TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, May 15, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS JOHN MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA KUPAMBANA NA RUSHWA LONDON

MAKALA YA USAFIRI WA MABASI YAENDAYO HARAKA













RAIS DKT MAGUFULI KUWA MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA WAKADIRIAJI MAJENZI AFRIKA








sekta ya sheria kuchangia utekelezaji wa dhana ya Kuimarisha Viwanda nchini










MIVARF YAONGEZA KASI YA UKUAJI WA UCHUMI ENDELEVU CHATO










Ruzuku kwa Wachimbaji Wadogo kutolewa mwezi Septemba


Kamishna Msaidizi wa Madini anayeshughulikia Leseni, Mhandisi John Nayopa (katikati), Meneja wa TANESCO Kanda ya ziwa, Mhandisi Amos Maganga (kulia) na Mhandisi Joseph Kumburu (kushoto) wakiwa katika kikao kilichofanyika mjini Geita kilichojumusha watendaji mbalimbali katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, baadhi ya Wabunge na Wakuu wa Wilaya za mkoa huo, Wawakilishi wa Wachimbaji Wadogo na Watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO). Kikao kililenga kujadili suala la magwangala na maeneo ya Wachimbaji Wadogo.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga (kulia) na Katibu Tawala mkoa wa Geita, Selestine Gesimba (kushoto) wakiwa katika kikao kilichofanyika mjini Geita kilichojumusha baadhi ya Wabunge na Wakuu wa Wilaya za mkoa huo, Wawakilishi wa Wachimbaji Wadogo na Watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).
Baadhi ya Wakuu wa Wilaya za mkoa wa Geita, Wawakilishi wa Wachimbaji Wadogo na Watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wakiwa katika Kikao kilichofanyika mjini Geita ambacho kililenga kujadili suala la magwangala na maeneo ya Wachimbaji Wadogo kilichoongozwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, (hayupo pichani).

MIRADI YA MAENDELEO KUHIFADHIWA KWENYE KANZI DATA




SERIKALI KUKAMILISHA MAABARA NNE ZA UPIMAJI KIFUA KIKUU NCHINI.

Na Tigaya Vincent_MAELEZO-Dodoma.

Wizara ya Afrika , Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maabara nne za Kanda ili kuboresha huduma za vipimo vya upimaji wa kifuu na kifuaa kikuu sugu.Hatua hiyo inalenga kuimarisha na kusogeza huduma karibu za upimaji wa kifuaa kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Dodoma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha Bungeni hotuba kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka ujao wa fedha 2016/17.

Amezitaja hospitali hiso ambazo zitakuwa na maabara hizo kuwa ni Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Kibong’oto mkoani Kilimanjaro.Waziri Ummy aliongeza kuwa Wizara hiyo itaendelea matibabu ya kifua kikuu sugu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Bugando.

Aidha ,Waziri huyo aliongeza kuwa Wizara imefanikiwa kufikia idadi ya vituo 547 vinavyotoa huduma shirikishi za kifua kikuu na UKIMWI nchini .Hatua hii inalenga kuondoa usumbufu kwa wagonjwa wenye maambukizi mseto ya Kifuua Kikuu na UKIMWI kupata huduma sehemu moja.

Waziri Ummy aliongeza kuwa chini ya utaratibu huo , Wizara imefanikiwa kutoa huduma watu 692,642 wanaoishi na Virusi vinavyosababisha UKIMWI (WAVIU) ili kubainisha uwepo na kutokuwepo kwa maambukizi ya kifua kikuumiongoni mwao.

Alisema kuwa kati ya hao watu 26,218 waligundulika kuwa na maambukizi ya kifua kikuu na walipatiwa matibabu.Aidha , Waziri huyo alisema kuwa katika mwaka ujao wa fedha ,Wizara hiyo itaendelea kutoa huduma za matibabu ya kifua kikuu sugu kufikia hospitali kumi za mikoa ya Dar es salaam, Mbeya, Mwanza, Dodoma, Morogoro, Mtwara, Tanga, Shinyanga, Geita na Mara.

Alisema kuwa Wizara itaongeza uwezo mikoa 16 yenye viwango vya chini kabisa vya uibuaji wagonjwa wa kifua kikuu ili kuongeza kasi ya kudhibiti ugonjwa huo nchini.Katika mwaka ujao wa fedha Wizara hiyo iliomba Bunge likubali kuidhinisha makadirio ya matumizi ya Wizara pamoja na Taasisi zake yenye jumla ys shilingi 845,112,920,056.00.

Kati ya fedha hizo shilingi 317,752,653,000.00 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 527,360,267,056.00 ni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. 

MEYA NA MKURUGENZI WA TANGA WAPEWA ONYO KALI.





Na Woinde Shizza,Tanga

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeitaka halmashauri ya Manispaa ya Mji wa Tanga kuitisha vikao vya madiwani kama kawaida na kumtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo atimize wajibu wake ipasavyo kabla hajachukuliwa hatua za kisheria .

Imeelezwa kuwa haiwezekani kwa mtumishi yeyote  aliyeajiriwa na serikali ya ccm akawa mzandiki, adui na msaliti wa sera za serikali ya chama tawala.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka ameeleza hayo  wakati akizungumza na wanachama wa uvccm na ccm kwenye ukumbu wa TANU Hall mjini hapa.

Alisema ni jambo la kushanagaza kuona vikao ambavyo ndivyo vinavyotakiwa kujadili, kupanga mipango na kutekeleza program za maendeleo vikiwa haviitishwi kwa muda mrefu  kwasabahu za kipuuzi zisizo na mashiko.

"Tunasikia  Meya wa Manispaa ya Tanga kupitia ccm kwamba CUF wana mpango wa kukununua ili uhame  ccm , tunakwambia kama kuna mkakati huo kataa, CCM  ni chama kikubwa, mikono yake ni mirefu "alisems Shaka.

Shaka alimtaka Meya wa Manispaa ya Tanga Mustafa Seleboss kuhakikisha vikao hivyo vinaitishwa na chama chochote kitakachojaribu kukwamisha  uvccm watapambana nacho.

Alisema si haki wala wajibu ikiwa kikao halaki cha madiwani kimemchagua mstahiki  Meya  wa mji Tanga  kwabtaratibu halali kilifanyika na matokeo yakakipa ushindi ccm hivyo tishio lolote la vurugu au la kukwamisha maendeleo ya wananchi  halitakubalika.
"Wana ccm na uvccm acheni kulalamima kila siku kwamba kuna baadhi ya viongozi na  waliosaliti bila kuwachukulia hatua za kinidhamu na kimaadili, akipatikana msaliti kwa ushahidi kamili mtoseni ili tusonge mbele"alisema.

Aidha Shaka alisisitiza kuwa kila mtendaji au Mkurugenzi wa halmashauri ana wajibu wa kusimamia maelekezo ya kisera katika utendajikazi  wake pamoja na kufuata taratibu za kisheria husika

Kwa upande wake mstahiki Meya selebos akijibu  madai ya Sgaka alimhakikishia kuwa hakuna mpinzani au chama vjochote chenye chenye ubavu na jeuri ya kumnunua na kumtoa ccm.

Mstahiki huyo Meya alikiri kuwa ni kweli wapo baadhi ya watendaji wa ngazi za serikali wanaoonekana kuwa waasi wasiotii matakwa na utashi wa kutoitumikia serikali ya ccm kwa.

Seleboss alisema hata hivyo pamoja na vikwazo vilivyopo katika baadhi ya maeneo na kuwepo kwa watendaji  watukutu alisema anaamini serikali itachukua nafasi yake kuwakabili na kuwadhibiti.

Jumla ya wanachama wapya wa uvccm kutoka Chuo cha utumishi Kange mkoani Tanga kwa hiari yao walijiunga na umoja huo pamoja na kumtawaza rasmi kamanda mpya wa uvccm Mkoa wa Tanga Najim Senga.

No comments:

Post a Comment