Mgombea
 wa nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani Kupitia tiketi ya Chama 
cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema) Japhet Kembo akifurahia huku 
akipongezwa na wanachama na wapenzi wa Chadema mara baada ya kuibuka 
mshindi wa Kiti cha Mwenyekiti kwa Kupata Kura 510 huku CCM wakiwa 
wamepata kura 215 na NCCR kupata kura 205
 Mawakala
 wa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Migombani 
wakihesabu kura ambapo sanduku hilo ndio lilikuwa sanduku la mwisho 
kuhesabiwa katika Kituo cha Kupigia kura cha Migombani ambao wakazi wa 
Mtaa wa Migombani walikuwa wakisubiria matokeo
 
 Askari Polisi wakiwa katika kituo cha Kupigia Kura cha Migombani 
kwaajili ya kuimarisha ulinzi na mpaka zoezi la kuhesabu kura 
likimalizika kwa Mgombea wa Chadema kuibuka Mshindi hakuna fujo 
zilizotokea.
 Baadhi
 ya wakazi wa Mtaa wa Migombani Wakisubiria Matokeo ya Uchaguzi wa 
Serikali ya Mtaa wa Migombani ambapo mpaka matokeo yanatangazwa Chadema 
iliibuka na Kura 510, CCM ikiwa imepata kura 215 na NCCR wakiwa na kura 
205.
Baadhi
 ya wapita njia nao ilibidi wasimame maana uchaguzi huu ulivuta hisia za
 watu wengi kutokana na hali iliyoonyeshwa na wakazi wa mtaa huo kukaa 
mpaka dakika za mwisho
 Msimamizi
 wa Uchaguzi katika Kituo cha Kupigia Kura cha Migombani akitangaza 
Mshindi wa Uchaguzi huo uliomalizika kwa Mgombea wa Chadema akiwa 
ameibuka Mshindi kwa Kupata Kura 510 huku wapinzani wake wakiwa na Kura 
215 za CCM na Kura 205 za NCCR
 Wakazi
 wa Mtaa wa Migombani wakishangilia ushindi mara baada ya Mgombea wa 
Chadema Kutangazwa Mshindi wa Kiti cha Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani
 Wakazi wakishangilia kwa Ushindi,
 Mgombea
 wa Nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani Japhet Kembo (Kushoto 
aliyenyoosha mkono) akipongezwa na wakazi wa Mtaa wa Migombani kwa 
kuibuka Mshindi wa uchaguzi
 Wakazi
 wa Mtaa wa Migombani Segerea wakishangilia mara baada ya mgombea wao 
kuibuka mshindi katika kinyanganyiro hiko.Picha Zote na Josephat Lukaza 
wa Lukaza Blog
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment