Naibu
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko Rashid Salum Ali wa
 kwanza (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar 
PBZ wa kwanza (kulia) wakitia saini makubaliano ya ubadilishanaji 
 majengo ya Taasisi hizo mbili katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya 
Benki ya Kiislamu ya PBZ Mpirani mjni Zanzibar. Katikati ni Mwenyekiti 
wa Bodi ya PBZ Abrahamani Mwinyi. 

Naibu
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko Rashid Salum Ali wa
 kwanza (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar 
PBZ wa kwanza (kulia) wakibadilishana hati ya makubaliano ya 
ubadilishanaji majengo ya Taasisi hizo mbili ambapo PBZ itachukua jingo 
la Ofisi ya Biashara ya Magari liliopo Malindi na Wizara ya Biashara 
itachukua Jengo la Makao Makuu ya sasa ya PBZ la Darajani 

Baadhi ya Maofisa wa PBZ wakiangalia utiaji saini wa makubaliano ya 
ubadilishanaji wa majengo ya Benki hiyo na iliyokuwa Ofisi ya Shirika la
 Biashara ya Magari lililochini ya Wizara ya Biashara, Viwanda na 
Masoko. 
Picha
 ya pamoja ya maafisa wa PBZ na Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko 
baada ya kumalizika hafla ya makubaliano ya ubadilishanaji wa majengo ya
 Taasisi hzo mbili iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya kiislamu ya PBZ 
Mpirani mjini Zanzibar. 
Jengo
 la Ofisi ya Biashara ya Magari liliopo Malindi Mjini Zanzibar ambalo 
limekabidhiwa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) kwa ajili ya kujenga Makao
 Makuu Mapya ya Benki hiyo. 
 
 
Jengo
 la Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) liliopo Darajani Mjini Zanzibar 
ambalo limekabidhiwa Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko. 
(Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar).



No comments:
Post a Comment