Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete 
akipokea maelezo ya hatua mbalimbali zilizofikiwa katika Ukarabati wa 
Jengo la Ofisi za Utawala za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
toka kwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi 
wa Magereza, Kibwana Kamtande (wa kwanza kushoto) alipotembelea hivi 
karibuni Mjini Dodoma(wa kwanza kulia) ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda(wa pili kulia) ni Waziri wa Sera
 na Uratibu wa Bunge. Mhe. William Lukuvi. 

Spika
 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne 
Makinda(katikati) akiwa ameongozana na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma, 
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Kibwana Kamtande kabla ya 
kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya 
Mrisho Kikwete alipotembelea kufanya ukaguzi wa Ukarabati wa Jengo la 
Ofisi za Utawala za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Mhe.
 Rais ameonyesha kuridhishwa na kasi ya ukarabati unaofanywa na Jeshi l 
Magereza kupitia Shirika lake la Magereza.
Mkuu
 wa Magereza Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza 
Kibwana Kamtande(wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na 
baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambao wanasimamia kwa 
karibu Ukarabati wa Jengo la Ofisi za Utawala za Bunge la Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania linalokarabatiwa na Jeshi la Magereza kupitia 
Shirika lake la Magereza ambapo hivi karibuni Mhe. Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameridhishwa na 
kasi ya ukarabati wa Jengo hilo alipotembelea Mjini Dodoma(Picha zote na
 Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza). 

Hatua
 mbalimbali iliyofikiwa  ya ukarabati wa Jengo la Ofisi za Utawala za 
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililopo Mjini Dodoma ambapo 
hivi karibuni Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. 
Jakaya Mrisho Kikwete alifanya ukaguzi wa Ukarabati wa Jengo hilo na 
kurudhishwa na kasi ya Ukarabati huo unaofanywa na Jeshi la Magereza 
kupitia Kikosi chake cha Ujenzi kilicho chini ya Shirika la Magereza.


No comments:
Post a Comment