TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, February 12, 2015

TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA YAENDESHA MAFUNZO YA SIKU MBILI KWA KAMATI ZA MAADILI ZA MIKOA YA RUKWA KATAVI

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Jaji Kakusulo Sambo akisoma hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo mapema leo tarehe 12 Februari 2015. Mafunzo hayo ya siku mbili yanayoshirikisha Mikoa ya Rukwa na Katavi yanafanyika Mkoani Rukwa. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya na Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Ibrahim Msengi. 
Jaji wa Mhakama Kuu ambae pia ni Mkuu wa Chuo cha Mahakama Lushoto Jaji Ferdinand Wambali akiendesha mafunzo hayo ambayo yameanza leo tarehe 12 Februari na yatamalizika kesho tarehe 13 Februari 2015 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa (RDC).
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Ibrahim Msengi akitoa shukurani za Mikoa ya Rukwa na Katavi kwa kuletewa mafunzo hayo ambayo ni muhimu kwa Kamati za maadili za Mikoa hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake ya siku.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Ndugu Iddi Kimanta (wa kwanza) na Katibu Tawala Wilaya Kalambo Bi Mapinduzi Severian ambao ni Wajumbe wa Kamati ya maadili Mkoa wa Rukwa wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati za maadili Mkoa wa Rukwa na Katavi wakifuatilia mafunzo hayo.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa (wa kwanza) na wajumbe wengine wa Kamati za Maadili Mikoa ya Rukwa na Katavi wakifuatilia mafunzo hayo.
Mafunzo yakiwa yanaendelea.
Picha ya pamoja.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa@Rukwareview.blogspot.com)

No comments:

Post a Comment