TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 30, 2013

MABIBO BEER YADHAMINI MAADHIMISHO YA MIAKA MITANO YA UPIGAJI DISCO NCHINI!!

001 
 Ma Dj wakitoa burudani wakati wa kusherekea miaka mitano ya Grooveback Djs ambayo inaundwa na Ma Dj maarufu nchini,  Dj Peter Moe, PQ, Crucial, KT, Tony na JB, iliyofanyika katika bar maharufu ya East 24  iliyoko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Ma Dj waalikwa wa kimataifa waliokuwepo ni Dj Pinye na Dj Nijo kutoka Kenya. Grooveback wanapiga Disco la nguvu kila jumamosi East 24 Bar, Arcade House, chini ya udhamini wa Windhoek Lager – 100% PURE BEER.002Mashabiki mbalimbali wakipata burudani wakati wa Kusherekea miaka mitano ya Grooveback Dj003  
Mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Mabibo, Jerome Rugemarila (katikati), akiwa na warembo wa kampuni hiyo.004 
Wana habari Dotto Mwaibale (kushoto), Faustine Kapama (katikati), wakiwa na mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Mabibo, Boniface.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla hiyo,  Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Mabibo, Kelvin Coster alisema muitikio wa wapenzi wa muziki ulikuwa ni mkubwa.
 
“Mashabiki ni wengi mno waliofika kushiriki sherehe hii ya kutimiza miaka mitano ya upigaji muziki wa disco” alisema Coster.
Alisema kampuni hiyo iliamua kudhamini sherehe hiyo kupitia kinywaji cha Windhoek kinachopendwa na watu wengi kutokana na ubora wa kimataifa na bei yake kuwa nafuu.
 
” Napenda kusisitita kuwa Windhoek ni bia ambayo ukinywa haileti matatizo yoyote kama ya kuumwa kichwa,  mnywaji akiamka asubuhi atajisikia vizuri pasipo mzingio wa ziada” alisema Coster.
Alisema wanywaji wanapaswa kuzingatia kunywa bia yenye namba MB66 ambayo inauzwa kwa chupa sh.3,000 na katoni kwa sh.58,000 ambapo faida yake ni sh.14,000 na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment