Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala, akifungua maji ya mradi wa kisima cha maji, Chang’ombe Unubini, wilaya ya Temeke. 
 
 
Naibu
 Waziri wa Maji, Amos Makala akizungumza na wakazi wa eneo la mradi wa 
kisima cha maji cha Kichapwi, kata ya Kilakala, wilaya ya Temeke, kulia 
ni Mwenyekiti wa mtaa wa Barabara ya Mwinyi, Yahya Mnali. 
 
 
Wakazi
 wa eneo la mradi wa kisima cha maji Kichapwi, kata ya Kilakala, wilaya 
ya Temeke, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala (hayupo 
pichani). Mradi wa kisima cha maji Tabata Segerea. 
 
 
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala, akifungua maji ya mradi wa kisima cha maji, Chang’ombe Unubini, wilaya ya Temeke.
……………………………………………………………………………….
Naibu
 Waziri wa Maji, Amos Makala, leo ameendelea na ziara yake ya jijini Dar
 es Salaam kwa kukagua miradi ya visima vya maji inayosimamiwa na DAWASA
 maeneo ya Temeke na Segerea.
Mhe.
 Makala aliweza kufika kwenye miradi ya visima vya maji maeneo ya 
Chang’ombe Unubini, Kichapwi na Segerea na kuona namna miradi hii 
ilivyosaidia kutatua kwa kiasi kikubwa cha tatizo la maji katika maeneo 
hayo ya jiji.
Naibu
 Waziri aliridhika namna miradi hiyo ya kijamii, ambapo Serikali 
ikishirikiana na wananchi wameweza kutekeleza mpango wa Serikali 
kuhakikikisha inaleta ahueni kwa kutoa huduma za kuridhisha za maji 
kufikia mwaka 2015.
“Napenda
 kuwashukuru wananchi na DAWASA kwa kazi nzuri iliyofanyika katika 
miradi hii, na ni dhahiri kuwa mpango wa kutoa huduma nzuri ya maji 
jijini Dar es Salaam na nchi nzima inaendelea vizuri. Ningependa kuwaasa
 wananchi wazidi kushirikiana kwa ukaribu na Serikali ili kuhakikisha 
miradi hii inatunzwa na kuendelea kupanuka zaidi kwa ajili ya maendeleo 
ya wananchi wenyewe na nchi nzima kwa ujumla”.
Vile
 vile Mhe. Makala aliipongeza Kamati ya Jumuiya ya Watumia Maji ya Mradi
 wa Kichapwi, Kilakala, wilaya ya Temeke kwa uendeshaji mzuri wa mradi 
huo na kuweza kukusanya pesa nyingi, kiasi cha sh. Mil 11. Huku 
wakifanikiwa kufungua akaunti mbili za benki kwa ajili ya makusanyo ya 
mapato na rasilimali kama walivyoagizwa na DAWASA.
“Pamoja
 na uchanga wake, Kamati ya Maji ya Kichapwi imefanya vizuri sana katika
 kutekeleza majukumu yake na hakika ni mfano wa kuigwa nchini na kwa 
kweli wanastahili pongezi nyingi”, alisema Naibu Waziri.
Mhe.
 Makala atamaliza ziara yake ya siku tano jijini Dar es Salaam kesho, 
kwa kutembelea maeneo ya Ubungo, na baada hapo kwenda Morogoro kuanza 
ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mkoani humo.

No comments:
Post a Comment