kueleza kuwa, litaleta matokeo bora kutokana na kwamba shughuli hiyo imekuwa shirikishi.
Kamishna Samaje ameyasema hayo katika kikao kazi kinachoendelea Jijini Mwanza na kuwashirikisha Wakaguzi wa migodi kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuandaa miongozo itakayokuwa nyenzo muhimu kwa shughuli za ukaguzi wa migodi nchini.
“ Kimekua ni kikao kizuri, kila mmoja ameshariki kikamilifu jambo ambalo linaashiria kuwa, tutatoka hapa tukiwa na kitu ambacho kitawezesha shughuli za ukaguzi migodini kufanyika kwa utaalamu ,” amesema Samaje.
Ameongeza kuwa, miongozo hiyo inatarajiwa kuleta mabadiliko katika shughuli za ukaguzi wa migodi, vilevile shughuli nzima itafanyika katika muonekano unaofafana kutokana na kwamba, miongozo hiyo inaandaliwa kwa ajili ya ukaguzi wa migodi yote nchini , ikiwemo na migodi mikubwa na midogo.
“Tutatoka hapa na miongozo mizuri, nina imani kwamba tutakuwa tofauti na miaka mingine. Tutaongea lugha moja katika shughuli za ukaguzi, lakini zaidi tutajenga kikosi bora kwa ajili ya shughuli za ukaguzi”, amesisitiza Samaje.
Aidha, ameongeza kuwa, uwepo kwa miongozo hiyo, utawezesha shughuli za ukaguzi migodi kufanyika kitaalamu zaidi na kuongeza kuwa, “suala jingine la kuzingatia ni kwamba uandaaji wa miongozo hii unakwenda unazingatia hali halisi ya mazingira yetu. Huku masuala ya afya,usalama na uhifadhi wa mazingira yakizingatiwa”, ameongeza Mhandisi Samaje.
Kwa upande wake, mwezeshaji katika kikao hicho, Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi, Laurian Rwebembera , akifafanua masuala kadhaa katika kikao hicho, ameeleza kuwa, miongozo hiyo inatarajiwa kuwa, shirikishi kutokana na kwamba washiriki wote wameshiriki kikamilifu katika zoezi zima la uandaaji miongozo hiyo.
“Kimekua ni kikao kazi kizuri, kila mmoja ameshiriki kuonesha uzoefu na namna bora ya kufanya ili kufikia lengo. Miongozo hii itakua nyenzo bora za kufanyia kazi, amesema Mhandisi Rwebembera.

No comments:

Post a Comment