TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, January 2, 2014

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA MWANALIBENEKE MPALULE SHAABAN

Kwanza kabisa Napenda kuchukua nafasi hii Kumshukuru sana Mwenyezi Mungu Mwingi Wa Rehema Kwa Kuweza Kunijalia Uwezo,Nguvu na Afya na Bahati Pia ya Kuweza Kufika Mwaka 2014, Siwezi Kujidanganya Wala Kudanganya Kuwa nimefika Hapa Leo Mnamo tarehe 1 Jan 2014 Kwa ujanja wangu au uwezo hapana Nimefika hapa Kwa Neema Na Rehema Zake Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema, Na pIa sio Kwasababu ameniwezesha Kuuona na kuingia leo tarehe 1 Jan 2014 basi mimi ni mwema, msafi na mtiifu sana mbele zake kuliko wengine hapana Ila Ni Kwa Neema na Makusudi yake Pia Wapo waliopenda kuiona Siku kama ya Leo Lakini kwa mapenzi yake Muumba Hawakuweza kufika na Pia wapo walioweza Kufika lakini wakiwa sio wazima Kiafya Na Sio kwamba wao ni wakosaji sana mbele za Mungu hapana Bali yote hayo Hutokea Kwa Makusudi yake na
Mipango yake Pia.

Tuna kila sababu ya Kumbuomba Mwenye Mungu Mwingi wa Rehema Kila Dakika itupitayo na Sio Kusubiri Mwaka Mpya ndio Tumuombe, Tuna kila sababu ya kufanya kila siku iendayo kwake basi iwe ni Mwaka Mpya Kwake Kwa Kuomba, Kusali na KUmwabudu maana ni yeye Pekee ndiye Muweza wa Kila Jambo.

Napenda Kuchukua Nafasi hii Kuwatakia Watanzania wote na Dunia Nzima wakiwemo Wazazi Wangu, Ndugu zangu, kaka zangu, Dada zangu ,Wajomba, Mashangazi, Mama Wadogo, baba Wadogo, Marafiki zangu, Watembeleaji wa Blogu zenu wote, Marafiki zenu, Ndugu zenu, Bila kuwasahau Maadui zangu Wote maana na wao pia ni sehemu ya mimi kupata mafanikio madogo sana maana Usijisifie Kuwa Unaweza kukimbia Sifa pia Kilichokukimbiza au aliyekukimbiza pia…Kwa Kuweza Kufika Mwaka 2014 wakiwa na afya na wazima wa afya, Na Hata wale waliokuwa wagonjwa Basi Mwenyezi Mungu Awatie Nguvu ili waweze kupona na Kurejea majumbani Mwao wakitokea Mahospitalini kwaajili ya Kuungana na Familia zao pia.

Mwaka 2014 umeanza ikiwa ndio siku ya Kwanza kabisa ya Mwaka 2014, Tuzidi Kumuomba Mungu Mwingi wa Rehema Azidi Kutuepusha na Kutupigania katika Vita ya Kiroho dhidi ya Mwovu Shetani na Mawakala zake kama CHuki, Roho Mbaya, Majungu, Masimango, Uchawi, Na vingine vingi vya namna hiyo.

Vilevile napenda Kuchukua nafasi Hii Kuwashukuru wote kwa kuendelea Kuwa nami katika Kipindi hiki chote cha Mwaka 2013 na naomba tuendelee kushikamana, Kupendana, Kuombeana Mazuri na yenye heri na Kuweza Kufika Pale tulipojiwekea malengo yetu tena Kwa Mwaka 2014.

Namwomba Pia Mwenye Mungu Mwingi wa Rehema Azidi kunipa Nguvu, Afya , Hekima na Busara katika Kazi zote za halali nizifanyazo na hatimaye kuweza kufanikiwa hadi pale apendapo yeye nifike.

Mwisho Nachukua Nafasi hii Kuwatakia Wote Heri ya Mwaka Mpya 2014. Tufanye kazi Kwa Bidii na Tuzidi Kumuomba Yeye Kwa Ni yeye ndie atupaye Nguvu na kututia uwepesi wa Kila Jambo

No comments:

Post a Comment