TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 5, 2014

SERIKALI YASEMA HAINA UGOMVI NA VYOMBO VYA HABARI.

IMG_4746

Frank Mvungi- Maelezo
Serikali imesema haina Ugomvi na vyombo vya habari hapa nchini kama ambavyo baadhi ya vyombo
hivyo vimekuwa vikiripoti.
Akizungumza leo katika ufunguzi wa mkutano wa Maafisa Habari na Mawasiliano  wa Serikali Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara alisema haoni sababu ya kuingia kwenye ugomvi na wadau muhimu kama vyombo vya habari.
“Kuna wanaozunguka zunguka wakieleza kwamba kuna ugomvi kati yetu na vombo vya habari, mkiwasikia wapuuzeni”.alisema waziri Mukangara.
Dkt Mukangara alipongeza kazi nzuri inayofanywa na vyombo vya habari na kuvitaja kuwa wadau muhimu wa Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kutoa taarifa.
Dkt.Mukangara aliongeza kuwa ni jukumu la Maafisa Habari na Mawasiliano kuwaunganisha wananchi na Serikali kwa kutoa taarifa zitakazowasaidia wananchi kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Akifafanua zaidi Dkt. Mukangara amesema kuwa Wizara itaendelea kuratibu mikutano ya Taasisi za Serikali na Vyombo vya Habari ili kuwapa wananchi fursa ya kujua mambo mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali.
Katika Utaratibu huo  Dk Mukangara amesema mikutano 156 kati ya taasisi za Serikali na Vyombo vya Habari ilifanyika  kati ya 204 iliyotarajiwa kufanyika katika kipindi cha julai hadi Desemba 2013 ikiwa ni utekelezaji wa jukumu la msingi la kuwapa wananchi taarifa kwa wakati.
Pia aliwaasa Maafisa Habari na Mawasiliano kote nchini kujituma na kufanya kazi kwa weledi ili kuwasaidia Taifa kufikia maendeleo endelevu.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel Alibainisha kuwa Mafunzo kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii katika kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma.,mafunzo ya vitendo kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii na mada kuhusu namna bora ya kutumia na kuendesha radio za kijamii.
Kauli mbiu ya Kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano zaidi ya 100 toka Tanzania nzima ni Matumizi ya Tehama na Mitandao ya Kijamii katika kuimarisha Mawasiliano ya Serikali kwa umma.

No comments:

Post a Comment