TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, May 20, 2016

SIKU YA WAUGUZI, MUHIMBILI WAADHIMISHA SIKU YAO LEO.

SIKU YA VIPIMO DUNIANI: VIJANA WA KITANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MAFUNZO KATIKA FANI YA VIPIMO ILI KUKIDHI MAHITAJI YA AJIRA KWENYE VIWANDA, GESI NA MAFUTA


MAAFISA WA JESHI LA MAGEREZA 327 WA CHUO CHA MAGEREZA KIWIRA, MKOANI MBEYA WATUNUKIWA VYEO.












MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA RIPOTI YATOLEO LA NANE LA UCHUMI TANZANIA


TAPELI WA MADINI BANDIA JIJINI DAR ES SALAAM ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI.


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linashikilia mkazi wa Makongo, Wencelaus Mtui anayedaiwa kuhujihusisha na utapeli wa madini kwa kumtapeli mtu na kisha madini bandia yenye thamani ya Sh.Milioni 90,000.
Akizungumza na waandishi habari leo Ofisini Kwake, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina (CP),Simon Sirro amesema kuwa mtu aliyetambeliwa kiasi cha fedha hizo alilipa kupitia benki ya CRDB kwa madini bandia ya dhahabu Kilogram 20 zenye thamani ya Dola za Kimarekani 40,000.
Amesema baada ya mtu huyo kulipa fedha hizo alikabidhiwa vipande vitatu vya madini venye uzito wa Kilogram 212 na kugundua kuwa ni madini bandia.
Jeshi la polisi lilipompekuwa ofisini kwake na nyumbani kwake walimkuta ,Chuma cha kuchomea madini,Mashine ya kupima madini ,vifaa vya kubania (Seal 53) pamoja na taarifa mbalimbali za malipo ambayo ameweka benki na kutoa.
Mtui ambaye anadaiwa kuwa ni tapeli wa madini pandia anamiliki kampuni ya Crown Logistics and Cargo Handling Limiited.
Wakati huo huo jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam linamskilia Waziri Jamal (39) mkazi wa Mbezi Msakuzi ambaye wamemkamata na silaha moja aina ya Bastola Browning 6.35 Calbre yenye namba za usajili A.08416/ Car 90522 na baada ya kumhoji wameweza kubaini mtandao wao wa watu nane.
Aidha jeshi la polisi limesema kuwa askari aliyeuawa jana kwa kupigwa risasi ni wa mkoa wa pwani na kuahidi lazima watakamatwa wote waliohusika.
=============================================

MWANAFUNZI MBARONI KWA KUMTUKANA RAIS WA ZANZIBAR DKT.SHEIN PAMOJA NA MKUU WA MAJESHI MWAMUNYAGE







Wakati hayo yakiendelea mshtakiwa  wa kesi ya kumtukana Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania  John Pombe Magufuli Isaac Emily (40),  mkazi wa Olasiti jiji  hapa  inatarajiwa kuanza kusikilizwa mfululizo kuanzia Juni 5 mwaka huu katika mahakama ya hakimu mkazi Arusha.

===================================================

Wanaobadilisha taka kuwa bidhaa watambuliwe







MWANAFUNZI MBARONI KWA KUMTUKANA RAIS WA ZANZIBAR DKT.SHEIN PAMOJA NA MKUU WA MAJESHI.









Wadaiwa 21,721 wajitokeza HESLB kurejesha mikopo


Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Robert Kibona akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa agizo la siku 60 kwa wadaiwa wa Bodi hiyo na waajiri, ambapo takribani asilimia 72 ya wadaiwa wote wameshawasilisha taarifa zao. Kulia ni Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi hiyo
Mkurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Cosmas Mwaisobwa (kushoto) akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utaratibu wa urejeshaji wa mikopo kwa wadaiwa ambao mikopo yao imeshaiva. Kulia ni Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Robert Kibona.PICHA NA FATMA SALUM-MAELEZO

Na FATMA SALUM -MAELEZO

Jumla ya wadaiwa wapya 21,721 wa mikopo ya elimu ya juu wamejitokeza ili kuanza kulipa madeni yao kufuatia agizo la siku 60 lililotolewa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) mnamo Machi 14 mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Robert Kibona wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu tathmini ya agizo lililotolewa na bodi hiyo kwa wanufaika wa mikopo na waajiri ili kutimiza wajibu wao kisheria.

Bw. Kibona alifafanua kuwa jumla ya Shilingi bilioni 151.5 zinatarajiwa kurejeshwa na wadaiwa hao ambao walikopeshwa ili kuwawezesha kupata elimu yao ya juu katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi kuanzia mwaka 1994.“Lengo la agizo lilikuwa ni kuhahakisha madeni yote yaliyoiva yanakusanywa ili kuongeza uwezo wa kukopesha watanzania wengi zaidi na agizo hili limeisha Mei 13 mwaka huu.” alisema Bw. Kibona

Kwa mujibu wa Bw. Kibona, kati ya wadaiwa waliopatikana, wadaiwa 19,528 walipatikana baada ya Bodi kuchambua taarifa za waajiriwa zilizowasilishwa na waajiiri na wadaiwa wengine wapatao 2,007 walijitokeza kwa hiari.“Waajiri wana wajibu wa kisheria wa kuwasilisha taarifa za waajiriwa wao, baadhi yao walifanya hivyo katika siku hizo sitini na tukawabaini wadaiwa hao, tunawapongeza waajiri kwa ushirikiano walioutoa na wanufaika wote waliojitokeza kwa hiari” alisema Bw. Kibona.

Aidha Bw. Kibona aliongeza kuwa Bodi imeongeza siku 30 za ziada kuanzia Mei 20, 2016 kwa wadaiwa waliobaki kujitokeza na uamuzi huo umetokana na tathmini iliyoonyesha kuwa kuna idadi kubwa ya waajiri na wanufaika wanaoendelea kujitokeza. Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo Bw. Cosmas Mwaisobwa alisema kuwa kiwango cha ukusanyaji wa madeni kwa mwezi kinatarajiwa kuongezeka kutoka shilingi bilioni 2.7 zinazokusanywa hivi sasa na kufikia shilingi bilioni 8 ifikapo mwezi Juni 2016.

Katika kipindi cha mwaka 1994/1995 hadi sasa, kiasi cha shilingi trilioni 2.44 kimetolewa kwa wanufaika 378,504 wakiwemo wanafunzi wanaoendelea na masomo yao hivi sasa ambao kwa sasa hawana wajibu wa kulipa hadi pale watakapomaliza au kusitisha masomo yao. 

SERIKALI KUMLINDA MKULIMA KWA KUANZISHA VITUO VYA UNUNUZI WA MAZAO








KONGAMANO MAALUM LA WADAU KUJADILI SUALA LA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA) LAFANYIKA LEO JIJINI DAR











No comments:

Post a Comment