BAO 
pekee la kiungo mtata wa Wekundu wa Msimbazi, Simba sc, Amri Ramadhan 
Kiemba limetosha kuibuka na pointi 3 muhimu za kwanza usiku jana katika 
mechi yao ya kwanza  kombe la Mapinduzi 2014 iliyoanza kutimua vumbi leo
 hii viwanja viwili vya Amaan, Unguja na Gombani, Pemba.
Mgeni
 rasmi katika mchezo huo alikuwa kocha wa Timu ya Taifa ya  Italia, 
Cesare Prandelli ambaye alikagua timu zote na kwenda katikati ya dimba 
la Amaan na kuudunda mpira ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa michuano ya 
mwaka huu.
Mchezo
 huo wa kundi B ulioanza majira ya saa 2:00 usiku ndio uliochaguliwa 
kuwa wa ufunguzi katika michuano ya mwaka huu ambayo ni maalumu 
kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
![]()  | 
Amri Kiemba amewaliza AFC Leopard  
 | 
Fundi
 Kiemba aliyeanzia benchi leo hii na kuingia dakika ya 47 kuchukua 
nafasi ya Kiungo mpya wa Simba aliyesajiliwa kutoka Mtibwa Sugar dirisha
 dogo mwaka jana, Awadh Juma Issa, alifunga bao hilo baada ya kuuwahi 
mpira uliookolewa na beki wa AFC Leopard kufuatia Amisi Tambwe kujaribu 
kuunganisha krosi maridadi uliochongwa na Ramadhan Singano `Messi` 
dakika ya 77 ya mchezo.
`Messi`
 huyu mtoto ni nuksi tupu!, alifanya vitu vyake vya Nani Mtani Jembe 
baada ya kumlamba chenga ya aibu beki mrefu zaidi na mkongwe, Joseph 
Shikokoti na kupiga krosi iliyosababisha bao hilo muhimu.
Ushindi
 wa leo kwa Simba sc umewapatia nguvu zaidi katika harakati zao za 
kuusaka ubingwa ambao kwa mara ya mwisho kuutwaa ni mwaka 2011.
Kwasasa Azam fc ndio mabingwa watetezi mara mbili mfululizo, yaani walitwaa `ndoo` hiyo 2012 na 2013.
Hata 
hivyo imekuwa neema kwa kocha msaidizi wa Simba, Suleiman Matola `Veron`
 ambaye alisimama kwenye benchi la ufundi wakati akimsubiri bosi wake 
Mcroatia, Zdravko Logarusic ambaye atawasili kesho Zanzibar.
Mechi
 ya leo ilijigawa kwa timu zote kwani Leopard walicheza vizuri dakika 45
 za kwanza, lakini Simba SC walichachamaa kipindi cha pili na kucheza 
soka safi, lakini kukosa umakini kwa washambuliaji wa klabu hiyo 
kumewanyima ushindi mnono.
Simba
 sasa wanashika nafasi ya pili kundi B wakijikusanyia pointi tatu sawa 
na KCC ya Uganda wenye pointi 3, lakini wao wanawastani mzuri wa mabao 
ya kufunga.
Kikosi
 cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Issa Rid, Joseph 
Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haruna Chanongo, Ramadhani 
Chombo/Uhuru Suleiman dk89, Amisi Tambwe/Betram Mombeki dk81, Ramadhan 
Singano, Awadhi Juma/Amri Kiemba dk47.
AFC 
Leopard; Martin Masalia, Etenesy Augustin, Abdallah Juma, Saleh Jackson,
 Joseph Shikokoti, Imbalebala Martin, Okwemba Charles, Mussa Mude, Kelly
 Jacb, Mang’ole Benard/Seda Edwin dk86 na Oscar Kadenge/Hassan Mohamed 
dk86.
Awali
 katika dimba hilo, mabingwa wa Zanzibar KMKM walilala kwa mabao 3-2 
dhidi ya KCC kutoka nchini Uganda katika mchezo wa Kundi A.
Mabao
 ya KCC yalifungwa na Herman Waswa dakika ya 10, Tony Odur katika dakika
 ya 20 na William Waoro dakika ya 82, wakati ya KMKM yalifungwa na 
Hamisi Ali dakika ya saba na Maulid Ibrahim dakika ya 79.
Huko uwanja wa Gombani, Pemba, vijana wa Juma Mwabusi, Mbeya City wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Clove Stars. 
Bao la Mbeya City lilifungwa dakika ya 13 na Deus Kaseke, lakini dakika ya 24 kipindi hicho cha kwanza, Clove Stars.

No comments:
Post a Comment