TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Wednesday, February 25, 2015
Rais Jakaya Kikwete awasili Zambia
MGOGORO WA MWEKEZAJI NA WANANCHI KUHUSU SHAMBA LA MAKANGALE WAMALIZIKA
Na Masanja Mabula -Pemba .
Mgogoro wa shamba kati ya Mwekezaji na wananchi wa Shehia ya
Makangale umemalizika ambapo pande hizo zimefikia makubaliano na
kuahidi kushirikiana kulinda na kudumisha amani pamoja na kukuza kipato
chao kupitia sekta ya Utalii .
Makubaliano hayo yamefikiwa mbele
ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman ambapo Mwekezaji
Amit Ladwa amekubali kulipa fidia ya miti aina ya mivinje ambayo
imepandwa na wananchi katika shamba hilo .
Akizungumza kwenye kikao hicho
kilichofanyika kwenye ufukwe wa Vumawimbi liliko shamba , Mkuu wa Mkoa
wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman ameiagiza Idara ya Misitu na
Maliasili zisizorejesheka Pemba kuharakisha kufanya tathmini na miti
hiyo ili wananchi walipwe fidia na Mradi huo uanze kutekelezwa .
BENKI YA POSTA TANZANIA (TPB) YABORESHA ZAIDI HUDUMA KWA WATEJA BAADA YA KUJIUNGA KATIKA MTANDAO WA TTCL KATIKA MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO
Benki ya
Posta Tanzania (TPB) na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), wamekabidhiana
rasmi mradi wa huduma kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.
SHULE ZA MSINGI MKOANI SINGIDA KUPOKEA VITABU 200
Shule
tatu za msingi katika mkoa wa Singida,zitapokea vitabu 200 wiki hii
kusaidia katika mchakato wa kuboresha elimu ya shule ya msingi. Vitabu
hivi vimetolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Children’s Book
Project for Tanzania na italenga maelfu ya watoto nchini kote katika
kuwakomboa kielimu.
Akizungumza
wakati wa kukabidhi vitabu hivyo,Afisa Mipango wa Children’s Book
Project for Tanzania,Ramadhani Ali alisema kuwa Watoto wanaotakiwa
kupata vitabu hivi ni wale walio na uhitaji sana na watapata nafasi ya
kunufaika zaidi kielimu.
“Watoto
wanaopata vitabu hivi ni wale walio na uhitaji sana na watapata nafasi
ya kunufaika zaidi kielimu. vitabu hivi vinatolewa kwa watoto ili waweze
kutumia katika masoma yao ya kila siku shuleni.” alisema Ramadhani
Msaada
huu wa vitabu umejikita katika kukomboa hali ya elimu Tanzania, huku
serikali ikijitahidi kuwekaza katika elimu nchini kwa kipindi kirefu.
Inakadiriwa kuwa asilimia kubwa ya watoto wa shule ya msingi Tanzania
hawajui kusoma na kuandika,Ukosefu wa vitabu unachangia wanafunzi wa
shule ya msingi kushindwa kusoma na kuandika.
Tafiti
mbalimbali kutoka za serikali na sekta binafsi zinaonyesha wazi kuwa
kujifunza kusoma mapema ni uwekezaji katika siku zijazo kwa mtoto,kwani
elimu katika ngazi ya chini kwa mwanafunzi inachangia kuboresha maisha
yake ya baadae.
Kwa
upande wake Doris Mollel ambaye ni Balozi wa Elimu mkoani Singida
anatambua umuhimu wa elimu katika ngazi ya chini na anatumia muda wake
mwingi katika harakati za kukomboa elimu ya shule ya msingi. Ziara zake
nyingi hujikita katika mikoa ya ukanda wa kati hususani Singida na
Tanzania kwa ujumla,Vile vile ni mshauri wa wanafunzi wa shule za
msingi.
“Msingi
wa kujifunza kusoma hufungua uwezo wa kufikiri kwa mwanafunzi akiwa na
umri mdogo bila kiini hiki cha msingi maendeleo na mafanikio ya
mwanafunzi ni magumu.” alisema Doris
Doris
Mollel ni Miss Singida kanda ya kati 2014/15 na analenga katika
kuboresha maisha ya jamii kwa kupitia elimu na masuala mengine ya
kitamaduni.

Miss
Singida kanda ya kati 2014/15,Doris Mollel akisikiliza jambo kutoka
kwa Afisa Mipango wa Children’s Book Project for Tanzania,Ramadhani Ali
wakati akipokea vitabu kutoka Children’s Book Project for Tanzania.
JAMHURI KIHWELO (JULIO) AJIUNGA NA COASTAL UNION YA TANGA
Kiwelu “Julio”kulia akisisitiza jambo mazoezini jana mara baada ya
kuwasilia mkoani Tanga kuifundisha timu hiyo kushoto ni Kocha Mkuu
James Nandwa ,Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Coastal Union,Albert
Peter,Katibu Mkuu Coastal Union,Kassim El Siagi na Meneja wa Coastal
Union Akida Machai.
PATO LA MWANANCHI MBEYA LAVUKA LENGO LA KITAIFA
Ametoa pongezi hizo jana usiku
(Jumanne, Februari 24, 2015) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa huo
na wilaya zote wakiwemo wadau mbalimbali na viongozi wa dini mara baada
ya kupokea taarifa ya Mkoa wa Mbeya.
Alisema katika mipango yake,
Serikali ililenga kwamba pato la mtu kwa mwaka liwe sh. 1,186, 200,
lakini kwa sababu ya jitihada mbalimbali mkoa huo umelivuka. “Katika
taarifa aliyonisomea, Kaimu Mkuu wa Mkoa amesema wastani wa pato la
mwananchi umeongezeka kutoka sh. 711,201/- mwaka 2008 hadi kufikia sh
1,420,427/- mwaka 2013 na kwamba mkoa unachangia asilimia 7.43 ya Pato
la Taifa,” alisema.
Alisema kipato cha mtu mmoja kwa
siku ni sh. 3,891/- ambazo ni zaidi ya Dola mbili za Marekani (sh.
3,400/-). “Wakubwa hawa wanatupima kwa kuangalia kipato cha mtu kwa
siku. Wanasema nchi ni maskini iwapo watu wake wanaishi chini ya dola
moja kwa siku (sawa na sh. 1,700/-).”
MIGODI YA DHAHABU YA GEITA, BULYANHULU, BUZWAGI NA NORTH MARA KUANZA KULIPA USHURU WA HUDUMA KWA KIWANGO CHA 0.3% YA MAPATO GHAFI KWA HALMASHAURI ZA WILAYA NA MIJI
Halmashauri zitakazonufaika na
malipo hayo ni: Mji wa Geita; Wilaya ya Geita; Mji wa Kahama; Wilaya ya
Msalala; na Wilaya ya Tarime. Malipo hayo yanaanza tarehe 1 Julai, 2014.
Malipo hayo yanafuatia makubaliano kati ya Serikali na Kampuni
zinazomiliki migodi husika kufanya marekebisho kwenye Mikataba ya
Maendeleo ya Uchimbaji Madini (Mining Development Agreement – MDA) baina
ya Serikali na Migodi ya Geita, Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara
kuhusu ulipaji wa ushuru wa 0.3% ya uzalishaji kulingana na Sheria ya
Local Government Finance Act, Cap.290 Revised Editions of 2002 badala ya
Dola za Marekani 200,000 kwa mwaka zilizokuwa zikilipwa awali
Mha. Ngosi C.X. Mwihava
KAIMU KATIBU MKUU
25 Februari, 2015
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MHE. GEORGE SIMBACHAWENE AKABIDHIWA RIPOTI YA KUMTAFUTA MSHINDI WA TUZO YA RAIS YA HUDUMA ZA JAMII NA UWEZESHAJI KWA MAKAMPUNI YA UZIDUAJI NCHINI
VURUGU KUBWA IRINGA, POLISI NA WANANCHI WAPAMBANA.
Zipo taarifa za kutokea kwa vurugu kubwa katika eneo la
Ilula mkoani Iringa.Taarifa zinadai kuwa vurugu hizo ni kati ya jeshi la
polisi na wananchi wa kawaida ambao wamefunga barabara kwa kuwasha moto
wa matairi ya gari.
Aidha taarifa kutoka kwenye eneo la tukio zinaendelea
kueleza kuwa hadi sasa magari manne ya Polisi na Pikipiki moja
vimechomwa moto, huku basi linalofahamika kwa jina la Nyagawa
linalosafirisha abiria kutoka Njombe kuja Dar es Salaam likiwa
limevinjwa vioo vyote.
Taarifa hizo zinadai kuwa tayari polisi wa kutuliza ghasia
FFU wameshafika eneo la tukio na kufanikiwa kwa sehemu kutuliza ghasia
hizo, na kwamba magari yanayokuja Dar es Salaam na mikoa mingine
yameshaanza safari zake.
Ungana nasi baadaye kwa taarifa zaidi
Chanzo Mwananchi
…………………………………
PICHA KWA HISANI YA IRINGA YETU BLOG
Rais Jakaya Mrisho Kikwete apokea vitabu vya sayansi kwa shule za Sekondari vilivyochapishwa kwa msaada wa watu wa marekani
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Wilaya
ya Kinondoni Mhe Paul Makonda baada ya kuwasili katika Shule ya
Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam leo tayari kwa kukagua ujenzi wa maabara na pia kupokea na kugawa vitabu vya
sayansi vilivyochapishwa na Watu wa Marekani.
ya Kinondoni Mhe Paul Makonda baada ya kuwasili katika Shule ya
Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam leo tayari kwa kukagua ujenzi wa maabara na pia kupokea na kugawa vitabu vya
sayansi vilivyochapishwa na Watu wa Marekani.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua maabara katika Shule
ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam
ambako pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi
vilivyochapishwa na Watu wa Marekani. Wa kwanza
kulia ni Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
akifuatiwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete
ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam
ambako pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi
vilivyochapishwa na Watu wa Marekani. Wa kwanza
kulia ni Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
akifuatiwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda AANZA ZIARA YA MKOA WA MBEYA
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akitazama mafunzo kwa vitendo yaliyokuwa yakifanywa na wanafunzi wa
kidato cha kwanza katika Shule ya Sekndari ya Igomelo wilayani Mbarari
akiwa katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi mkoani Mbeya Februari 24,
2015.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda AZINDUA UANDIKISHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizindua Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura katika mji
mdogo wa Makambako Februari 24, 2015.Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva na Katikati ni Katibu wa Tume
hiyo, Ndugu Malaba.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na
Naibu Katibu Mkuu ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa CHEDEMA John Mnyika
wakitazama kadi mpya ya mpigakura baada ya Waziri Mkuu, Kuzindua
uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika mji mdogo wa
Makambako Februari 24, 2015.
Wizara yatangaza utoaji ruzuku awamu ya pili ya wachimbaji wadogo wa madini
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Matokeo ya utekelezaji wa utoaji wa ruzuku kwa wachimbaji Madini
wadogo nchini Awamu ya Pili yanatarajiwa kufanyiwa tathmini na
ufuatiliaji kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).
Hayo yamebainishwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na
Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava wakati akiongea katika Kipindi cha Jambo
Tanzania kinachorushwa kupitia Televisheni ya Taifa TBC1 mapema leo,
ambapo amefafanua kuhusu taratibu za maombi ya namna ya kupata ruzuku
kwa wachimbaji wadogo wa madini Awamu ya Pili.
Mhandisi Mwihava ameeleza kuwa, ili kupata matokeo bora ya namna
ruzuku hiyo itakavyotumiwa na wachimbaji wadogo watakaokidhi vigezo vya
maombi na kunufaika na ruzuku hiyo, mpango wa BRN utatumika ipasavyo
kuhakikisha kwamba fedha hizo zinatumika kama ilivyopangwa.
“BRN itatumika kufuatilia utekelezaji wa ruzuku. Wizarani tuna
Sehemu ya Ukaguzi wa Migodi, lakini pia tuna Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO), hawa wote watashirikiana kufanya tathmini yenye matokeo
tunayotarajia,” amesisitiza Mhandisi Mwihava.
Mhe. Said Ali Mbarouk atembelea kituo kipya cha kurushia matangazo cha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).
Ni Mnara wa kurushia matangazo wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) ulioko Bungi Wilaya ya Kati Unguja.
Ni chumba chenye mitambo ya kurushia matangazo (Transmitter) kilichopo katika Kituo cha Bungi Unguja.
MKUTANO MKUU WA TFF KUFANYIKA mkoani MOROGORO.
Hatua hiyo imefikiwa na Kamati ya
Utendaji kutokana na sababu za kutokukamilika kwa miundombinu ya mkutano
mkuu na kuwepo ka shughuli nyingine za kijamii mkoani humo.
Kamati ya Utendaji inamshukuru
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Singida (SIREFA), na
uongozi mzima kwa kujitolea kuandaa mkutano huo na huko nyuma waliweza
kuandaa mkutano wa makatibu wa vyama vya soka vya mikoa.
TFF itaandaa vikao na matukio
mengine mkoani Singida itakapotokea hapo baadae, tarehe ya mkutano mkuu
itaendelea kubakia ile ile ya Machi 14, 15 mwaka huu.
SHIRIKA LA SPECSAVER LA NORWAY Linatarajia kutoa HUDUMA YA UPIMAJI WA MACHO NA KUTOA DAWA KWA WANANCHI WA ZANZIBAR BILA MALIPO
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar,
Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na wandishi wa habari kuhusu ujio wa
madaktari wa Shirika la Specsaver la Norway ambao watatoa huduma ya
macho bila malipo kwa kushirikiana na wataalamu wazalendo wa Zanzibar
katika skuli ya Kiembesamaki.
Baadhi ya waandishi wa habari
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo (hayupo pichani)
katika mkutano huo uliofanyika Wizara ya Afya Mnazi mmoja Zanzibar.
(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
WAZIRI MKUU AZINDUA UANDIKISHAJI WAPIGA KURA KITAIFA
Ametoa wito huo leo mchana
(Jumanne, Februari 24, 2015) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali
na wananchi waliofika kushuhudia uzinduzi huo uliofanyika kwenye kata ya
Lumumba, Halmashauri ya Mji wa Makambako, mkoani Njombe.
“Ninawasihi viongozi wa siasa
tuwahimize wanachama wetu waende kujiandikisha kwa wingi. Tuache kauli
za kukatisha tamaa, tuache kauli za kejeli sababu zoezi hili ni jema na
lina nia ya kuwawezesha Watanzania wote kutumia haki yao ya kupiga
kura,” alisema.
Mkuu wa Idara ya utumishi wa umma Mpanda Bw. Peter Kijika aagwa
Picha ya pamoja wa kwanza
aliyevaa shati jekundu ni Katibu wa TSD Mkoa wa Katavi Deogratias Shija
,wa pili ni aliyekuwa Katibu wa TSD Halmashauri ya wilaya ya Mpanda
Peter Kijika,watatu ni Bi Debora Mwakaje Afisa Utumishi wa TSD,aliyevaa
shati jeupe ni Alphonce Mwakyusa Afisa Utumishi Kaimu Katibu TSD
Halmashauri ya Mpanda.
…………………………………………………………………………………..
Na Kibada Kibada -Katavi
Watumishi wa Ofisi ya Rais ,Tume
ya Utumishi wa Umma Idara ya Utumishi wa Walimu TSD Halmashauri ya
Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi imefanya hafla fupi ya kumuaga aliyekuwa
Mkuu wa Idara hiyo Bw Peter Kijika kwa kuitumikia Idara hiyo kwa
utumishi uliotukuka.
Akizungumza akizungumza katika
Hafla hiyo mgeni rasmi katika hafla hiyo Katibu (TSD) Mkoa wa Katavi
Bw,Deogratias Shija alisema kwa niaba ya Tume ya Utumishi wa Umma
alimshukuru kwa kuitumika Idara kwa utumishi wake uliotukuka.
Subscribe to:
Posts (Atom)
