Wachezaji
 tisa wa Kanembwa JKT pamoja na timu yao wanaolalamikiwa na Shirikisho 
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kumpiga mwamuzi Peter Mujaya 
wanatakiwa kujitetea mbele ya Kamati ya Nidhamuitakayokutana Jumapili (Februari 9 mwaka huu).
Utetezi
 huo unaweza kuwa wa mdomo kwa walalamikiwa kufika wenyewe mbele ya 
kamati itakayokutana saa 4 kamili asubuhi au kuuwasilisha kwa njia ya 
maandishi.
Kamati
 ilikutana jana Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko 
dhidi ya wachezaji hao na timu yao kwa tukio hilo lililotokea Novemba 2 
mwaka jana kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) dhidi ya Stand 
United FC iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Wachezaji
 hao ni Abdallah Mgonja, Bariki Abdul, Philipo Ndonde, Mbeke Mbeke, 
Mkuba Clement, Mrisho Mussa, Nteze Raymond, Ntilakigwa Hussein na Uhuru 
Mwambungu. Mlalamikiwa mwingine ambaye naye anatakiwa kujitetea ni timu 
ya Kanembwa JKT.
Ikiwa
 chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, Kamati hiyo baada ya kusikiliza
 malalamiko dhidi ya wahusika na kupokea ushahidi wa aina mbalimbali 
kutoka kwa mlalamikaji imesema ili iweze kutenda haki katika shauri hilo
 ni lazima walalamikiwa wapate fursa ya kusikilizwa.
Katika
 hatua nyingine, Kamati hiyo iliyokutana kwa mara ya kwanza tangu 
ilipoundwa imesema imesikitishwa na vitendo vya fujo ndani ya mpira wa 
miguu, na kuwataka watu wasijihusishe na aina yoyote ya fujo.
No comments:
Post a Comment