TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 11, 2015

Baraza la Ujenzi Endelevu na Mazingira Tanzania (Tanzania Green Building Council ) latambulisha shughuli zake nchini

Rais wa Baraza la Ujenzi Endelevu na Mazingira Tanzania (Tanzania Green Building Council ), Ngwisa Mpembe (wa pili kulia) akilitambulisha baraza hilo la kitaalamu ambalo Shirika la Nyumba la Taifa ni mmoja wa waasisi wake kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) mojawapo wa majukumu ya Baraza hilo ni kushawishi, kuratibu na kusimamia ujenzi wa nyumba za kisasa zilizo rafiki wa mazingira. Baraza lina wadau wengi wakiwamo Wasanifu Majenzi , Wakadiriaji majengo, wahandisi watengenezaji vifaa na watumiaji wa vifaa. Machi 19-20 mwaka huu, Baraza kwa kushirikiana na wadau mbalimbali litafanya Kongamano la Kwanza la Ujenzi Endelevu na Mazingira jijini Arusha litakaloshirikisha wadau zaidi ya 400 kutoka pembe mbalimbali za Dunia. Kushoto ni Ipyana Moses Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Green Building Council, Makamu wa Rais wa Baraza hilo, Farizan d’Avezac de Moran na Mike T’chawi wa Chama cha Wasanifu Majengo.
 Bango lililoonyesha maandalizi ya mkutano utakaofanyika Machi 19-20 mwaka huu huko Arusha

Viongozi wa Tanzania Green Building Council wakijadiliana jambo kwenye  mkutano na waandishi wa habari kulitambulisha baraza hilo la kitaalamu ambalo Shirika la Nyumba la Taifa ni mmoja wa waasisi wake kwa waandishi wa Habari.
Viongozi wa Tanzania Green Building Council wakijadiliana jambo kwenye  mkutano na waandishi wa habari kulitambulisha baraza hilo la kitaalamu ambalo Shirika la Nyumba la Taifa ni mmoja wa waasisi wake kwa waandishi wa Habari.
Ipyana Moses Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Green Building Council akizungumza kwenye  mkutano na waandishi wa habari kulitambulisha baraza hilo la kitaalamu ambalo Shirika la Nyumba la Taifa ni mmoja wa waasisi wake kwa waandishi wa Habari kulia kwake ni Makamu wa Rais wa Baraza hilo, Farizan d’Avezac de MoranRais wa Baraza la Ujenzi Endelevu na Mazingira Tanzania (Tanzania Green Building Council ), Rais wa Baraza la Ujenzi Endelevu na Mazingira Tanzania (Tanzania Green Building Council ) Ngwisa Mpembe na Mike T’chawi wa Chama cha Wasanifu Majengo.

No comments:

Post a Comment