TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Wednesday, February 4, 2015
Establish an inclusive multi-stakeholder Education
PINDA AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA DINI
MULTICHOICE YAZINDUA KING’AMUZI KIPYA CHA DStv HD
Meneja Uhusiano wa MultiChoice
Tanzania, Barbara Kambogi (Katikati) akifafanua jambo kwenye mkutano na
wanahabari (hawapo pichani), wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa
king’amuziki kipya cha DStv HD leo jijini Dar. Kulia ni kwake
ni Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na
kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu.
Na Andrew Chale
KAMPUNI ya MultiChoice Tanzania
wasambazaji wa ving’amuzi vya DStv, leo imezindua king’amuzi kipya
cha DStv HD ambacho kitaanza kutumika kwa mara ya kwanza hapa Nchini.
Akizungumza na wandishi wa habari
mapema leo jijini Dar es Salaam, Meneja Uendeshaji wa MultiChoice
Tanzania, Ronald Shelukindo, akielezea umuhimu wa huduma hizo alisema
king’amuzi hicho kina ubora wa hali ya juu ikiwemo kuonyesha picha zenye
ubora mzuri zaidi.
Pia alieleza kuwa, DStv HD mteja atapata kuona picha zenye mvuto zaidi pamoja na kiwango cha juu cha sauti Dolby Digital 5.1.
“Wateja wa DStv watafurahia
ving’amuzi hivi kwa ubora wa hali ya juu hivyo ni wakati wa
kuchangamkia ofa kwani ndio mara ya kwanza kuingia kwa Tanzania”
alisema Ronald Shelukindo.
Meneja uendeshaji wa
Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akielezea ubora wa king’amuzi
hicho cha DStv HD wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari leo
jijini Dar.
Ronald Shelukindo akielezea kwa
kina, alisema DStv HD, mteja anaweza kufurahia vipindi mbalimbali
ikiwemo mifumo na mipangilio ya kila vipindi kwa kupendekeza atazame
kipi gani, muda gani na wakati gani?.
Bunge laridhika na hali ya ulinzi na usalama wa raia
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali la mbunge Bungeni Dodoma.
Wamiliki wa shule za sekondari watakiwa kuzingatia viwango vya ufaulu
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Anna Kilango Malecela akijibu swali la Mh. Joseph Selasini Mbunge wa Rombo.
Mbunge la Mbunge wa Rombo Joseph Selasini, akiuliza swali.
Serikali yajenga barabara zenye urefu wa kilometa 42 mji wa Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akijibu swali Mbunge Bungeni.
………………………………………………………………………………..
Na Lorietha Laurence-Maelezo , Dodoma
SERIKALI kupitia mradi wa uendelezaji miji (TSCP) imefanikiwa
kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 42 kwa mji wa Dodoma kwa msaada
wa mfuko wa Benki ya Dunia.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge,
Jenista Mhagama ameeleza hayo Bungeni Dodoma, kuwa ujenzi huo wa
barabara umehusisha pia ujenzi wa mifumo ya maji ya mvua ,dampo la
kisasa kwa kijiji cha Chidaya pamoja na mitambo y usombaji taka.
Serikali ya Tanzania yapokea takribani shillingi bilioni 15.5 kutoka Uganda
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima.
………………………………………………………………………………………….
Na Lorietha Laurence-Maelezo Dodoma
Serikali ya Tanzania imepokea takribani shillingi bilioni 15.5 kutoka Serikali ya Uganda ikiwa ni fidia itokanayo na athari za vita vya Kagera.
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima ameeleza hayo Bunge mjini Dodoma kuwa fidia iliyokuwa inatakiwa kulipwa ni Dola za Marekani milioni 18.4 ingawa Uganda imelipa Dola milioni 9.7 zilizoingizwa kwenye mfuko mkuu wa Hazina.
“Kiasi hicho cha fedha kilipokelewa na kuwekwa katika Mfuko Mkuu wa Hazina kwa ajili ya matumizi ya maendelao ya wananchi ” alisema Malima.
Alibainisha kuwa taratibu za fidia zitokanazo na hasara za vita hiyo zinaongozwa na sheria na kanuni za kimataifa pamoja na utaratibu wa kutathmini kiwango cha hasara kitokanacho na vita.
Aliongeza kuwa licha ya kwamba vita hivyo viliathiri taifa zima la Tanzania ,mkoa wa Kagera umepokea fedha kutoka Mfuko Mkuu wa serikali ambayo imesaidia kusukuma maendelao ya wananchi.
Serikali ya Tanzania imepokea takribani shillingi bilioni 15.5 kutoka Serikali ya Uganda ikiwa ni fidia itokanayo na athari za vita vya Kagera.
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima ameeleza hayo Bunge mjini Dodoma kuwa fidia iliyokuwa inatakiwa kulipwa ni Dola za Marekani milioni 18.4 ingawa Uganda imelipa Dola milioni 9.7 zilizoingizwa kwenye mfuko mkuu wa Hazina.
“Kiasi hicho cha fedha kilipokelewa na kuwekwa katika Mfuko Mkuu wa Hazina kwa ajili ya matumizi ya maendelao ya wananchi ” alisema Malima.
Alibainisha kuwa taratibu za fidia zitokanazo na hasara za vita hiyo zinaongozwa na sheria na kanuni za kimataifa pamoja na utaratibu wa kutathmini kiwango cha hasara kitokanacho na vita.
Aliongeza kuwa licha ya kwamba vita hivyo viliathiri taifa zima la Tanzania ,mkoa wa Kagera umepokea fedha kutoka Mfuko Mkuu wa serikali ambayo imesaidia kusukuma maendelao ya wananchi.
Tanzania Early Childhood Development Network (TECDEN) Your partner in child Care, Parenting and Support
This Network was established in
year 2000 and officially registered in 2004. The headquarters of the
Network are based in Dar es Salaam. To date 2015, the Network has a
total of more than 200 members’ organizations in 14 Administrative
regions of Tanzania Mainland and Zanzibar.
1. Goal:
The Network aimed at improving the livelihood of young children in Tanzania through provision of various services to enable them grow to their full potentials.
The Network aimed at improving the livelihood of young children in Tanzania through provision of various services to enable them grow to their full potentials.
2. Objectives.
2.1 Advocating for rights of young children and other issues that affecting young children in Tanzania
2.2 Mobilizing community members to actively participate in promoting early Childhood development in Tanzania through National campaign which is investing to a young child for National Development 2.3 Coordinating information sharing among stakeholders on issues affecting young children in Tanzania 2.4 Conducting research and situational analysis for the purpose of generating evidence based facts to feed Advocacy work to issues affecting young children in Tanzania.
2.2 Mobilizing community members to actively participate in promoting early Childhood development in Tanzania through National campaign which is investing to a young child for National Development 2.3 Coordinating information sharing among stakeholders on issues affecting young children in Tanzania 2.4 Conducting research and situational analysis for the purpose of generating evidence based facts to feed Advocacy work to issues affecting young children in Tanzania.
Ujumbe wa Taasisi ya Kijerumani ya Hanns Seidel Foundation watembelea Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma
ZIARA YA RAIS WA UJERUMANI ZANZIBAR
RAIS JAKAYA KIKWETE AMUANDALIA RAIS WA UJERUMANI DHIFA YA KITAIFA YA CHAKULA CHA USIKU, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Jakaya Kikwete(wa pili kutoka kulia) na mgeni wake Rais wa Shirikisho la
Ujerumani, Joachim Gauck (wa tatu kutoka kulia) wakifurahia wakati wa dhifa ya kitaifa ya
chakula cha usiku aliyomwandalia
kiongozi huyo jana usiku, Ikulu
jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mke wa Rais wa Tanzania, mama Salma Kikwete na
Mke wa Rais wa Ujerumani Bi. Daniella Schadt.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt.
Jakaya Kikwete(wa pili kutoka kulia) akiwa na mgeni wake Rais wa
Shirikisho la
Ujerumani, Joachim Gauck (wa tatu kutoka kulia) wakiwa wamesimama wakati
wimbo taifa wa Tanzania na ujerumani ulipopigwa wakati wa dhifa ya
kitaifa ya
chakula cha usiku aliyomwandalia
kiongozi huyo jana usiku, Ikulu
jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mke wa Rais wa Tanzania, mama Salma Kikwete na
Mke wa Rais wa Ujerumani Bi. Daniella Schadt.
Tuesday, February 3, 2015
WAMILIKI WA VIWANDA WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADADISI WA SENSA YA VIWANDA.
Mkuu wa chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika kilichopo eneo la
Changanyikeni jijini Dar es salaam Prof.Ngalinda Innocent akizungumza na
wadadisi watakaokusanya takwimu za Sensa ya Viwanda mwezi huu wakati wa
ufunguzi wa mafunzo ya siku 14.Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Maria Bilia akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya wadadisi 200 wa Sensa ya Viwanda itayofanyika nchi nzima mwezi huu. Mafunzo hayo yanafanyika chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika kilichopo eneo la Changanyikeni jijini Dar es salaam.
MWISHO.
Msanii wa Muziki Juma Nature, Aomba Msaada Wa Kuwanusuru Wasanii
Nyota na msanii mkongwe wa muziki wa bongo flava nchini
Tanzania, Juma Nature amesema kuwa wasanii wakongwe wa muziki huo
watapotea kabisa katika ramani ya muziki kama wadau wa muziki pamoja na
vyombo vya habari havitawapa nafasi ya kutosha kama wanavyopewa wasanii
wengine wa sasa.
Nature amesema kuwa zamani kipindi yeye yupo Bongo Records wasanii
wote walikuwa kitu kimoja na kazi zao walikuwa wanafanya kwa
kushirikiana na kwa umoja kitu ambacho kilifanya wote kuwa na mafanikio
sawa kwani hata maonesho yao walikuwa wanagawana fedha sawa kitu
kisichowezekana kwa sasa.
Nature amesema kuwa kwa sasa wasanii kama yeye watapotea kutokana na
wadau wa muziki kuwatumia wasanii wachache katika shughuri zao za kila
siku huku akitolea mfano jinsi Diamond anavyopewa kipaumbele katika
maonesho na kazi nyingine huku wasanii wazuri kama Rich Mavoko na Ali
Kiba wakisahaulika kitu kinachosababisha kuwa na matabaka kwani
wanaopewa nafasi ndio wanaofanikiwa.
Katika hatua nyingine Juma Nature amewaasa wadau wa muziki
kutowasahau wakongwe wa muziki nchini kwani wao ndio walioufikisha
muziki huu hapa ulipofika.
Monday, February 2, 2015
RAIS WA UJERUMANI JOACHIM GAUCK AWASILI NCHINI USIKU HUU.
Rais wa Ujerumani Mh. Joachim Gauck akiwa ameambatana na mkewe Bibi
Schadt akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere usiku huu jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib
Bilal (kulia) akiwa mwenye furaha mara baada ya kumpokea Rais wa
Ujerumani Mh. Joachim Gauck na Mkewe Bibi Schadt (walioshika maua),
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
WAZIRI WA UJENZI DKT. MAGUFULI AKAGUA BARABARA MKOANI MBEYA NA RUKWA.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John
Pombe Magufuli amewahakikishia wakazi wa mji wa Tunduma mkoani Mbeya kuwa Serikali
itajenga barabara ya njia nne katika mji huo ili kupunguza msongamano wa magari
na kuuwezesha mji huo kuwa wa kisasa na kibiashara.
Amesema hayo katika ziara
yake ya ukaguzi wa miradi ya barabara inayoendelea katika mikoa ya Mbeya na
Rukwa ambapo akiwa mjini Tunduma amekutana na wananchi wanaofanyabiashara
katika mji huo.
“Dumisheni umoja,amani na
mshikamano ili mfanye biashara zenu na kukuza uchumi nasi tutahakikisha
tunajenga barabara ya njia nne ili kupunguza msongamano wa magari na kuuwezesha
mji wa Tunduma kuwa wa kisasa na kibiashara na hivyo kuwa mahali pazuri pa watu
kuishi”,amefafanua waziri Magufuli.
Katika ziara hiyo waziri Magufuli
amekagua mizani ya Nkangamo na barabara ya Tunduma –Sumbawanga KM 225, iliyojengwa
kwa kiwango cha lami na kuwataka wananchi wa mkoa wa Rukwa kutumia barabara hiyo
kukuza uchumi wao na wa mkoa wao kwa kufanyakazi kwa bidii.
Akihutunbia wananchi wa
Sumbawanga Waziri Dkt. Magufuli amewataka wananchi kutambua kuwa barabara za
lami zinajengwa kwa gharama kubwa hivyo wazitumie kwa manufaa na wale walioko
kwenye hifadhi ya barabara wabomoe nyumba zao mapema ili kuwezesha ujenzi
kufanyika kwa wakati.
Waziri Magufuli amesema Serikali
iko katika hatua za awali kujenga barabara ya Matai-Kasesha KM 50 kwa kiwango
cha lami ili kuunganisha mkoa wa Rukwa nan chi ya Zambia na hivyo kuvutia
wawekezaji wengi kuwekeza mjini Sumbawanga na hivyo kutoa fursa za ajira na
uchumi kwa wananchi.
Waziri Magufuli yuko
katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya barabara katika mikoa ya Mbeya,Rukwa,Katavi
na Tabora ambako kuna miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara za lami
inayoendelea.
Imetayarishwa
na kitSengo cha habari na mawasiliano serikalini wizara ya ujenzi.
RAIS WA UJERUMANI KUWASILI LEO USIKU , MAANDALIZI YA MAPOKEZI YAKE YAKAMILIKA.

Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam, Said Meck Sadiki amewaomba wakazi wa jiji la Dar es salaam kujitokeza
kwa wingi katika mapokezi ya Rais wa Shirikisho la Ujerumani Mh.Joachim
Gauck anayetarajiwa kuwasili nchini
Tanzania leo usiku kwa ziara ya kikazi ya siku tano.
Akizungumzia ujio wa
rais huyo ofisini kwake leo jijini Dar
es salaam Mh. Meck Sadiki amesema kuwa rais Joachim Gauck na msafara wake
atawasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere majira
ya saa 2.30 usiku na kulakiwa na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
Ameeleza kuwa mapokezi
rasmi ya rais huyo yatafanyika kesho katika viwanja vya Ikulu majira ya saa 3
asubuhi ambapo rais huyo akiwa na mwenyeji wake atapata fursa ya kukagua
gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake na Jeshi la Wananchi wa Tanzania
na kupigiwa mizinga 21.
Amesema kuwa akiwa
nchini Tanzania Rais Joachim Gauck atakuwa na mazungumzo ya faragha na Rais
Jakaya Kikwete, Ikulu jijini Dar es salaam na baadaye kufanya mazungumzo na
baadhi ya viongozi wa Vyama vya hiari, uongozi wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani pamoja na kukutana na
wafanyabiashara wa Dar es salaam.
Amefafanua kuwa
Februari 4, 2015, Rais huyo ataelekea Zanzibar ambapo atakutana na kuwa na
mazungumzo na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na viongozi wengine wa
Serikali.
Aidha kabla ya
kuhitimisha ziara yake nchini Tanzania
Februari 6, 2015 rais huyo wa Shirikisho la Ujerumani atatembelea mbuga
ya wanyama ya Serengeti ,Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mahakama ya Kimataifa ya Haki za Binadamu
jijini Arusha.
Wageni wabainika wakitengeneza Filamu bila Kibali
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi Joyce Fisoo( wakwanza kushoto) akitoa ufafanuzi kuhusu filamu hiyo
iliyokuwa ikirekodiwa na raia wa Norway katika Ofisi ya Bodi ya Filamu mwishoni
mwa wiki.
Raia hao wa Norway katika picha wakiwa
katika kikao kuhusu filamu waliyokuwa wakirekodi kwenye Ofisi ya Bodi
ya Filamu hivi karibuni.
BODI YA MICHEZO YA BAHATI NASIBU YAKABIDHI LESENI KWA KAMPUNI YA MURHANDZIWA KUENDESHA MICHEZO HIYO
Mkurugenzi
Mkuu wa Bodi ya Michezo ya bahati nasibu , Bw Abbass Talimba
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya
kukabidhi leseni ya kuendesha bahati nasibu ya Taifa kwa Kampuni ya
Murhandziwa.
Bodi
ya Michezo ya bahati nasibu ya Taifa leo imetoa leseni ya kuendesha
Bahati nasibu ya Taifa kwa Kampuni ya Murhandziwa ambayo itakuwa
ikiendesha bahati nasibu hiyo hapa nchini ambapo Bahati nasibu hiyo
itaanza mnamo tarehe 4 Julai 2015.Bei ya tiketi zitakazouzwa itagharimu
shilingi za Kitanzania shilingi 500 kwa kila tiketi.
Baadhi
ya viongozi wa Kampuni ya Murhandziwa pamoja na viongozi wa Bodi ya
Michezo ya Bahati nasibu ya Taifa wakitazama video ya Mwenyekiti wa
kampuni ya Kampuni ya Murhandziwa amaye hakuweza kufika kwenye hafla hiyo
Subscribe to:
Posts (Atom)











