TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 30, 2013

KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA GNSM CONTRACORS CO. LTD INAYOENDESHA NA GEOFREY MUNGAI YATOA MSAADA WA CHAKULA CHA MWAKA MPYA KWA YATIMA TOSAMAGANGA



Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai akiwa na  watoto  yatima  wa  kituo  cha Tosamaganga  wilaya ya Iringa jimbo la kalenga ambako alifika kukabidhi msaada wa chakula chenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 1.5 kwa ajili ya mwaka mpya kwa  watoto hao 

Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  akiwa karibu na gari  lililobeba msaada  wa  chakula 
Baadhi ya watoto  yatima  wa  kituo cha Tosamaganga  Iringa  wakiwa  wamepumzika 
Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia akiwa amemshika mmoja kati ya  watoto yatima kituo cha Tosamaganga kushoto ni diwani wa  viti maalum tarafa ya Kalenga Shakra  Kiwanga  ambae  alikuwa ni  mwenyeji wa Mungai katika  kukabidhi msaada  wa chakula  kwa  yatima hao
Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  akiwa na mmoja kati ya  watoto yatima  wa  kituo cha  Tosamaganga  Iringa leo 
Mlezi  wa  watoto  hayo Sisita Herena  Kihwele  kushoto  akiwa na  ugeni  uliofika  kituoni Tosamaganga kwa ajili ya  kushuhudia  tukio la Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia kukabidhi msaada wa chakula  xcha mwaka mpya kwa  watoto kituoni hapo 
Watoto  hao yatima   wakiimmba  mbele ya ugeni 
Mtoto  aliyefahamika kwa  jina la Nyota  akimsalimia Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  ambae  alifika  kituoni hapo leo  kuwapa watoto hao chakula cha sikukuu ya mwaka  mpya ,mtoto  huyo alitelekezwa porini na mzazi  wake baada ya  kujifungua kabla ya  kituo  hicho kumuokota na kumtunza kituoni hapo 
Baadhi ya  yatima  kituo cha Tosamaganga 

Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia  akiwa na mlezi wa  kituo hicho sisita Herena  Kihwele 
Diwani  wa  viti maalum tarafa ya  Kalenga  Shakra  Kiwanga  kulia akimpongeza Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia kwa kusaidia  yatima
Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai kulia akikabidhi msaada  wa chakula na  vitu mbali mbali vyenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 1.5 kwa mlezi wa  kituo cha watoto  yatima cha  Tosamaganga Sisita  Herena Kihwele 
Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia  akiwa na wadau mbali mbali  walioongozana  kukabidhi misaada kwa yatima kituo cha Tosamaganga  leo 
Watoto  yatima  wa  kituo cha Tosamaganga  wakimpongeza Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia kwa kuwajali kwa  mwaka  mpya 

Diwani  wa  viti maalum tarafa ya  Kalenga  Shakra  Kiwanga  kushoto  akimpongeza Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa Ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia kwa kusaidia  yatima
 Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa ya  GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai   amekabidhi  msaada  wa chakula  cha mwaka  mpya chenye thamani  ya  zaidi ya Tsh milioni 1.5 kwa  kituo cha kulelea  watoto yatima  cha  Tosamaganga katika   jimbo la kalenga wilaya ya  Iringa vijijini .
Akikabidhi  msaada  huo  leo  Mungai  alisema  kuwa  amelazimika  kufika katika  kituo  hicho  ambacho  kinasimamiwa na masisita  wa kanisa la RC  kama  sehemu ya  mwendelezo wa kampuni  yake kuendelea  kuzungukia  vituo mbali mbali vya kulea yatima  na  kuwapa faraja  hasa katika msimu huu wa sikikuu.
Alisema  kuwa miongoni mwa vituo ambavyo amepata  kuvikumbuka katika msimu  huu wa sikukuu ya Krismas na Mwaka mpya ni pamoja na  kituo cha Daily Bread Life (DBL) kilichopo jimbo la Iringa mjini na kituo hicho cha Tosamaganga  kilichopo jimbo la Kalenga huku lengo likiwa ni  kuwakumbuka  yatima  hao  na  kuihamasisha  jamii  kuelekeza nguvu  zao kwa  yatima kama  hao.
Bw  Mungai alisema  kuwa   takwimu  za maambukizi ya VVU katika  mkoa  wa Iringa zimeendelea  kuongezeka na iwapo  jamii haitajenga  utamaduni  wa kujali  yatima  vifo vya watoto  yatima ambao watakosa chakula baada ya kupoteza wazazi  wao kwa VVU pia  vitazidi  kuongezeka   hivyo lazima  misingi  ya  kuwajali  yatima ikaanzwa kuwekwa mapema  zaidi. 
” Hawa  watoto  iwapo  jitihada za vituo vya  kusaidia yatima visinge kuwa na moyo huo  leo yawezekana  baadhi yao  wasingekuwepo hapo  tungekuwa  tumewazika  ila kazi nzuri  ya  kujitolea  inayofanywa na vituo  vya yatima  ndio  imewafikisha hapa leo ….hivyo lazima  sisi kama  jamii  kuunganisha  nguvu zetu na vituo vya yatima”
Pia  alisema  kuwa  hata  viongozi  wa vyama vya siasa na serikali ni vema wakaweka utaratibu  wa  kufanya ziara  za mara kwa mara katika  vituo  vya yatima na  kujifunza mazingira ambayo  watoto hao  wanaishi ikiwa ni  pamoja na  kusaidia  kutatua changamoto  zinazovikabili vituo vya yatima mkoani Iringa .
Kwani  alisema kwa upande wake kama  mkandarasi ambae amekuwa akifanya kazi ya ujenzi wa barabara  mkoani Iringa na nje ya mkoa ameona  ni vema  katika fedha  kiasi ambazo anazipata  kuweka utaratibu wa kusaidia watoto yatima kama njia ya  kuwahamasisha pia wenzake  kujitoa kwa yatima  katika maeneo yao ama  kusaidia kuchangia maendeleo ya maeneo yao. 
Katika  hatua  nyingine Mungai aliwapongeza  walezi  wa  vituo vya  yatima katika mkoa  wa Iringa kuwa kutokana na mchango wao  wa kulea yatima hata  idadi ya yatima  na  watoto wa mitaani katika mji wa Iringa imeonekana  kupungua zaidi  
Kwa  upande  wake  diwani  wa viti  maalum tarafa  ya Kalenga Shakra  Kiwanga  akimpongeza  Mungai  alisema  kuwa ameonyesha upendo mkubwa kwa  yatima  hao na kuwataka makandarasi  wengine  kuiga mfano  huo. 
Kiwanga  ambae pia ni mmoja kati ya makandarasi wadogo mkoani Iringa alisema  kuwa alichofanya Mungai ni somo kwao pia katika kutoa sehemu ya makusanyo wanayoyapata  kupitia kazi mbali mbali. 
Awali mlezi  wa  kituo  hicho Herena Kihwele  alisema kuwa kituo hicho kina  watoto zaidi ya 100 na  kuwa kwa  sasa kituo kinakabiliwa na changamoto kubwa ya kushindwa  kuwalipia ada  sekondari   watoto zaidi ya 10  waliofaulu darasa la  saba ila kituo hakina uwezo wa  kuwasomesha . 
Iwapo umeguswa kuchangia  kituo hicho ada ama msaada  wowote  ule waweza  kuwasiliana na mlezi wa kituo hicho Sisita Herena Kihwele kwa simu  0768831477 pia  waweza  kutumia namba hiyo kwa kutuma M-PESA.

No comments:

Post a Comment